Farhan Jr
MMEAMUA KUTOMUELEWA MO DEWJI? MMEINGIA MTEGONI?
Nimesikiliza interview zote za Tajiri Kijana Afrika, MO Dewji nimetafakari kila alichosema ila headlines za wengi zimeenda tofauti na kile alichomaanisha na wengi wameelewa tofauti na alichomaanisha.
MO DEWJI amerejesha mpira kwa Mashabiki na Wanachama wa Simba ambao wengi walipaswa kumuelewa ila bahati mbaya hawajaelewa, MO ameongea vitu vikubwa sana na vina maana kubwa sana.
Shabiki wa Simba sikiliza! MO DEWJI analalama kuwa kuna Watu wanakwamisha mchakato wa mabadiliko, kuna watu amesema anawafahamu! Kuna ubaya gani MO kuhitaji kila kitu kikamilike ili klabu isimame wima kwa miguu miwili?
MO anaweka pesa zake sehemu ambayo bado hatma yake haijulikani kwakuwa mchakato haujakamilika, MO ameipanua bajeti mara 10 kutoka Billion mbili mpaka BILLION 20 kwa mwaka, kwanini asiongee kama anakwamishwa?
MO ana hoja nzuri sana! Anahitaji Mashabiki na Wanachama waamke kwakuwa mabadiliko yalipitishwa na Wanachama wote hivyo anataka waielewe katiba, hapo kosa lake nini? Tajiri anapambana 51% za Wanachama ziwe na nguvu ili zisaidiane na 49% zake, hapo amekosea nini?
MO DEWJI ndani ya Simba sio suala la biashara tu bali Passion ya kweli kutoka moyoni mwake! Leo hii anawekeza kwenye timu za Vijana kuanzia U14, U16 na U20 unaweza kuelewa namna gani pesa zitamwagwa? Kuanzia watalaam na huduma zote?
Leo hii watu wanapiga kelele kuhusu MO DEWJI FOUNDATION nyuma ya jezi! Wanafahamu kuwa ndio mfuko utakaoenda kudhamini watoto wa timu za vijana kuanzia ELIMU (watasomeshwa) na pia gharama za kuishi (watatafutiwa familia Dar Es Salaam) hapo Tajiri ana kosa gani? Tumeshindwa kumuelewa?
Yes MO ana hoja! Tajiri gani angekubali kuendelea kutupa hela sehemu ambapo bado hatma ipo juu juu inaelea? Tajiri gani angeendeleza long term plans wakati hajui hatma yake? Ni suala la kimchakato.
Mashabiki na Wanachama kadhaa mmechagua kutomuelewa wakati ambao MO alipaswa kueleweka zaidi na kupewa support! Sio kwamba anasimanga ila ni ukweli kuwa mchakato umekuwa mgumu na muda unakwenda.
Mmechagua kutomuelewa Tajiri @moodewji anawakumbusha kuhusu kuheshimiwa mawazo yenu mliyopitisha kwenye mkutano mkuu??