Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20230328_071020_Opera%20Mini.jpg
 
Rais wa Tanzania, Dkt.Samia Suluhu Hassan ameunda Kamati kwa ajili ya kutathmini utendaji kazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ili kuiwezesha Wizara hiyo kutekeleza malengo ya Serikali katika kukuza diplomasia ya uchumi na ushirikiano wa kimataifa.

Ili kutekeleza azma hiyo amemteua Balozi Yahya Simba, aliyekuwa Balozi wa Tanzania chini Zambia kuwa Mwenyekiti wa Kamati.

Aidha, amewateua wafuatao kuwa Wajumbe wa Kamati, Balozi Ramadhan Mwombe Mwinyi, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar, Mstaafu, Balozi Dkt. Mwanaidi Sinare Maajar, aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Balozi Peter Allan Kallaghe, aliyekuwa Balozi wa Tanzania chini Uingereza.

Wengine ni Balozi Tovako Nathaniel Manongi, aliyekuwa Mwakilishi wa Kudumu wanTanzania kwenye Umoja wa Mataifa New York, Marekani, Kamati hiyo itazinduliwa rasmi tarehe 31 Machi, 2023 Ikulu Dar es salaam.
Screenshot_20230329_044932_OGInsta%2B.jpg
 
Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) imesema majeruhi pekee wa ajali ya basi la mwendokasi iliyotokea tarehe 22/2/2023 Jijini Dar es Salaam ambaye alionekana akigongwa na basi hilo Osam Milanzi, ameruhusiwa kutoka Hospitali baada ya afya yake kuimarika.

Meneja uhusiano @taasisiyamifupa_moi Patrick Mvungi amesema “Milanzi alipokelewa MOI tarehe 22/2/2023 ambapo alipata huduma za kibingwa katika kitengo cha dharura (EMD), ICU, HDU na wodi 2A “

“Milanzi alipokelewa MOI akiwa ameumia maeneo ya kichwa, mguu wa kushoto, mkono na bega upande wa kulia ambapo ataendelea na huduma kama Mgonjwa wa nje na atarudi kliniki baada ya wiki mbili”

“Tunatoa shukran za dhati kwa Watanzania wote, vyombo vya habari ambao kwa pamoja wameshirikiana nasi katika kumuombea na kumtangaza Osam Milanzi”
Screenshot_20230329_045429_OGInsta%2B.jpg
 
Makamu Rais wa Marekani Kamala Harris ameahidi Nchi yake itaisaidia Ghana ambayo inakabiliwa na mgogoro wa kiuchumi na wasiwasi wa kiusalama.

Makamu huyo wa Rais wa Marekani amesema hayo mjini Accra, kituo cha kwanza cha ziara yake Barani Afrika, ambako alikutana na Rais wa Nchi hiyo, Nana Akufo Addo.

Katika mkutano na Waandishi wa Habaari pamoja na Rais Addo, Kamala Harris amesema chini ya Uongozi wa Rais Addo Ghana imekuwa mwanga wa demokrasia na Mchangiaji wa amani na usalama Duniani.

Ametangaza msaada wa USD Milioni 100 na kuahidi kwamba Marekani itaimarisha ushirikiano wake na Bara la Afrika.

Aidha Serikali ya Marekani imeliomba Bunge la Nchi hiyo USD Milioni 139 nyingine kwa ajili ya kuisadia Ghana kupunguza kiwango cha watoto wanaofanyishwa kazi, kuimarisha shughuli za utafiti wa hali ya hewa, kuwasaidia Wanamuziki nchini humo pamoja na kukabiliana na mlipiuko ya magonjwa.
Screenshot_20230329_045640_OGInsta%2B.jpg
 
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara wa PASS Trust, Adam Kamanda, ameelezea fursa zilizopo PASS kwa Wadau wa kilimo biashara katika kuwekeza kwenye miradi inayozingatia utunzaji wa mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi, ambapo Taasisii hiyo inatoa dhamana ya hadi 80% kwenye mnyororo wa thaman katika sekta ya kilimo, mifugo, uvuvi, viwanda na mazao ya misitu.

Miradi hiyo ni pamoja na inayowekeza kwenye; matumizi bora ya maji, matumizi ya nishati mbadala, matumizi bora ya ardhi, inayozingatia urejeleshaji wa taka zitokanazo na shughuli za kilimo, matumizi ya mbolea asilia na miradi yote inayozingatia kanuni na taratibu zote za uhifadhi wa mazingira.

Lengo kuu la PASS Trust @passtrust ni kuhakikisha wadau wa kilimo biashara wanaongeza tija katika shughuli zao huku wakitumia rasilimali vizuri, kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kuleta uendelevu wa shughuli hizo.
Screenshot_20230329_045832_OGInsta%2B.jpg
 
Ofisi ya Rais - TAMISEMI imetoa fursa kwa Wahitimu wa Elimu ya Sekondari Kidato cha Nne kufanya mabadiliko ya Tahasusi (COMBINATION) na kozi za Vyuo vya Kati walizochagua kupitia fomu za Selform mwaka 2022.

Mabadiliko yanafanyika kwenye Mfumo wa Uchaguzi wa Wanafunzi (Student Selection MIS) kupitia kiunganishi cha selform.tamisemi.go.tz

Jinsi ya kufanya mabadiliko unatumia namba yako ya mtihani, jina la mwisho, mwaka wa kuzaliwa na alama ya ufaulu katika somo au swali utakaloulizwa ambapo zoezi hili limeanza Kufanyika kuanzia tarehe 15/03/2023 na mwisho ni tarehe 06/04/2023.

“Kwa changamoto yoyote, wasiliana nasi kwa barua pepe helpdesk@tamisemi.go.tz au piga 0262 160 210 na 0735 160 210 na ili kujenga uelewa wa pamoja Mzazi/Mlezi unashauriwa kushirikiana na Mtoto wako katika mabadiliko ya machaguo ya Tahasusi na kozi za Vyuo vya kati”
Screenshot_20230329_050351_OGInsta%2B.jpg
 
Shirika la Reli Tanzania (TRC) limesitisha safari zake katika mikoa sita hapa nchini kutokana na mvua zinazoendelea kuonyesha katika maeneo mbalimbali.

Mikoa itakayoathiriwa na uamuzi huo wa TRC ni Dar es Salaam kuelekea mikoa ya Morogoro, Dodoma, Mwanza, Tabora, Mpanda na Kigoma.

Kupitia taarifa iliyotolewa kwa Umma na kusainiwa na Meneja Uhusiano wa TRC, Jamila Mbaruk leo Machi 28,2023 uamuzi huo umefikiwa kutokana na mvua zinazoendelea kuonyesha maeneo mbalimbali nchini ambazo zimeathiri miundombinu.
Screenshot_20230329_050545_OGInsta%2B.jpg
 
Mchezo wa kufuzu fainali za Mataifa Afrika ya (AFCON) kati timu ya taifa 'Taifa Stars' dhidi ya Uganda 'The Cranes' umetamatika kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa kwa wenyeji kukubali kichapo cha bao 1-0.

Bao la Uganda limefungwa dakika ya 90 na nyota wake, Rogers Mato na kuifanya Stars kujiwekea mazingira magumu ya kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Ivory Coast.

Kwa matokeo hayo katika kundi F Stars inasalia nafasi ya pili na pointi nne nyuma ya vinara Algeria ambayo tayari imefuzu baada ya kufikisha jumla ya pointi 12 kufuatia timu zote kucheza michezo minne.

Screenshot_20230329_050950_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom