”
Mshambuliaji wa Yanga, Fiston Mayele amefanikiwa kutwaa kiatu cha ufungaji Bora wa michuano ya kombe la Shirikisho akimaliza na mabao saba na kuasisti mara tatu.
Mayele anaiweka Yanga katika ramani za juu za CAF licha ya kushindwa kutwaa taji hilo baada ya kufika fainali kwa mara ya kwanza na kuonyesha kiwango bora katika mashindano hayo.View attachment 2645745
USMA MABINGWA SHIRIKISHO AFRIKA
.
FT: USM ALGER0-1
YANGA SC
07’—️ Djuma Shaban
Agg (2-2)
.
View attachment 2645723














Tuendelee kutetema auntie.Mshambuliaji wa Yanga, Fiston Mayele amefanikiwa kutwaa kiatu cha ufungaji Bora wa michuano ya kombe la Shirikisho akimaliza na mabao saba na kuasisti mara tatu.
Mayele anaiweka Yanga katika ramani za juu za CAF licha ya kushindwa kutwaa taji hilo baada ya kufika fainali kwa mara ya kwanza na kuonyesha kiwango bora katika mashindano hayo.View attachment 2645745
Hivi huyu kahawa kaoa?Huyu ndie Cindy Le Coeur wa bendi ya Koffi Olomide !
Ukisikia sauti yake kwenye nyimbo kama Ikea ama Etoile D'Etat ama Lili Kaniki hata kama ulikuwa unakaribia kukata roho unaweza kuishi siku mbili au tatu zaidi. Huyu anaitwa Cindy. Jina lake halisi ni Candy Kunku.
Kabla ya mwaka 2007, Cindy alikuwa mwana kwaya akiimba nyimbo kanisani huko Congo kama walivyo wanamuziki wengi wa Congo. Mwaka huo au wa nyuma yake Koffi Olomide aliondokewa na wanamziki wake tegemeo hasa Fally Ipupa na Fere Gora hata hivyo huyu wa pili alikuwa hajaitumikia sana band ya Quartier Latin. Huo ndio wakati ambao mwanamzuki huyu mchanga, mwenye sauti laini na ya kuvutia masikioni aliacha kumwimbia Yesu. Akachukuliwa na Koffi. Kwa sababu ilikuwa ni nyota tayari, mawingu yalipoondoka ikaendelea kung'aa.
Koffi hakutumia nguvu sana kumfanya mwanamke huyu kung'ara.Cindy akaimbishwa, akaimba. Akachezeshwa, akacheza. Akatunga na kuimba mwenyewe. Kuanzia album ya Bord Ezanga Kombo mpaka wimbo wa hivi majuzi wa Je te Jure, Cindy anang'ara. Cindy anajua kupanda na kushuka. Unachoweza kusema ni kwamba mwanamke huyu anajua kuimba. Tena amebarikiwa sauti ya kuvutia.
Nje ya Koffi Olomide na kundi lake la Quartier Latin Cindy hajawa huru. Pengine anabanwa kama Koffi alivyofanya kwa wanamziki wake wengine kabla ya Cindy. Cindy ametoa album moja ambayo nyimbo zote pamoja na Remixes ni utunzi wa Koffi Olomide. Hata hivyo inasemwa semwa kwamba mwanamama huyu ambaye sasa ni mama wa mtoto mmoja pengine wana mahusiano mengine zaidi ya mziki na bosi wake Koffi Olomide.
Kwa sasa Cindy ndie Mkurugenzi wa bendi, yaani baada ya Koffi Olomide yeye ndie Boss. Ikea ndio wimbo wa kwanza uliomtambulisha alipojiunga na bendi ya Koffi Olomide. Ukisikiliza wimbo wa Egerie huwezi kuacha kujiuliza kwa nini Cindy bado yuko chini ya Koffi Olomide. Koffi Olomide anamwita Cindy Malkia wa Nyota. Hata hivyo wapenzi wa muziki huko Congo wanajiuliza maswali zaidi ya elfu moja, kwanini mwanamzuki huyu hana boyfriend!?
Pichani ndie Cindy akiwa na bosi wake Kofi Olomide..!View attachment 2647312
Ebu niache auntieTuendelee kutetema auntie.
Ameoa miaka 29 iliyopita najua auntie ulikiwa haujazaliwaHivi huyu kahawa kaoa?

mkewe anaitwa aliya aliana
Kwema mzeeiyaaa habari yakoWazee kwema?
Sikua nafahamu hili kuhusu pepe kale, asante kwa kushare.Kifo cha Pepe Kale
Ilikuwa majira ya mchana, tarehe 29 November mwaka 1998 ndipo radio za kimataifa zilitangaza kifo cha Pepe Kale. Mwamba, mwanaume aliyekuwa na kilo zake nyingi tu na urefu kama unaotajwa katika Biblia alifariki kwa ugonjwa wa moyo katika Hospitali ya Ngaliema huko Kinshasa. Wakati dunia inatangaziwa kwamba Pepe Kale, amefariki kwa ugonjwa wa moyo, huko Congo kulikuwa na habari nyingine kwenye vijiwe vya kahawa na vilabu vya pombe. Wacongo kama walivyo waafrika wengine, walikuwa wanasema ushirikina na ndagu ndio ilikuwa chanzo cha kifo cha Pepe Kale.
Pepe Kale alifariki akiwa na umri wa miaka 46 tu, mwili wake ulionekana wa kizee lakini umri alikuwa bado kabisa. Huko Congo ilikuwa inasemwa kwamba Pepe Kale alikuwa amepewa masharti na mganga wake. Kila alipokuwa anataka kutoa albamu mpya alikuwa anajifungua bafuni kwa muda wa siku tatu. Huko bafuni alikuwa anakuwa kama mtu aliyekufa na kuoza, funza na mende wanamjaa kwenye mwili. Baada ya hizo siku 3 alikuwa anaamka tena na kwenda kuachia albamu yake. Na hiyo album ilikuwa moto na kuvuma dunia nzima. Hayo ndio yalikuwa masharti ya mganga. Sasa, wakongo wanaendelea kusema katika vijiwe vya kahawa, kwamba mwaka huo Pepe Kale alikuwa anajiandaa tena kutoa albamu yake. Akawa ameenda bafuni tena, bahati mbaya mfanyakazi wake wa ndani alikuwa hajui masharti hayo. Siku hiyo mfanyakazi akaenda kufanya usafi bafuni. Alipofika akamkuta Pepe Kale akiwa kama mtu aliyeoza, funza zimejaa mwilini, ndipo yule binti alipopiga kelele kuomba msaada. Na hiyo ndiyo ikawa imesababisha kifo cha Pepe Kale.
Afrika watu wengi ambao huwa wanafanikiwa hata kama wanafanya kazi kwa bidii na maarifa bado mafanikio yao huwa hayaachwi kuambatanishwa na uchawi ama ushirikina. Pepe Kale alifikia mafanikio kutokana na kujituma na kuandaa mziki mzuri. Kwa mtu mwenye uzito kama aliokuwa nao Pepe Kale, sio ajabu kwamba kifo huwa kinatokea katika umri mdogo. Alikuwa na kilo 150. Licha ya hayo yanayosemwa lakini historia imeandika Pepe Kale alipata mshtuko wa moyo tarehe 28 Novemba akiwa nyumbani kwake na kukimbizwa kwenye Hospitali ya Ngaliema huko Kinshasa ambako usiku wa tarehe 29 aliaga dunia...!View attachment 2647319
Aaaah we!!Ebu niache auntie