Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20230322_074138_Opera%20Mini.jpg
 
Ramadhan njema wadau mnaoanza mfungo na wale mnaondelea na Kwaresma komaeni.

Ndugu yenu nipo na nitafanya tu kama nilivyofanya mwaka jana.
 
Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali imejiridhisha uwepo wa chakula cha kutosha kwenye maghala mbalimbali ya Zanzibar na kuwataka Wananchi kutokua na hofu ya kupatikana kwa chakula katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan licha ya bei za chakula kuwa juu katika Mataifa mengi Duniani.

Rais Mwinyi amenukuliwa akisema “Serikali imejiridhisha chakula kipo katika maghala mbalimbali ya Wafanyabiashara wakubwa wanaoingiza chakula Zanzibar, hakuna haja ya Wananchi kuwa na hofu ya upatikanaji wa chakula”

“Wito wangu kwa Wafanyabiashara wauze chakula kwa bei elekezi ya Serikali na waache kuficha chakula kitendo hicho hakitovumiliwa , Wananchi mtoe ushirikiano kwa Vyombo husika ili kuhakikisha hakuna Mfanyabiashara anayekwenda kinyume na maagizo”
Screenshot_20230323_044705_OGInsta%2B.jpg
 
Mtu mmoja amenusurika kifo baada ya gari alilokuwa akiendesha kuacha njia na kupinduka kwenye mtaro katika Mji wa Babati Mkoani Manyara.

Gari hilo (Harrier) lililokuwa likiendeshwa na Dereva ambaye bado hajafahamika jina lake limeanguka kwenye mtaro katika Mji wa Babati Mkoa wa Manyara.

@Ayotv_ imefika eneo la tukio kuongea na Mashuhuda wa ajali hiyo ambapo mmoja amenukuliwa akisema “Nilikuwa nimesimama hapa nikashangaa gari imetoka huko ikiwa inayumbayumba ikapiga Kalvati kwa kishindo kikubwa ndipo ikaruka juu ya kupinduka, nikawaambia wenzangu tumuokoe huyu Jamaa mbona tumeona kimya ila Jamaa akatoka mwenyewe tukamuuliza akasema hajaumia ila Sasa hatujui yupo wapi maana wengine wanasema ametoroka"

"Jamaa anaonekana alikuwa anachati kwenye simu yake ila hakuwa speed sana bahati mbaya gari likahama ndipo likagonga kalvati na kupaa juu na kugeuka kisha kuanguka kwenye mtaro ila Jamaa ameweza kutoka kupitia mlango wa abiria"

Hakuna aliyepoteza maisha katika ajali hiyo ambapo jitihada za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara zinaendelea.
Screenshot_20230323_045459_OGInsta%2B.jpg
 
Kamanda wa zamani wa Jeshi la Ardhini la Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba ambaye pia ni Mtoto wa Rais Museveni, amesema Kampuni za kigeni ambazo zinataka kuondoka Uganda kisa muswada wa kupinga mapenzi ya jinsia moja uliopitishwa na Bunge la Nchi hiyo, waondoke tu tena watawasaidia kupack mabegi yao.

Muhooz amenukuliwa akisema “Nasikia kuna Kampuni za kigeni (Sijui ni Kampuni gani) zinataka kuondoka Uganda kisa tu tumepitisha muswada wa kupinga mapenzi ya jinsia moja, tupo tayari kuwasaidia kupack mabegi yao na waondoke kwenye Taifa letu lenye baraka, tena wasirudi milele, Uganda ni Taifa la Mungu na Taifa litastawi bila wao”

Itakumbukwa Bunge la Uganda jana Jumanne March 21,2023 limepitisha muswada wa sheria wa kupinga vitendo vya kufanya mapenzi ya jinsia moja ambapo kama Rais Museveni atausaini kuwa sheria Mtu yoyote anayehusika na vitendo vya kufanya mapenzi ya jinsia moja au yeyote atakayejitambulisha hadharani kama Mwanachama wa kundi la LGBTQ anaweza kukabiliwa na kifungo cha hadi miaka 10 jela.

Sheria hiyo inapendekeza hatua mpya kali zichukuliwe kwa Watu wanaojihusisha na mahusiano ya aina hiyo nchini Uganda ambako ushoga ni kitendo kisichokubalika, chini ya sheria inayopendekezwa, Marafiki, Familia na Wanajamii watakuwa na wajibu wa kuripoti Watu walio katika mahusiano ya jinsia moja kwa Mamlaka mbalimbali za kisheria.
Screenshot_20230323_045613_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Innocent Bashungwa @innocentbash amesema maagizo ya Rais wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. Samia ya kupeleka misaada kwa Nchi ya Malawi iliyokumbwa na Kimbunga Freddy, yanaendelea kutekelezwa huku akimpongeza Mkuu wa Majeshi Jenerali Jacob John Mkunda na Makamanda wengine kwa kasi ya upelekaji huo wa chakula na misaada mingine Malawi.

Akiongea wakati alipofika kukagua usafirishaji wa chakula kwenye Ofisi za Wakala Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Jijini Dodoma, Bashungwa amesema “Maelekezo ya Rais kwenye msaada unaoenda Malawi, alielekeza logistics zisimamiwe na kuratibiwa na Jeshi la Wananchi Tanzania, nimefika kwenye eneo ambalo Jeshi linapokea misaada kwa ajili ya Malawi, nampongeza Mkuu wa Majeshi Jenerali Jacob John Mkunda na Makamanda wote wanaomsaidia kwa namna ambavyo wamepokea maelekezo ya Rais na kuyasimamia vizuri”

"Ndani ya muda ambao Rais ameelekeza misaada hii kutoka Tanzania kwenda Malawi tutaipeleka kwa wakati kama tulivyoelekezwa na Mh.Rais na Amiri Jeshi Mkuu, nampongeza Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dr.Tax kwa kushirikiana na Wizara yetu kulikamilisha hili”
Screenshot_20230323_050348_OGInsta%2B.jpg
 
Huu ni muonekano wa jengo la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Mpanda litakapokamilika, gharama ya mradi ni takribani Tsh. Bilioni 1.4 na jengo litakapokamilika litakuwa na uwezo wa kuhudumia abiria 240 kwa wakati mmoja.

Mkandarasi amekabidhiwa eneo la mradi Machi 2023 na unatarajiwa kujengwa kwa mwaka mmoja na Kampuni ya Ujenzi ni Wesons Engineering Limited.
Screenshot_20230323_050510_OGInsta%2B.jpg
 
Ripoti ya pili ya uchunguzi wa ajali ya ndege ya Precision Air iliyotokea Novemba 6, 2022 na kusababisha vifo vya watu 19 na majeruhi 24 imebaini mambo nane.

Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Uchunguzi wa Ajali za Ndege, Redemptus Bugomola amesema ripoti ya kwanza walikwenda na kushuhudia eneo la tukio na kuona ndege ilivyoumia, “na hii ya pili, tumekwenda mbele zaidi kwa kuangalia vinasa sauti.”

Mambo hayo nane ni;
1. Ndege ilikuwa imeandikishwa kihalali.
2. Marubani wa ndege hiyo hawakuwa na tatizo la kiafya.
3. Hali ya hewa katika uwanja wa ndege wa Bukoba haikuwa nzuri.
4. Hali mbaya ya hewa iliathiri marubani kutekeleza jukumu lao.
5. Marubani hawakutilia maanani ishara za tahadhari zilizotolewa.
6. Ndege iligonga kwanza bawa lake la kushoto wakati ikianguka.
7. Pia, ilianguka kwa kasi na kugonga sehemu ya mbele kwenye kina cha maji ya ziwa.
8. Vifaa vyote vya kuongezea ndege vilikuwa vinafanyakazi kwa kuzingatia matakwa ya rubani.

Ripoti ya awali ya ajali hiyo ilitoka Novemba 23, 2022 ilichambua mambo mbalimbali ya kitaalamu yaliyotokea wakati wa ajali hiyo.
Screenshot_20230323_050704_OGInsta%2B.jpg
 
"Niipongeze Yanga kwa kufika hatua hii ya robo fainali kwenye Kombe la Shirikisho Afrika maana walikuwa wamelala sana wakiamini kuifunga Simba ilikuwa ndio mafanikio kwao,

"Mpira wa nchi hii umepiga hatua kubwa kwa timu za Simba na Yanga kufuzu robo fainali kwa sababu ni kwa mara ya kwanza lakini pia kuna nchi utaona ina timu moja tu kwenye hii hatua sasa hili ni jukumu letu kubwa la kuhakikisha tunaendelea kushikilia hapa tulipo." Ahmed Ally, Ofisa Habari wa Klabu ya Simba akichangia mada kwenye Twitter Space iliyoandaliwa na Mwananchi Communications Ltd.
Screenshot_20230323_050819_OGInsta%2B.jpg
 
"Kitendo cha Simba na Yanga kuingia hatua ya robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho Afrika ni mafanikio makubwa kwa upande wa Bodi ya Ligi (TPLB) kutokana na wao kuitangaza vyema Ligi yetu," Katibu Mkuu wa Zamani wa TFF, Angetile Osiah.
Screenshot_20230323_050918_OGInsta%2B.jpg
 
"Kitendo cha Simba na Yanga kuingia hatua ya robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho Afrika ni mafanikio makubwa kwa upande wa Bodi ya Ligi (TPLB) kutokana na wao kuitangaza vyema Ligi yetu," Katibu Mkuu wa Zamani wa TFF, Angetile Osiah.
Screenshot_20230323_050918_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom