Makapuku Forum

Makapuku Forum

ALGERIA YAFUZU AFCON
.
FT: NIGER 0-1 ALGERIA
06’—️ Bounedjah
.
Msimamo Kundi F
1. Algeria — 12pts
2. Tanzania — 4pts*
3. Niger — 2pts
4. Uganda — 1pts*
Screenshot_20230328_051801_OGInsta%2B.jpg
 
AZAM FC kwa sasa inatafuta kocha mpya ili ainoe kwa msimu ujao na katika mipango yao jina limepewa kipaumbele ni la Kocha wa Al Hilal, Mkongo Florent Ibenge.
.
Taarifa zinaeleza kuwa Mabosi wa Azam FC tayari wamefanya mazungumzo ya awali na Kocha Florent Ibenge anoe kikosi chao msimu ujao. Inadaiwa endapo Ibenge atashindwa kuifikisha Al Hilal robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika huenda akatimuliwa huko Sudan na moja kwa moja akatua kwa matajiri wa Chamazi.
Screenshot_20230328_052154_OGInsta%2B.jpg
 
SINGIDA WANA JAMBO LAO SIMBA
.
Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya Singida Big Stars kinasema, klabu hiyo imeanza mipango ya kumng’oa kipa Beno Kakolanya kutoka Simba ambaye mkataba wake unaelekea mwishoni kwa lengo la kumsajili aitumie kuanzia msimu ujao.
.
Mkataba wa Kakolanya na Simba unaisha mwishoni mwa msimu huu na hadi sasa inadaiwa hakuna makubaliano ya kusaini dili jipya licha ya mabosi wa Msimbazi kuzungumza naye hivi karibuni. Mazungumzo baina ya Singida na Kakolanya yamefikia pazuri na muda wowote baada ya kurejea kutoka Misri anaweza kumwaga wino.
Screenshot_20230328_052353_OGInsta%2B.jpg
 
SIMBA KUTUA MOROCCO KIMKAKATI
.
Mastaa wa Simba wasiokuwepo kwenye timu za taifa wanaendelea kujifua mazoezini Mo Simba Arena, huku mabosi wa klabu hiyo wakiweka mikakati ya kuifuata Raja Casabalanca kwa mafungu kati ya kesho na keshokutwa wakipanga kumaliza hatua ya makundi ya Ligi za Mabingwa Afrika kwa heshima.
.
Mabosi wa Simba katika kuhakikisha wanaenda kuweka heshima ugenini wamepanga timu iondoke mapema kati ya kesho na Jumatano ili kuwahi mchezo huo baada ya kubaini kuna tatizo la usafiri kwenda Morocco utakapochezwa mchezo huo utakaopigwa saa 10:00 jioni saa za Afrika Mashariki.
.
Habari kutoka ndani ya Simba zilizonaswa zinaeleza kikosi cha timu hiyo kinatarajiwa kuondoka kwa mafungu, huku msafara wa kwanza ukianza kuondoka kesho Jumanne na ule wa mwisho utaondoka Jumatano na mastaa waliopo katika timu nyingine za taifa nje ya Tanzania wataunga huko huko.
Screenshot_20230328_052524_OGInsta%2B.jpg
 
FRII-KIKI BAO
600/800 —Bao la 600 la Lionel Messi katika maisha ya soka alilifunga kwa frii-kiki (Barca v Atletico Madrid), bao lake la 600 la ngazi ya klabu alilifunga pia kwa frii-kii (Barca v Liverpool) na la 800 katika maisha yake ya soka pia kalifunga kwa frii-kiki (Argentina v Panama).

Screenshot_20230328_052809_OGInsta%2B.jpg
 
OFFICIAL: TOTTENHAM imefikia makubaliano ya pande zote mbili kuachana na Kocha wake, Muitaliano Antonio Conte.
.
Aliyekuwa msaidizi wa Conte, Cristian Stellini atakaimu nafasi ya Kocha mkuu hadi mwisho wa msimu, na kiungo wa zamani wa Spurs, Ryan Mason atakuwa msaidizi wake.
Screenshot_20230328_052900_OGInsta%2B.jpg
 
TUCHEL AMTAKA MENDY BAYERN
.
Kocha mpya wa Bayern Munich, Thomas Tuchel huenda akawasilisha jina la kipa wa Chelsea, Edouard Mendy, 31, ili akawe mbadala wa Manuel Neuer ambaye huenda akaondoka mwisho wa msimu huu kutokana na umri wake.
.
Mendy ni miongoni mwa mastaa ambao wameruhusiwa kuondoka kwenye kikosi cha Chelsea baada ya kutofikia makubaliano ya kusaini mkataba mpya Stamford Bridge.

Screenshot_20230328_053006_OGInsta%2B.jpg
 
Shaffih Dauda #VituExtra.

MATOKEO UBAONI YANGA 4-1 SIMBA

Nilikua najaribu kuwaweka hawa ‘Mapacha wa kariakoo’ kwenye mzani ila naona mpaka naingia mitamboni mzani hauja’Balance upande wa Simba.

Tuwapime Simba na Yanga kwenye haya maeneo

Social Media Engagement & Interaction

Kuanzia Twitter, Instagram na Youtube, Simba Sc wanaupiga mwingi sana. Wamewazidi Yanga kila eneo. Data zipo wazi

Simba Twitter:1.3M, Insta: 4.7m na Youtube: 340k Subscribers

Yanga: Twitter: 247.1K, Insta: 2.4M
Youtube: 293k Subscribers

Jersey Design, Quality & Distribution

Yanga: Kwa zaidi ya misimu 4 mfululizo wametoa Jezi kali zenye concept na ambazo zina quality inayofanya wao wafanye vizuri kwenye soko la mauzo ya jezi. Yanga chini ya GSM wameset standard kwenye suala la jezi. They are simply unbeatable

Simba: Upande wa jezi, Simba design zao ni average sana, kwa ufupi ni kuwa hawana maajabu sana.

Kwa misimu kadhaa sasa wamekua hawafanyi vizuri sokoni kwenye upande wa jezi. Ucheleweshwaji wa jezi kufika kwa wakati msimu uliopita na msimu huu imekua tatizo. Ipo kazi ya kufanyika hapa

Gate Collections

Yanga: Kwa misimu miwili mfululizo zimetoka takwimu wameongoza kwa kuingiza mashabiki wengi uwanjani. Hata mapato mlangoni wameyakusanya sana zaidi ya Simba. Hii inachangiwa na perfomance nzuri ya timu.

Simba: Kwenye suala la kuingiza mashabiki wengi kwenye mechi za ligi kuu, Simba wapo ‘Hoves’ sana.

Mashabiki wa Simba wanachagua sana mechi, tuseme hawana mizuka sana na timu yao. Hii inawezekana labda ni kwa sababu kwa kiasi fulani ni kushuka kwa perfomance ya Simba kwenye mechi za ligi kuu

Fans Involvement.

Yanga: Wanaupiga mwingi kwenye ‘Uhusishwaji wa wanachama na mashabiki’ kwenye ukuaji wa timu yao. Kuanzia msimu uliopita Yanga wamesajili sana wanachama wao kwa njia ya Kidijitali. Kama club wameingiza zaidi ya 1Billion kwenye miezi 6 ya kwanza.

Simba: Kwenye suala la usajili wa wanachama Simba hawana jipya. Simba wapo nyuma hatua 10, hawaendi na kasi ya teknolojia.

Mpaka sasa Ubaoni Yanga anaongoza bao 4, Simba bao 1. Muda sasa ifanyike ‘Substitution’ ili mzani uweze ku’Balance.
Screenshot_20230328_053134_OGInsta%2B.jpg
 
Klabu ya Chelsea jana waliandaa hafla fupi ya Iftaar kwa Mashabiki wa timu hiyo ambao wapo kwenye mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan, Chelsea wamefanya hivyo kuthamini Mashabiki wao wakishirikiana na taasisi ya Open Iftaar.
Screenshot_20230328_053435_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Kikao cha bodi ndani ya Bayern Munich April, 2014 kilikuwa mahsusi kuhusu kitengo chao cha Habari na Mawasiliano (Media and Communications) baada ya kampuni moja kufanya tafiti zao wakagundua wanahitaji mabadiliko.

Bayern waligundua kadri muda unavyozidi kwenda kuna kiu kubwa ya Bavarians kufika kwenye mioyo ya watu kupitia Media, waligundua kuna mvuto hawana ndipo wakafanya jambo.

Press Officer Dieter Nickles na Stefan Mennerch ambaye ndie Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano waliitwa na katika maongezi marefu klabu ikaamua kumpandisha Bwana Max Breitner kuingia kama Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano.

Kutokea hapo mpaka hii leo kila kitu wanachokifanya Bayern kwenye mitandao ya kijamii na Media kwa ujumla ni daraja lingine, simply ni kuwa walimpata Mtu ambaye viatu vinamtosha na amefanya kazi kubwa sana.

Connect dots na anachokifanya! ENGINEER Hersi pale Yanga, kwanza fanya tafiti zote Maafisa Habari wote mpaka sasa kisha tazama takwimu na mwisho pima mzani utagundua karata ya Ali Kamwe ndio karata iliyochangwa kwa umaridadi mkubwa sana.

Mr President is the Wizard of the Capital gain? Unamchukua Ali na Priva wenye idadi ya followers kama Million tatu kwa platforms zao, kizazi kipya na wana audience kubwa ya Simba na Yanga wote! Ambapo wanafikisha ujumbe kwa timu zote mbili japo walengwa ni Yanga.

Ukiwatazama Yanga wamewin sana kwenye digital ni akili ambayo imetumika kuisafisha brand yao ambayo ilikuwa haina mvuto muda fulani mbele ya watu, wakati Simba wana Ahmed hii generation ilimtreat kama Mtu wao na anaongea na watu wengi wa kizazi chake, Simba iliwin sana hapa.

Yanga waliulewa vyema mchezo na waliona namna Ahmed anapenya kirahisi sana kutokana na zama zake, watu wake na umri wake! Ndipo Rais akaisukuma hii kete, imemlipa sana! Tazama press za Ali kwasasa na clips zake mtandaoni ni kama Ahmed, hivi ndivyo michezo ya branding inachezwa hivi sasa.

Msemaji @alikamwe @ahmedally_ mna kitu mtafika mbali huu ni muda wenu

Screenshot_20230328_054855_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Kiongozi wa Yanga mjanja mjanja na Mhuni ambaye akipewa Urais wa hii timu ataiharibu na wataonekana Wahuni aliwahi kupata hii picha bora kabisa huko Unguja.

Pichani Kiongozi Mhuni alipiga picha na IBRAHIM BACCA wakati huo anakipiga KMKM huko Unguja baada tu ya mchezo wao na Yanga, Kiongozi huyo Mjanja mjanja ambaye hajui mpira alitambua uwezo wa mchezaji huyu.

Kwasasa Mchezaji huyo ni lulu kwa taifa na Kiongozi Mhuni Mjanja Mjanja ni Rais wa Yanga na mpaka sasa kwakuwa hajui mpira wamebeba Ngao back to back na Premier League on process

Hongera sana Kiongozi Mhuni na Mjanja mjanja ambaye hufai kupewa Urais wa Yanga

WANANCHI mnaendeleaje na Rais wenu Mhuni hapo Jangwani!?

Screenshot_20230328_055029_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

MO DEWJI anaongea ukweli ambao wengi hawataki kuusikia na kuna siku niliandika andiko langu hapa kuwa mpira wa miguu bado sio mchezo ambao ni biashara bali mchezo wa sifa na ufahari tu (Prestigious game) lakini sio mchezo ambao una hiyo return kwa hapa kwetu.

MO ana 49% ya hisa na ndie pekee yupo active ila tuulizane hiyo 51% ya Wanachama ina nguvu gani? Wanachama wangapi wamelipia kadi, wanachama wangapi wamekuwa wateja wa klabu moja kwa moja? Bado kuna changamoto kubwa.

Leo hii Al Ahly ya Misri ina kadi za Uanachama mpaka Million 100, Ahly wana kadi za watoto ambapo ada hufika hadi 100,000/= ambapo huku kwetu unalipia kadi za watu hata watano kwa mwaka, tazama umbali uliopo.

MO DEWJI ama Matajiri wengine wana passion na huu mchezo na ndicho kitu wanachokifanya lakini nje ya passion unachoweka na unachokipata ni kidogo sana, mfumo wetu bado haupo kwenye mfumo wa kibiashara.

SENZO alipokuja nchini alitaka kutupa nchi format nzuri sana ya Mpira biashara, alitaka kutupa format nzuri sana ambayo South Africa wale giants wanaitumia kiasi ambacho wanaridhika na mapato wanayotengeneza.

MO ana hoja tena kubwa sana asikilizwe, ana 49% tu na ndie anawekeza ila 51% iko imeganda na wala sio asset kwa klabu hivyo mfumo unaendeshwa na mwenye hisa ndogo.

Screenshot_20230328_055212_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Wakati nimeandika kuhusu kauli ya MO DEWJI kuna watu walikuja na mifano ya Roman Abramovich na Chelsea, wakisema hajawahi kulalamika kuwa timu inamwingizia hasara na kuwa Chelsea imetengeneza tu faida, SIO KWELI! Hatuwezi kufananisha watu haiba.

Wakati Roman anaichukua Chelsea 2003 hapakuwa na suala la FINANCIAL FAIRPLAY (FFP) kwa maana ya kuwa klabu inapaswa kutumia kwa kile inachozalisha, hii sheria ilikuja 2011 na ikaanza kutumika msimu wa 2011/12 barani Ulaya.

Hapa ndipo ikaendelea kuonesha kuwa klabu haziwezi kusimama kwa pesa zinazozalisha tu bali lazima kuwa na mfuko wa nje ambao kwa sheria za Ulaya ni kama zinaendeshwa kwa kukopa au kwa mtindo wa udhamini mfano Manchester City walivyochezesha dili la ETIHAD kukaa kifuani na naming rights za uwanja kutoka City of Manchester.

Mpira wa miguu HAUNA FAIDA haswa kwa Matajiri wenye ndoto kubwa na ushindani ndio maana City wanachezesha sana ili pesa za nje ya mfuko ziingie!

Sasa turejee kwenye suala la Chelsea na Roman Abramovich, watu wanasahau kuwa Roman alisamehe deni lake la PAUNI 1.6 BILLION anayoidai Chelsea, yaani licha ya udhamini na uwekezaji wake bado iliundwa kampuni maalum inaitwa FORDSTAM ambayo ni tanzu na Chelsea ndio ilikuwa inachukua mzigo kwa Roman kupitia kampuni yake nyingine Camberley International Investments, ili kukwepa FFP.

Kwanini MO DEWJI anaposema mpira ni hasara tunapinga?? Ni ukweli uliowazi hakuna hela kwenye huu mpira na ni ukweli kuwa lazima Matajiri waumie na wanazidai sana hizi timu.

Fikiria Roman ameondoka akiwa ameisamehe Chelsea deni la pesa nyingi sana! Fikiria unaandaa timu inashindania Ligi Kuu ambayo unapata mfano Million 500 na umetumia mara mbili yake.

Fikiria gharama za Simba kucheza hatua za awali mpaka hatua za mtoano, fikiria camps na bonus bado usafiri na usajili! tukisema MO anapata hasara kwanini hatukubali?

Football is nothing than a prestigious game! Hivyo Tajiri ana haki ya kuongea anapohitaji kwakuwa anaweka hela.
Screenshot_20230328_055315_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom