Shaffih Dauda
Baada ya Feisal kuzungumza kupitia #PowerBreakFast @cloudsfmtz imetupa fursa ya kufanya mjadala ambao ni balanced, tumezisikia pande zote mbili.
Tangu mwanzo kabisa mimi nilikuwa naliangalia hili jambo kama sehemu ya kujifunza kwa manufaa ya tasnia nzima.
Ukiliangalia hili jambo kama la Feisal pekeyake unaweza ukapotea lakini ukilibeba kwa picha kubwa kwamba kuna matukio mengi ya aina hii na mengine yanaweza kutoke huko mbele.
Kupitia hili la Feisal kuna vitu vingi sana vya kujifunza;
Makubaliano ya mchezaji na klabu kuanzia hatua za mwanzo kabisa na kujua kila upande unapaswa kutekeleza majukumu gani kwa wakati gani.
Kuacha kufanya vitu kienyeji kama ambavyo tumezoea, sio kwakuwa klabu inamtaka mchezaji inamfata na kumsaini.
Kwenye masuala ya kazi mchezaji anapaswa kuishi kama taasisi sio mtu mmoja. Wanapokuwa wanaenda kwenye masuala ya usajili waende kama taasisi yenye watu wengi nyuma kwa ajili ya maslahi mapana kwa ajili ya leo na kesho yao.
Klabu nazo zisikubali kufanya mazungumzo na mchezaji pekeake bila wasimamizi, lazima awe na watu wa kumsaidia kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo ya kimikataba. Wasitumie kama fursa pindi mchezaji anapokuwa pekeake.
Hiki kilichotokea kati ya Yanga na Feisal iwe fundisho na sehemu ya mabadiliko kwenye tasnia nzima na masuala ya mikataba na usajili kati ya mchezaji na klabu.
Mfano mchezaji akiishi kama taasisi hizi habari za simu kutokupokelewa hazitakuwepo kwa sababu kutakuwa na mawasiliano rasmi kati ya taasisi moja na nyingine.
Inatoka barua kutoka upande wa mchezaji inaenda kwa klabu, tarehe fulani wawakilishi wa mchezaji wanaomba kikao na upande wa klabu na kusubiri majibu.
Kama hawajajibu kwenye tarehe ambayo waliomba kikao inatumwa barua nyingine ya kuwakumbusha kwamba tarehe fulani ilikuja ikiomba kikao.
Leo hii kungekuwa na ushahidi wa kimaandishi ambao hata wanasheria wa mchezaji wanaweza kumtetea mchezaji wao.