Lee
JF-Expert Member
- Jul 31, 2013
- 44,001
- 150,526
Mfanyabiashara maarufu wa Zanzibar na Mwanasiasa ambaye aliwahi kuwa Mwakilishi Jimbo la Uzini Mkoa wa Kusini Unguja, Mohamed Raza amefariki dunia leo wakati alipokuwa akipatiwa matibabu Hospitalini Jijini Dar es Salaam.
Taarifa za msiba huo zimethibitishwa na mmoja wa Wanafamilia aitwae Mohammed Ibrahim Raza ambapo maziko yatafanyika leo Kisutu Dar es salaam.
Itakumbukwa May 09,2023 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali alimtembelea Mohamed Raza baada ya kulazwa Hospitalini Jijini Dar es salaam. View attachment 2650702
Baada ya mvutano wa kimakataba wa muda mrefu kati ya Yanga SC na Mchezaji Feisal Salum hatimaye leo suala hilo limefikia tamati baada ya Yanga kumuuza Mchezaji huyo kwa Azam FC.
Taarifa rasmi ya Yanga SC imesema wamepokea ofa kutoka Azam FC na kuamua kumuuza Mchezaji huyo baada ya makubaliano ya pande zote mbili.
Feisal anaenda Azam FC kwa ada ya uhamisho ambayo hata hivyo bado haijatajwa ambapo amekuwa nje ya uwanja takribani kwa miezi sita… toka 24/12/2022 alipoandika barua ya kuomba kuvunja mkataba na Yanga. View attachment 2650701




Tumekumiss pia dear mimi huyu nistaafu makapukuMakapukuu nimewamicc mnoo
Dear shuu, magazeti huweki? Au umestaafu??
![]()

haiwezi tokea kipenzi hili ndio jukwaa langu pendwa panda juu utaona magazeti na habari mchanganyikoNjoo mlimani hapa sheikh.Mnalewa wapi ? Niko hapa King D
Shunie Hujambo mama.Una nini lakini ex babeebu muamala usome basi
![]()