Makapuku Forum

Makapuku Forum

Djigui Diarra's game by numbers vs USM Alger:

56 touches
29/39 accurate passes
10/19 accurate long balls
5 saves
2 high claims
1 penalty saved
1 clean sheet
Screenshot_20230604_122957.jpg
 
Ndege iliyotolewa na Rais @samia_suluhu_hassan kupeleka msafara wa Yanga nchini Algeria na kuwarudisha nyumbani tayari imewasili Algiers tangu usiku wa jana, asubuhi hii msafara mzima upo uwanja wa ndege wakicheck in ili kuanza safari ya kurejea Tanzania.

Ndege ya @airtanzania_atcl imetulia ikisubiri safari ya kurejea ambapo safari itaanza saa saba mchana huu ikiwa ni saa tano asubuhi jijini Algiers.
Screenshot_20230604_123305.jpg
 
Uongozi wa Klabu ya Yanga umewatangazia Mashabiki wa Klabu hiyo kwamba Klabu hiyo pamoja na Mashabiki waliosafiri nao pamoja kwenda kuishangilia Algeria watatua Tanzania saa tatu usiku.

Meneja Habari na Mawasiliano wa Klabu hiyo, Alli Kamwe @alikamwe amesema “Yanga Tutaondoka Algeria saa 5;00 asubuhi (Sawa na saaa 7:00 mchana kwa saa za Tanzania) na tunatarajia kutua nyumbani saa 3:00 Usiku

Itakumbukwa kwamba licha ya kuifunga USM Alger bao moja kwa sifuri hapo jana kwenye mchezo wa marudiano, Yanga ilishindwa kubeba kombe kutokana na faida ya ushindi wa USM Alger ugenini ambapo katika mchezo uliopigwa Dar es Salaam USM waliibuka kidedea 2-1.
Screenshot_20230604_123627.jpg
 
Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameipongeza Yanga SC kwa hitimisho la mchezo wa Fainali ya Kombe la Shirikisho hapo jana dhidi ya USM Alger nchini Algeria ambapo amesema historia iliyoandikwa na Timu hiyo katika safari ya michuano hiyo ni kubwa na ya heshima kwa Taifa la Tanzania.

Rais Samia amesema “Hongereni sana Yanga kwa hitimisho la mchezo wa Fainali ya Kombe la Shirikisho (CAF Confederation Cup), historia mliyoandika katika safari yenu ya michuano hii ni kubwa na ya heshima kwa Taifa letu, nawatakia kheri katika mipango yenu ya siku zijazo”

Itakumbukwa kwamba licha ya kuifunga USM Alger bao moja kwa sifuri hapo jana kwenye mchezo wa marudiano, Yanga ilishindwa kubeba kombe kutokana na faida ya ushindi wa USM Alger ugenini ambapo katika mchezo uliopigwa Dar es Salaam USM waliibuka kidedea 2-1.
Screenshot_20230604_123834.jpg
 
Watu 25 wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mbozi baada ya kunywa pombe ya kienyeji katika Kijiji cha Halambo Kata ya Halungu Wilaya ya Mbozi Mkoani Songwe.

Akiongea na @ayotv_ Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbozi, Dkt Keneth Lesilwa amesema kuwa Watu hao walifikishwa Hospitalini hapo juzi Ijumaa wakiwa dhaifu “Walianza kupatiwa huduma ya matibabu tangu juzi, wapo 25 na kati yao Wanawake wapo 13 na Wanaume wapo 12, kwa sasa hakuna vifo ingawa bado haijabainika kuwa pombe hiyo ilikuwa na kitu gani”

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe (RPC), Theopister Mallya amesema kuwa Watu hao walikuwa kwenye msiba ambapo walipotoka walikwenda kwenye kilabu cha pombe wakanunua pombe na baada ya kunywa asubuhi walianza kuumwa wengine kutapika na kuharisha ndipo wakapelekwa Hospitali.

“Tumechukua mabaki ili kuyapaleka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kubaini kama pombe hiyo ilikuwa na sumu au lah, mpaka sasa hakuna Mtu yoyote anayeshikiliwa mpaka pale tutakapopata majibu ya mabaki yaliyochukuliwa"
Screenshot_20230604_123954.jpg
 
Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Anthony Mavunde ameahidi kusimamia na kumaliza kero ya upimaji wa ardhi iliyopo eneo la Michese na maeneo mengine ya kata ya Mkonze ili kusaidia urahisi wa upatikanaji wa huduma mbalimbali za maji,umeme na barabara ambapo kwa kiasi kikubwa vinakwamishwa na kusuasua zoezi la upimaji ardhi.

Mavunde ameyasema hayo jana Juni 3, 2023 katika viwanja vya Shule ya Msingi Michese wakati wa mkutano wa kusikiliza kero za wananchi.

“Najua kumekuwa na kero ya muda mrefu ya zoezi la upimaji ardhi ambalo pia limechelewesha zoezi la upitishaji wa mabomba ya maji,huduma ya umeme kwa kuwa maeneo mengi hayajatambuliwa,tumekubaliana jumamosi tarehe Juni 10, 2023 kufanyike kikao cha wananchi na watu wa Jiji upande wa ardhi tumalize hili jambo hili mkae kwa amani katika maeneo yenu,”amesema

Screenshot_20230604_124133.jpg
 
Rais Samia Suluhu ameipa Yanga maua yake kwa kushinda nafasi ya pili Kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC).

Katika taarifa aliyoitoa leo kwenye mtandao wa Twitter ameandika; "Historia mliyoandika katika safari yenu ya michuano hii ni kubwa na ya heshima kwa Taifa letu,"

Yanga imeshika nafasi hiyo baada ya kutoa sare ya mabao 2-2 na USM Alger na mshindi kuamuliwa kwa mabao ya ugenini ambapo Yanga ilikubali kichapo cha mabao 2-1 Dar.
Screenshot_20230604_124326.jpg
 
Mshambuliaji wa Yanga, Fiston Mayele amefanikiwa kutwaa kiatu cha ufungaji Bora wa michuano ya kombe la Shirikisho akimaliza na mabao saba na kuasisti mara tatu.

Mayele anaiweka Yanga katika ramani za juu za CAF licha ya kushindwa kutwaa taji hilo baada ya kufika fainali kwa mara ya kwanza na kuonyesha kiwango bora katika mashindano hayo.
Screenshot_20230604_124518.jpg
 
Mshambuliaji wa Yanga, Fiston Mayele amefanikiwa kutwaa kiatu cha ufungaji Bora wa michuano ya kombe la Shirikisho akimaliza na mabao saba na kuasisti mara tatu.

Mayele anaiweka Yanga katika ramani za juu za CAF licha ya kushindwa kutwaa taji hilo baada ya kufika fainali kwa mara ya kwanza na kuonyesha kiwango bora katika mashindano hayo.View attachment 2645745

Kombe lipo wapi
 
Huyu ndie Cindy Le Coeur wa bendi ya Koffi Olomide !

Ukisikia sauti yake kwenye nyimbo kama Ikea ama Etoile D'Etat ama Lili Kaniki hata kama ulikuwa unakaribia kukata roho unaweza kuishi siku mbili au tatu zaidi. Huyu anaitwa Cindy. Jina lake halisi ni Candy Kunku.

Kabla ya mwaka 2007, Cindy alikuwa mwana kwaya akiimba nyimbo kanisani huko Congo kama walivyo wanamuziki wengi wa Congo. Mwaka huo au wa nyuma yake Koffi Olomide aliondokewa na wanamziki wake tegemeo hasa Fally Ipupa na Fere Gora hata hivyo huyu wa pili alikuwa hajaitumikia sana band ya Quartier Latin. Huo ndio wakati ambao mwanamzuki huyu mchanga, mwenye sauti laini na ya kuvutia masikioni aliacha kumwimbia Yesu. Akachukuliwa na Koffi. Kwa sababu ilikuwa ni nyota tayari, mawingu yalipoondoka ikaendelea kung'aa.

Koffi hakutumia nguvu sana kumfanya mwanamke huyu kung'ara.Cindy akaimbishwa, akaimba. Akachezeshwa, akacheza. Akatunga na kuimba mwenyewe. Kuanzia album ya Bord Ezanga Kombo mpaka wimbo wa hivi majuzi wa Je te Jure, Cindy anang'ara. Cindy anajua kupanda na kushuka. Unachoweza kusema ni kwamba mwanamke huyu anajua kuimba. Tena amebarikiwa sauti ya kuvutia.

Nje ya Koffi Olomide na kundi lake la Quartier Latin Cindy hajawa huru. Pengine anabanwa kama Koffi alivyofanya kwa wanamziki wake wengine kabla ya Cindy. Cindy ametoa album moja ambayo nyimbo zote pamoja na Remixes ni utunzi wa Koffi Olomide. Hata hivyo inasemwa semwa kwamba mwanamama huyu ambaye sasa ni mama wa mtoto mmoja pengine wana mahusiano mengine zaidi ya mziki na bosi wake Koffi Olomide.

Kwa sasa Cindy ndie Mkurugenzi wa bendi, yaani baada ya Koffi Olomide yeye ndie Boss. Ikea ndio wimbo wa kwanza uliomtambulisha alipojiunga na bendi ya Koffi Olomide. Ukisikiliza wimbo wa Egerie huwezi kuacha kujiuliza kwa nini Cindy bado yuko chini ya Koffi Olomide. Koffi Olomide anamwita Cindy Malkia wa Nyota. Hata hivyo wapenzi wa muziki huko Congo wanajiuliza maswali zaidi ya elfu moja, kwanini mwanamzuki huyu hana boyfriend!?

Pichani ndie Cindy akiwa na bosi wake Kofi Olomide..!
Screenshot_20230605_222817.jpg
 
Kifo cha Pepe Kale
Ilikuwa majira ya mchana, tarehe 29 November mwaka 1998 ndipo radio za kimataifa zilitangaza kifo cha Pepe Kale. Mwamba, mwanaume aliyekuwa na kilo zake nyingi tu na urefu kama unaotajwa katika Biblia alifariki kwa ugonjwa wa moyo katika Hospitali ya Ngaliema huko Kinshasa. Wakati dunia inatangaziwa kwamba Pepe Kale, amefariki kwa ugonjwa wa moyo, huko Congo kulikuwa na habari nyingine kwenye vijiwe vya kahawa na vilabu vya pombe. Wacongo kama walivyo waafrika wengine, walikuwa wanasema ushirikina na ndagu ndio ilikuwa chanzo cha kifo cha Pepe Kale.

Pepe Kale alifariki akiwa na umri wa miaka 46 tu, mwili wake ulionekana wa kizee lakini umri alikuwa bado kabisa. Huko Congo ilikuwa inasemwa kwamba Pepe Kale alikuwa amepewa masharti na mganga wake. Kila alipokuwa anataka kutoa albamu mpya alikuwa anajifungua bafuni kwa muda wa siku tatu. Huko bafuni alikuwa anakuwa kama mtu aliyekufa na kuoza, funza na mende wanamjaa kwenye mwili. Baada ya hizo siku 3 alikuwa anaamka tena na kwenda kuachia albamu yake. Na hiyo album ilikuwa moto na kuvuma dunia nzima. Hayo ndio yalikuwa masharti ya mganga. Sasa, wakongo wanaendelea kusema katika vijiwe vya kahawa, kwamba mwaka huo Pepe Kale alikuwa anajiandaa tena kutoa albamu yake. Akawa ameenda bafuni tena, bahati mbaya mfanyakazi wake wa ndani alikuwa hajui masharti hayo. Siku hiyo mfanyakazi akaenda kufanya usafi bafuni. Alipofika akamkuta Pepe Kale akiwa kama mtu aliyeoza, funza zimejaa mwilini, ndipo yule binti alipopiga kelele kuomba msaada. Na hiyo ndiyo ikawa imesababisha kifo cha Pepe Kale.

Afrika watu wengi ambao huwa wanafanikiwa hata kama wanafanya kazi kwa bidii na maarifa bado mafanikio yao huwa hayaachwi kuambatanishwa na uchawi ama ushirikina. Pepe Kale alifikia mafanikio kutokana na kujituma na kuandaa mziki mzuri. Kwa mtu mwenye uzito kama aliokuwa nao Pepe Kale, sio ajabu kwamba kifo huwa kinatokea katika umri mdogo. Alikuwa na kilo 150. Licha ya hayo yanayosemwa lakini historia imeandika Pepe Kale alipata mshtuko wa moyo tarehe 28 Novemba akiwa nyumbani kwake na kukimbizwa kwenye Hospitali ya Ngaliema huko Kinshasa ambako usiku wa tarehe 29 aliaga dunia...!
Screenshot_20230605_223145.jpg
 
Mshambuliaji wa Yanga, Fiston Mayele amefanikiwa kutwaa kiatu cha ufungaji Bora wa michuano ya kombe la Shirikisho akimaliza na mabao saba na kuasisti mara tatu.

Mayele anaiweka Yanga katika ramani za juu za CAF licha ya kushindwa kutwaa taji hilo baada ya kufika fainali kwa mara ya kwanza na kuonyesha kiwango bora katika mashindano hayo.View attachment 2645745
Tuendelee kutetema auntie.
 
Huyu ndie Cindy Le Coeur wa bendi ya Koffi Olomide !

Ukisikia sauti yake kwenye nyimbo kama Ikea ama Etoile D'Etat ama Lili Kaniki hata kama ulikuwa unakaribia kukata roho unaweza kuishi siku mbili au tatu zaidi. Huyu anaitwa Cindy. Jina lake halisi ni Candy Kunku.

Kabla ya mwaka 2007, Cindy alikuwa mwana kwaya akiimba nyimbo kanisani huko Congo kama walivyo wanamuziki wengi wa Congo. Mwaka huo au wa nyuma yake Koffi Olomide aliondokewa na wanamziki wake tegemeo hasa Fally Ipupa na Fere Gora hata hivyo huyu wa pili alikuwa hajaitumikia sana band ya Quartier Latin. Huo ndio wakati ambao mwanamzuki huyu mchanga, mwenye sauti laini na ya kuvutia masikioni aliacha kumwimbia Yesu. Akachukuliwa na Koffi. Kwa sababu ilikuwa ni nyota tayari, mawingu yalipoondoka ikaendelea kung'aa.

Koffi hakutumia nguvu sana kumfanya mwanamke huyu kung'ara.Cindy akaimbishwa, akaimba. Akachezeshwa, akacheza. Akatunga na kuimba mwenyewe. Kuanzia album ya Bord Ezanga Kombo mpaka wimbo wa hivi majuzi wa Je te Jure, Cindy anang'ara. Cindy anajua kupanda na kushuka. Unachoweza kusema ni kwamba mwanamke huyu anajua kuimba. Tena amebarikiwa sauti ya kuvutia.

Nje ya Koffi Olomide na kundi lake la Quartier Latin Cindy hajawa huru. Pengine anabanwa kama Koffi alivyofanya kwa wanamziki wake wengine kabla ya Cindy. Cindy ametoa album moja ambayo nyimbo zote pamoja na Remixes ni utunzi wa Koffi Olomide. Hata hivyo inasemwa semwa kwamba mwanamama huyu ambaye sasa ni mama wa mtoto mmoja pengine wana mahusiano mengine zaidi ya mziki na bosi wake Koffi Olomide.

Kwa sasa Cindy ndie Mkurugenzi wa bendi, yaani baada ya Koffi Olomide yeye ndie Boss. Ikea ndio wimbo wa kwanza uliomtambulisha alipojiunga na bendi ya Koffi Olomide. Ukisikiliza wimbo wa Egerie huwezi kuacha kujiuliza kwa nini Cindy bado yuko chini ya Koffi Olomide. Koffi Olomide anamwita Cindy Malkia wa Nyota. Hata hivyo wapenzi wa muziki huko Congo wanajiuliza maswali zaidi ya elfu moja, kwanini mwanamzuki huyu hana boyfriend!?

Pichani ndie Cindy akiwa na bosi wake Kofi Olomide..!View attachment 2647312
Hivi huyu kahawa kaoa?
 
Kifo cha Pepe Kale
Ilikuwa majira ya mchana, tarehe 29 November mwaka 1998 ndipo radio za kimataifa zilitangaza kifo cha Pepe Kale. Mwamba, mwanaume aliyekuwa na kilo zake nyingi tu na urefu kama unaotajwa katika Biblia alifariki kwa ugonjwa wa moyo katika Hospitali ya Ngaliema huko Kinshasa. Wakati dunia inatangaziwa kwamba Pepe Kale, amefariki kwa ugonjwa wa moyo, huko Congo kulikuwa na habari nyingine kwenye vijiwe vya kahawa na vilabu vya pombe. Wacongo kama walivyo waafrika wengine, walikuwa wanasema ushirikina na ndagu ndio ilikuwa chanzo cha kifo cha Pepe Kale.

Pepe Kale alifariki akiwa na umri wa miaka 46 tu, mwili wake ulionekana wa kizee lakini umri alikuwa bado kabisa. Huko Congo ilikuwa inasemwa kwamba Pepe Kale alikuwa amepewa masharti na mganga wake. Kila alipokuwa anataka kutoa albamu mpya alikuwa anajifungua bafuni kwa muda wa siku tatu. Huko bafuni alikuwa anakuwa kama mtu aliyekufa na kuoza, funza na mende wanamjaa kwenye mwili. Baada ya hizo siku 3 alikuwa anaamka tena na kwenda kuachia albamu yake. Na hiyo album ilikuwa moto na kuvuma dunia nzima. Hayo ndio yalikuwa masharti ya mganga. Sasa, wakongo wanaendelea kusema katika vijiwe vya kahawa, kwamba mwaka huo Pepe Kale alikuwa anajiandaa tena kutoa albamu yake. Akawa ameenda bafuni tena, bahati mbaya mfanyakazi wake wa ndani alikuwa hajui masharti hayo. Siku hiyo mfanyakazi akaenda kufanya usafi bafuni. Alipofika akamkuta Pepe Kale akiwa kama mtu aliyeoza, funza zimejaa mwilini, ndipo yule binti alipopiga kelele kuomba msaada. Na hiyo ndiyo ikawa imesababisha kifo cha Pepe Kale.

Afrika watu wengi ambao huwa wanafanikiwa hata kama wanafanya kazi kwa bidii na maarifa bado mafanikio yao huwa hayaachwi kuambatanishwa na uchawi ama ushirikina. Pepe Kale alifikia mafanikio kutokana na kujituma na kuandaa mziki mzuri. Kwa mtu mwenye uzito kama aliokuwa nao Pepe Kale, sio ajabu kwamba kifo huwa kinatokea katika umri mdogo. Alikuwa na kilo 150. Licha ya hayo yanayosemwa lakini historia imeandika Pepe Kale alipata mshtuko wa moyo tarehe 28 Novemba akiwa nyumbani kwake na kukimbizwa kwenye Hospitali ya Ngaliema huko Kinshasa ambako usiku wa tarehe 29 aliaga dunia...!View attachment 2647319
Sikua nafahamu hili kuhusu pepe kale, asante kwa kushare.

Ila hata kama ni uchawi au ushirikina huyu mwamba mziki wake ulitushika kwakweli, nimekumbuka miaka ile ya 95 na 2000 mwanzoni hakuna harusi iliyofanyika bila nyimbo za pepe kale awilo nk.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom