Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20230410_052847_Instagram%20Lite.jpg
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata Watu wanne akiwemo Emmanuel Msofe ambaye ni Dereva na Mkazi wa Keko kwa tuhuma za wizi wa mabomba ya mradi wa maji wa Kisarawe II aina ya PVs inch 6.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema, Jeshi hilo kwa kushirikiana na Wananchi jana Aprili 8, 2023 majira ya saa 2 hadi 3 usiku walikamata gari namba T 719 AGL (Canter Mitsubish) likiwa na mabomba ya mradi wa Kisarawe II aina ya PVC inch 6, maeneo ya Kibugumo Mji Mwema Kigamboni.

"Mradi huu ni miongoni mwa miradi mikubwa inayofanywa na Serikali lakini inasimamiwa kwa karibu sana na DAWASA, wezi hawa wamekamatwa na kimsingi tunawahoji kwa kina kwasababu pale yapo mabomba mengi tunataka kujua kabla ya kuwakamata wameiba mara ngapi mabomba haya kwa sababu muda wa saa 2 haukuwa usiku sana kwa maana hapa kuna njama na Watu fulani bado hatujawatambua na tunafanya uchunguzi wa kina tujue haya mabomba yamekwisha ibwa mangapi na kama wameiba mengi, je huu mradi utakwisha kwa namna gani!?”
Screenshot_20230410_054211.jpg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amevunja Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Aidha, Rais Samia ametengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA), Mhandisi John Nzulule.

Katika hatua nyingine, Rais Samia amemuelekeza Katibu Mkuu Kiongozi kuhakikisha kuwa Makatibu Wakuu na Watendaji Wakuu wote wa Taasisi za Serikali wanaipitia kwa kina taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kujibu na kuzifanyia kazi kwa haraka hoja zote zinazogusa maeneo yao.

Vilevile, Rais ameelekeza kuwa Watendaji wote watakaobainika kuhusika na uzembe au ubadhirifu wachukuliwe hatua za kisheria.
Screenshot_20230410_054537.jpg
 
Taasisi ya Dini ya Kiislam ya Al- Hikma Foundation ya Jijini Dar es salaam, imetanganza kuwaozesha Vijana 50 kwa kuwalipia mahari ambao bado hawajaoa kutokana na changamoto za kifedha na wapo tayari kutekeleza Ibada ya ndoa.

Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Sheikh Nurdini Kishki ameleeza hayo wakati wa Mashindano ya 23 ya Kimataifa ya kuhifadhi Qur’aan Tukufu yaliyofanyika leo April 09 2023, Uwanja wa Uhuru Dar es salaam, yakihudhuriwa na Viongozi wa Serikali na Kidini huku Mgeni rasmi katika mashindano hayo akiwa ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi.

Sheikh Kishki amenukuliwa akisema “Tutafanya ndoa ya pamoja Watu 50, mahari ya Vijana hao itakuwa juu yetu sisi Al- Hikma Foundation, sharti usiwe unaongeza Mke wa pili na ndoa itafanyika Dar es salaam chini ya Mufti wa Tanzania Sheikh Dkt. Abubakar Zubeir Bin Ally”
Screenshot_20230410_054817.jpg
 
Taasisi ya Dini ya Kiislam ya Al- Hikma Foundation ya Jijini Dar es salaam, imetanganza kuwaozesha Vijana 50 kwa kuwalipia mahari ambao bado hawajaoa kutokana na changamoto za kifedha na wapo tayari kutekeleza Ibada ya ndoa.

Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Sheikh Nurdini Kishki ameleeza hayo wakati wa Mashindano ya 23 ya Kimataifa ya kuhifadhi Qur’aan Tukufu yaliyofanyika leo April 09 2023, Uwanja wa Uhuru Dar es salaam, yakihudhuriwa na Viongozi wa Serikali na Kidini huku Mgeni rasmi katika mashindano hayo akiwa ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi.

Sheikh Kishki amenukuliwa akisema “Tutafanya ndoa ya pamoja Watu 50, mahari ya Vijana hao itakuwa juu yetu sisi Al- Hikma Foundation, sharti usiwe unaongeza Mke wa pili na ndoa itafanyika Dar es salaam chini ya Mufti wa Tanzania Sheikh Dkt. Abubakar Zubeir Bin Ally”
View attachment 2582747
hahahaha
 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango na Mkewe Mama Mbonimpaye Mpango leo tarehe 09 Aprili 2023 wameungana na Waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Mwenyeheri Maria Theresa Ledochowska Kiwanja cha Ndege Dodoma katika Ibada ya Jumapili ya Sikukuu ya Pasaka.

Akiongea na Waumini wa Kanisa hilo mara baada ya kumalizika Ibada, Makamu wa Rais amewasihi Wazazi na Walezi kuwalinda Watoto pamoja na Vijana wao dhidi ya matumizi mabaya ya simu pamoja na kufuatilia mienendo yao wakati wote.

Amewaasa Wazazi na Walezi kulea Watoto wao kwa kuzingatia maadili mema ya kitanzania pamoja na kuwa makini na maudhui ya Watoto (Katuni) katika televisheni ili kuwaepusha na kujifunza mambo yasiofaa.

Makamu wa Rais amesema ni vema kwa Wazazi kutambua Marafiki wa Watoto wao na kuwapa miongozo sahihi wakati wote na kutowaacha kujiongoza wenyewe.

Pia amewataka Walimu wa Shule za Msingi, Sekondari na hata Vyuoni kukemea kwa nguvu uharibifu wa maadili ya kitanzania katika maeneo ya kutolea elimu.
Screenshot_20230410_054951.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom