Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20230602_051701_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20230602_051719_Opera%20Mini.jpg
 
KADI KAMA ZOTE
.
13—Kulikuwa na kadi za njano 13 zilizotolewa katika mechi ya fainali ya Europa League baina ya Sevilla (6) na Roma (7) juzi usiku, idadi ambayo ni kubwa zaidi katika mechi yoyote ya Europa League. Kadi saba walizoonyeshwa Roma ni rekodi ya kipekee katika michuano hiyo.
Screenshot_20230602_071746.jpg
 
KIPARA ATATUUA! ANAMTAKA KOVACIC ETIHAD
.
Klabu ya Manchester City imeanza mazungumzo na Chelsea kwa ajili ya uhamisho wa kiungo wake, Mateo Kovacic kwa mujibu wa mkali wa masuala ya usajili, Fabrizio Romano.
.
Kiungo huyo atakuwa huru hadi mwaka 2024, lakini kwa mujibu wa Romano kocha Pep Guardiola anataka kuongeza kiungo mwingine.
.
Chelsea imeonyesha nia ya kumuuza katika kipindi hiki cha usajili wa kiangazi baada ya kuingia mwaka wa mwisho ndani ya viunga vya Stamford Bridge.

…………
Screenshot_20230602_071918.jpg
 
SPAIN WABABE WA ULAYA
.
18—TIMU za Hispania zimeshinda michuano mikubwa ya Ulaya 18 iliyopita ambayo zilikutana na timu za mataifa ambayo siyo ya Hispania, kuanzia ushindi wa Real Madrid dhidi ya Bayer Leverkusen ya Ujerumani katika mechi ya fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya 2002.

Screenshot_20230602_072020.jpg
 
Farhan Jr

A story to tell, picha ambazo zina maandishi mengi kwenye mikono yangu! Nilikuwa nina uwezo wa kufahamu vitu vya kuvisoma ila sikuwahi kuuishi utamaduni tofauti na kufahamu maisha ya nchi nyingine.

Sikuwahi kuona namna gani Makocha wanaandaa Wachezaji kuelekea mechi kubwa ama Wachezaji wanajiandaa vipi kuelekea mechi kubwa zaidi ya kusoma vitabuni.

Ukiniuliza kama Mimi Kijana kutoka Morogoro niliwahi kuiota picha hii nitakuwa naongopa, sikuwahi kufikiria nitafika nchi hii ya mpira, kwa ajili ya mpira na kukutana na watu wa mpira.

Siku moja nitaandika juu ya hii picha, sote tulimtazama Coach Nabi hapo baada ya Press Conference, alizungumza vitu kama Baba ambaye kila Kijana anapaswa kusikia.

Kwangu safari hii ni darasa kubwa sana sana sana, nina mengi ya kuandika kama sio hivyo basi nina mengi ya kusimulia siku moja nikiwa kijijini kwangu huko Ifakara, Morogoro.
Screenshot_20230603_052727.jpg
 
KOCHA NASREDDINE NABI :
.
“Hakuna kocha ambaye ataamua kumweka nje Morrison kwa kipaji chake kama yuko sawa, watu wasidhani sisi makocha hatupendi kuona timu inashinda. Mimi sio kocha wa kumpa nafasi mchezaji kwa jina lake au presha ya nje ya Uwanja tofauti na kile anachonionyesha mazoezini.”
Screenshot_20230603_052727.jpg
 
MOSES PHIRI ni Mzambia mwingine ambaye anaishi nyumba moja na Chama, Phiri mwenye mabao 10 kwenye Ligi Kuu Bara naye anaishi Mikocheni jijini Dar es Salaam.
.
Mshambuliaji huyo anaishi na familia yake, akiwa na mke na watoto wawili na chanzo kinaonyesha kuwa kwenye ghorofa hilo lililopo Mikocheni analipa kiwango kilekile kama cha Chama cha dola 800 kwa mwezi, lakini ikionekana kuwa hana gari analomiliki jijini Dar es Salaam zaidi ya kuonekana mara kwa mara akiwa na magari ya Chama au usafiri wa kukodi.
Screenshot_20230603_053244.jpg
 
Kiungo Said Hamis Ndemla anamtaja Meneja wa Simba, Patrick Rweyemamu ndiye aliyeona kipaji chake wakati akiichezea timu ya mtaani ya Mesina na ilikuwa mechi ya kirafiki dhidi ya Simba B na hapo ndio ukawa mwanzo wake wa kutua Simba.
.
“Aliyekiona kipaji changu kwa mara ya kwanza ni Meneja wa Simba, Patrick Rweyemamu, tulicheza mechi ya kirafiki nikiwa na timu yangu ya mtaani ya Mesina dhidi ya Simba B Uwanja wa Kinesi, baada ya mechi akaniita akasema nipe namba yako nitakupigia ili uchezee Simba B, ilikuwa mwaka 2012, kisha akafanya hivyo nikasaini.”
Screenshot_20230603_053428.jpg
 
Ni kiungo mshambuliaji raia wa Burkina Faso akiwa anatajwa kati ya wachezaji ambao walisajiliwa kwa kitita kikubwa cha fedha. Huyu anaishi kwenye mjengo Kawe Mzimuni, lakini tofauti kwake ni kwamba anakaa sehemu kubwa zaidi na analipa dola 800 kwa mwezi.
.
Anatumia magari ya Benard Morrison mara kwa mara au magari ya kukodisha. Ni mchezaji ambaye anaishi kimahesabu sana, hapendi makuu.
Screenshot_20230603_053523.jpg
 
JUST IN: Kocha wa timu ya taifa ya Senegal Aliou Cisse amemjumuisha Kiungo mshambuliaji wa Simba, PAPE SAKHO katika kikosi cha wachezaji 24 cha timu ya taifa ya Senegal ‘Simba wa Terenga’ kitachocheza mechi mbili, moja ya kufuzu michuano ya AFCON dhidi ya Benin na nyigine ya Kirafiki dhidi ya Brazil .
Screenshot_20230603_053629.jpg
 
Huyu ni mshambuliaji wa Yanga ambaye amekuwa akifanya vizuri msimu huu akitokea DR Congo, ndiye mfungaji bora kwenye Ligi Kuu, Mayele anaongoza pia kwenye kupachika mabao kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika akiwa na mabao saba na pasi tatu za mabao.
.
Huyu anaishi kwenye Apartment maeneo ya Victoria, Kijitonyama Jijini Dar es Salaam. Sehemu ambayo mchezaji huyo anakaa na familia yake na analipa dola 800 ambayo ni sawa na shilingi milioni 1.8 milioni Ana gari kali aina ya Toyota Harrier nyeusi na Toyota Premio.
Screenshot_20230603_053751.jpg
 
Amekuwa akitajwa kati ya wachezaji bora sana akiwa amepangiwa na Simba ghorofa moja matata eneo la Mikocheni Jijini Dar es Salaam ambapo uchunguzi umeonyesha kuwa analipa dola 800 kwa mwezi sawa na Sh 1.8 milioni.
.
Chama raia wa Zambia anakaa na watoto wake watatu pamoja na mchumba wake. Staa huyo kwenye upande wa gari anatajwa kuwa mmoja kati ya watu wanaotumia magari ya bei ghali zaidi, kwa sasa akiwa anatumia Range Rover na BMW kwenye mihangaiko yake ya jiji la Dar es Salaam, lakini chanzo kinasema kuwa magari hayo ndiyo pia amekuwa akitumia akiwa kwao Zambia.
Screenshot_20230603_053845.jpg
 
YANGA YAONDOKA NA WAPISHI
.
Msafara wa kikosi cha Yanga, viongozi na mashabiki umeondoka jana Alhamisi asubuhi kuelekea Algeria kumalizia mechi ya pili ya fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika lakini kuna mambo mawili mazito wameyafanya.
.
Wakitumia ndege ya Shirika la Tanzania Yanga imeondoka na viroba vya vyakula, maji na wapishi wao wa kambini huku wakisema watu wao wawili waliotangulia tayari wameshawatumia taarifa kamili ya vitu gani vya kufanya wakati msafara huo unaondoka jana.
.
Yanga ilishawatanguliza watu wawili Algeria akiwemo makamu wao wa Rais Arafat Haji na mratibu wa klabu hiyo Hafidh Saleh kwenda kuandaa mazingira sahihi ya kufikia timu yao.
.
Msimu huu Yanga ndio mara ya kwanza inakwenda kucheza ugenini ikiwa na vyakula vyake na wapishi wakichukua tahadhari zote kabla ya mchezo huo utakaopigwa Juni 3, jijini Algers.

Screenshot_20230603_054054.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom