Makapuku Forum

Makapuku Forum

Marekani imeonya kwamba Ulimwengu haupaswi kudanganywa na hatua za China kusema kwamba haiegemei upande wowote kwenye vita ya Urusi na Ukraine ambapo Marekani imesema China inamuunga mkono Putin na inaiuzia silaha Urusi.

China imekanusha vikali madai hayo tangu kuanza kwa vita ya Urusi na Ukraine mwaka jana ambapo Rais wa China Xi Jinping amesema mahusiano ya karibu kati ya Urusi na China yanahusu malengo na majukumu mengi ya pamoja na sio kwamba wanaunga mkono Urusi kwenye vita hiyo ambapo China imesisitiza inataka vita hiyo iishe kwa amani.

Katika hatua nyingine Rais Vladmir Putin amemwambia mwenzake wa China Xi Jinping kuwa Urusi iko tayari kuyajadili mapendekezo ya China ya kumaliza mapigano nchini Ukraine, Putin amesema hayo jana mwanzoni mwa mazungumzo kati ya Marais hao nchini Urusi wakati huu ambapo Rais wa China yupo Urusi kwenye ziara yake ya kikazi.

Mkutano wa Marais hao umefanyika wakati China ikitafuta kujiweka kama Nchi isiyoegemea upande wowote katika vita hivyo, Putin na Xi Jinping watakutana tena leo kwa mazungumzo rasmi.
Screenshot_20230321_144418_OGInsta%2B.jpg
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa amesema Treni ya Mwendokasi inatarajia kuanza safari kwa kipande kilichokamilika mwishoni mwa mwezi April au mwazoni mwa mwezi May mwaka huu.

Kadogosa amesema hilo Jijini Dodoma mara baada ya kuwasili kwa msafara wa Wajumbe wa Baraza Kuu la Wanawake wa CCM waliotumia usafiri wa Treni ya Mkandarasi kutokea Dar es salaam hadi Dodoma ili kushuhudia mwenendo wa ujenzi wa Reli ya kisasa (SGR).

Kadogosa amesema “Hatutapandisha kwanza Abiria kuna matakwa ya kisheria ambayo tunafuata LATRA ambao wanatakiwa wafanye ukaguzi wao wakishajiridhisha kwenye mifumo tutweza kuanza, pia tuna suala la bei ambalo wanashirikisha Wananchi sehemu mbalimbali tunapofika”
Screenshot_20230321_144514_OGInsta%2B.jpg
 
Serikali ya Urusi imewaambia Maafisa waliohusika katika maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2024 wa nchini humo kuacha kutumia simu za iPhone ambazo ni za kampuni ya Marekani ya Apple kwa sababu ya wasiwasi kwamba vifaa hivyo vinaweza kudukuliwa na Mashirika ya kijasusi ya Magharibi.

Katika semina iliyoandaliwa na Serikali ya Urusi kwa Maafisa wanaohusika na siasa za ndani ya Nchi hiyo, Sergei Kiriyenko ambae ni Naibu Mkuu wa kwanza wa utawala wa Rais, aliwataka Maafisa hao kubadilisha simu zao ifikapo April 1, 2023.

Kwa upande mwingine, Msemaji wa Serikali ya Urusi Dmitry Peskov aliwaambia Waandishi wa Habari kuwa simu janja (smart phones) hazipaswi kutumika katika masuala rasmi ya kitaifa kwani zinahofiwa kudukuliwa kudukuliwa kutokana na mifumo yake bila kujali ni mfumo gani wa uendeshaji iwe ni android au iOS.

Rais Vladimir Putin wa Urusi alisema kuwa yeye binafsi hatumii smartphone na vilevile Peskov amenukuliwa akisema Rais huyo hutumia mtandao wa Internet mara chache japo rekodi kadhaa za baada ya Urusi kuanza vita yake nchini Ukraine mwaka jana, Majasusi wa Marekani na Uingereza walidai kufichua na kuweka hadharani mpango mzima wa Putin kutaka kuivamia Ukraine lakini haijulikani ni jinsi gani Majasusi hao walipata taarifa hizo.
Screenshot_20230321_144612_OGInsta%2B.jpg
 
VINARA WA UFUNGAJI CAFCC 22/23
.
4—️ Paul Acquah (Rivers United)
3—️ Fiston Mayele (Yanga SC)
3—️ Mostafa Fathi (Pyramids)
Screenshot_20230321_144728_OGInsta%2B.jpg
 
CHAMA AMDUWAZA BEKI HOROYA

KIUNGO fundi wa mpira wa Simba, Clatous Chama yuko juu katika orodha ya wafungaji mabao wa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi akiwa na manne sawa na Makabi Lilepo wa Al Hilal ya Sudan, huku beki wa Horoya ambaye ni mrefu Mohamed Fofana ametoa kauli ya kuumizwa na Mzambia huyo.
.
“Nadhani yule aliyevaa jezi namba 17 (Chama) ni mchezaji hatari sana amesababisha matatizo makubwa sana kwenye eneo letu la ulinzi na hata katikati.
.
“Alikuwa na mbio ambazo tulishindwa kumdhibiti vizuri, lakini kitu kibaya zaidi ni utulivu wake anapokuwa na mpira, hana papara wala hachezi kwa presha kama wenzake, tumelazimika kukubali matokeo. Ukiangalia mabao yote aliyoyafunga utagundua utulivu wa akili yake, ameisaidia timu yake nafikiri kitu bora tumejifunza tutarudi kujipanga kwa mashindano yajayo.”
Screenshot_20230321_144822_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo amesema Serikali itatoa kiasi cha Sh 500 milioni endapo timu ya Taifa Stars itafuzu fainali za AFCON 2023.
.
WADAU ongezeni dua kwa Stars .!!
Screenshot_20230321_145109_OGInsta%2B.jpg
 
INADAIWA mbali na kuhusishwa na timu mbalimbali za Uarabuni na Marekani, taarifa za ndani zinadai staa wa PSG na Argentina Lionel Messi, 35, huenda akarejea tena Barcelona katika dirisha lijalo la majira ya kiangazi kutokana na mawasiliano ya karibu aliyonayo kwa sasa na kocha wa wababe hao Xavi Hernandez.
.
Mkataba wa Messi unaisha mwisho wa msimu huu na bado haijafahamika kama ataendelea na maisha ya Paris.
Screenshot_20230321_145244_OGInsta%2B.jpg
 
ANATISHA
.
12—BUKAYO Saka (+10G +10A) ni mchezaji wa kwanza wa Arsenal kufikisha mabao 10 na asisti 10 katika msimu wa EPL tangu Alexis Sanchez (2016-17); kiujumla Saka ni mchezaji pekee kuwa na takwimu hizo msimu huu katika EPL nzima. Kafunga mabao 12 EPL.
Screenshot_20230321_145355_OGInsta%2B.jpg
 
CHELSEA INATAFUTA UWANJA
.
Jirani yako ndio nduguyo wanasema. Ndicho unachoweza kusema baada ya Chelsea kuripotiwa kuwa na mpango wa kuwafuata wapinzani wao kwenye Ligi Kuu England, Fulham kwenda kuwaomba watumie uwanja mmoja wa mechi zao za nyumbani wakati watakapofanya maboresho ya Uwanja wa Stamford Bridge.
.
The Blues wanapanga kuwaomba Fulham ili watumie Uwanja wa Craven Cottage kwa kipindi cha miaka minne kwa mechi zao za nyumbani kwenye Ligi Kuu England. Mmiliki wa Chelsea, bilionea Todd Boehly na mmiliki mwenza, Behdad Eghbali wamepanga kuifanya The Blues kuwa moja ya timu zenye viwanja matata kabisa duniani hadi ikifikapo mwaka 2030.
.
Kinachoelezwa ni kwamba Chelsea kwa sasa ina machaguo matatu juu ya mipango ya uwanja wao itakaotumia kwa ajili ya mechi zao za nyumbani. Chaguo la kwanza la mpango wao ni kujenga uwanja mpya kwenye eneo jipya kabisa. Chaguo la pili la mpango wao ni kuubomoa wote Stamford Bridge na kuujenga upya kabisa, wakati mpango wao wa tatu ni kuufanyia maboresho tu na kuufanya kuwa kwenye muonekano wa kisasa
Screenshot_20230321_145447_OGInsta%2B.jpg
 
“Kwa Horoya ilikuwa rahisi kwa Simba kufanya kila walichotaka uwanjani kwa sababu wapinzani wao walionekana kuwa DHAIFU na hawakuwa na mipango madhubuti. Hata katika pambano la kwanza kule Conakry, Simba hawakustahili kupoteza pointi tatu kama kina John Bocco wangekuwa makini.
.
Lakini sasa wanaenda kukutana na timu kali zaidi (Robo Fainali) Wanaweza kulitumia pambano la marudiano dhidi ya Raja pale Casablanca kama mfano wa namna wanavyoweza kucheza na timu kubwa katika hatua inayofuata (Robo)” - Edo Kumwembe [via Mwanaspot]
Screenshot_20230321_145616_OGInsta%2B.jpg
 
KOCHA Antonio Conte amewaudhi mastaa wa Totteham Hotsputs kuafuatia kauli dhidi yao na taarifa zimedai hawamtaki kwenye timu. Kocha huyo amerejea Italia kwa ajili ya mapumziko mafupi kupisha mechi za kimataifa ambazo zitachezwa wiki hii.
.
Taarifa zinadai kuna uwezekano mkubwa mwenyekiti wa Spurs, Daniel Levy akamfukuza kazi Muitaliano huyo mwenye maneno mengi. Vilevile wapo mastaa ambao wangependa kuona anaondolewa kipindi hiki cha mapumziko ya mechi za kimataifa. Conte aliwaponda wachezaji wake akidai hawajitumi uwanjani.
.
“Wachezaji hawajitumi kabisa kwasababu hawaoni umuhimu wa mechi wanayocheza. Tottenham imezoea kucheza hivyo. Wachezaji hawapendi kucheza kwa presha. Kila mechi wanayocheza wanachukulia kawaida. Hii ndio historia ya klabu hii. Kila siku nawaambia nataka wachezaji wapambane, sio mazoezini tu hata uwanjani,” alisema Conte.
.
Wadau wa soka England wanajiuliza maswali kufuatia kauli hiyo wengi wakidai Conte ameikosea heshima klabu na hakupaswa kuzungumza hivyo. Spurs mara ya mwisho kubeba Kombe ilikuwa Carabao 2008.
Screenshot_20230321_145705_OGInsta%2B.jpg
 
Sports Arena Tz

KILA nikiwafikiria Mamelodi Sundowns siombei wakutane na Simba kwenye Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Jamaa wanatisha balaa. Ni bora wakutane na kinara wa kundi A ambaye kuna uwezekano mkubwa akawa Wydad au kinara wa kundi D ambaye kuna uwezekano mkubwa akawa ni Esperance
.
Licha ya ubishi wote ambao umekuwepo, kwenye hili la Mamelodi nakataa, Jamaa kwanza wana bonge la timu halafu limeundwa na kundi kubwa la wachezaji wa nyumbani kwao lakini wengi wamekulia katika njia sahihi za kimpira maana kule Afrika Kusini kuna vituo vya soka la vijana vingi kuliko hata idadi ya timu zao.
.
Safu yao ya ulinzi sio tishio sana ila tatizo kubwa ni ile safu yao ya kiungo na ushambuliaji. Ina watu wana njaa kweli na kumpiga mtu nne, tano na hata sita kwao ni jambo la kawaida wakiongozwa na yule Mnamibia, Peter Shalulile.
.
Sawa Simba inaweza kupata bao au hata mabao dhidi yao lakini je kwa ile beki ya Simba inaweza kuwazuia wale wasifunge?
.
Inaendelea ..
Screenshot_20230321_145835_OGInsta%2B.jpg
 
Sports Arena Tz

KINACHONIPA wasiwasi zaidi ni kasi ya wale watu wao pale mbele, wanaoweza kumiliki mpira na kupiga pasi za haraka haraka. Kama hauna ukuta imara, basi angalau unapaswa kuwa na kiungo/viungo mahiri wa ulinzi wa kupunguza athari yao.
.
Mbaya zaidi Mamelodi wale jamaa hawamtegemei mchezaji mmoja katika kufunga mabao. Katika mabao 11 waliyofunga hadi sasa, wachezaji saba tofauti wamefunga na kati yao kuna washambuliaji, viungo na hadi mabeki. Halafu nawakumbusha jamani, wale Mamelodi huwezi kuwadhulumu kirahisi maana bosi wao ndio Rais wa CAF.
.
Ukiwadhulumu jua cha moto utakipata. Ukipangwa kucheza na wale jamaa unapaswa kujipanga vilivyo ili wasikutoe na kukuaibisha vinginevyo ukijichanganya wanaweza kukupiga 10 wale nimekaa paleeeeeeee.

#EnjoySoccer
Screenshot_20230321_145940_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa zamani wa CAF, Ahmad Ahmad amemaliza kifungo chake na kuamua kutema nyongo kuhusu mahusiano ya CAF na FIFA akiyaita ya 'kibeberu' na sio ya kuusaidia mpira wa Afrika!

Ametoa kauli hiyo mara tu baada ya kumaliza kifungo chake cha miaka miwili alichokuwa anakitumikia kutokana na kufungiwa kujihusisha na masuala ya soka kwa sababu mbalimbali. Moja kati ya sababu ni matumizi mabaya ya ofisi yake akiwa Rais wa CAF.

Mwaka 2020 Kamati ya Maadili ya FIFA ilimfungia miaka mitano lakini Ahmad alikata rufaa kwenye Mahakama ya Usuluhishi wa masuala ya Michezo CAS adhabu ikapunguzwa toka miaka mitano hadi miwili.

Sababu ya yeye kufungiwa anaiita ni sababu ya kisiasa kwenye mpira! Kwa sababu alitofautiana na Rais wa FIFA Gianni Infantino.

Walitofautiana nini? Infantino kwa kujua fika Bara la Afrika lina mtaji wa kura nyingi, ameamua kuliweka karibu.

Mkasa unarudi nyuma kidogo tangu Infantino aliposhinda kiti cha Urais wa FIFA mwaka 2016, moja ya ajenda zake ilikuwa ni kumuondoa madarakani aliyekuwa Rais wa CAF Mzee Issah Hayatou ambaye aliongoza kwa miaka 29.

Baada ya kufanikiwa kumtoa, Infantino alimwambia Ahmad Ahmad agombee Urais wa CAF! Ahmad akashinda uchaguzi na kuwa boss wa CAF.

Mikakati ya Infantino ilikuwa ni namna gani ataweza kuhudumu kwenye kiti cha Urais wa FIFA kwa muda mrefu, ndio maana akaliweka karibu Bara la Afrika kwa sababu lina mtaji mkubwa wa kura! Akaleta sera ya FIFA kuendesha baadhi ya maeneo ya CAF kimkakati ili kusaidia soka la Afrika kukua.

Akamleta mwanamama Fatma Samoura kwenye eneo la fedha na utawala [CAF] ili kusaidia uendeshaji wa shughuli za CAF.

Ahmad baada ya kupokea hiyo taarifa akawaruhusu kuingia kwenye mifumo ya CAF kufanya shughuli za Utawala na Fedha huku akiamini baada ya muda wataondoka wakiwa wamewaachia uzoefu watendaji wengine wa CAF.

Siku moja wakiwa kwenye kikao, Ahmad akamchana Infantino kwamba kwa sasa CAF inaweza kujiendesha kwa hiyo wale wataalam wanaweza kusepa! Kauli ile ilimkwaza Infantino akasusia kiao akaondoka bila kuaga moja kwa moja airport akasepa

Na hapo ndipo likaanzia anguko la Ahmad Ahmad, zikaanza kuzaliwa kesi juu ya utawala wake na makandokando! Mwisho wa siku akafungiwa.
Screenshot_20230321_150338_OGInsta%2B.jpg
 
Kiungo Feisal Salum akiwa na msafara wa mastaa wa Yanga ambao wamewasili Misri kujiunga na kikosi cha Taifa Stars kinachojiandaa na michezo miwili ya kufuzu AFCON 2023 dhidi ya Uganda.

Kundi hilo la wachezaji ndio la mwisho lililokuwa linasubiriwa kukamilisha kikosi cha wachezaji 31 walioitwa na Kocha Adel Amrouche.
Screenshot_20230321_150512_OGInsta%2B.jpg
 
Mmoja kati ya watu watano waliofariki dunia kwa ugonjwa wa ajabu katika Kata ya Maruku na Kanyangereko Bukoba vijijini, mkoani Kagera alikuwa bwana harusi mtarajiwa.

Watu hao waliofariki dunia ni kati ya saba walioripotiwa kuwa na ugonjwa huo huku wakiwa na dalili za homa, kutapika, kutokwa damu maeneo mbalimbali ya mwili na figo kushindwa kufanya kazi.

Taarifa ambazo gazeti hili limezipata kutoka kwa ndugu wa karibu ni kwamba kati ya waliofariki ambao tayari miili yao imezikwa alitarajiwa kufunga ndoa Aprili mwaka huu.

Bwana harusi huyo mtarajiwa, Benson Rutabingwa alifikwa na mauti Machi 15 baada ya kuugua ugonjwa huo unaosemekana aliupata kwa ndugu zake watatu ambao ni miongoni mwa watano walioripotiwa kufariki dunia.

Screenshot_20230321_150608_OGInsta%2B.jpg
 
Sakata la mchungaji mmoja nchini Uganda (jina limehifadhiwa) aliyefunga kanisa baada ya kushinda Sh100 milioni kwenye mchezo wa bahati nasibu, limewaibua viongozi wa kiroho huku kila mmoja akija na mtazamo wa tofauti.

Machi 16, mwaka huu mtandao mmoja Uganda ulichapisha taarifa za mchungaji huyo akieleza kuwa ameamua kufunga kanisa lake ili afanye shughuli nyingine kwa kuwa amepata fedha nyingi.

Mtandao huo ulimnukuu mchungaji akieleza namna alivyocheza bahati nasibu ya Sh1 milioni lakini akashinda Sh100 milioni ambazo hakutarajia kama angepata.

“I must admit that I opened this church due to greed but not anointing (lazima nikiri nilifungua kanisa hili kwa sababu ya ‘kiroho’ lakini sio upako) inasema sehemu ya habari hiyo ikimnukuu mchungaji huyo.
Screenshot_20230321_150719_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amesema upimaji wa sampuli za waliogua ugonjwa uliokuwa haujulikani Wilayani Bukoba, Kagera ambao umeua Watu watano umethibitisha ugonjwa huo ni ugonjwa wa Marburg ambao unasababishwa na virusi vya Marburg ambapo amesema mpaka sasa waliopata ugonjwa huo ni wanane na kati ya hao waliofariki ni watano.

“Hadi kufikia leo ikiwa ni siku tano tangu kuripotiwa kwa Watu wenye dalili jumla ya Watu waliothibitika kuwa na ugonjwa huu ni nane na kati yao vifo ni vitano, Wagonjwa watatu wanaendelea kupatiwa matibabu katika vituo vilivyoandaliwa Mkoani Kagera, kwa niaba ya Serikali natoa pole kwa walioguswa na msiba huu”

“Dalili za ugonjwa huu ni homa, kuumwa kichwa, maumivu ya misuli, kuishiwa nguvu, kutapika, kuharisha, kutokwa damu maeneo ya wazi n.k”

“Niwatoe hofu Watanzania kuwa hadi sasa Serikali yetu imefanikiwa kudhibiti kasi ya maambukizi mapya ya ugonjwa huu na haujatoka nje ya eneo lililoripotiwa ambalo ni Mkoani Kagera Wilayani Bukoba”
Screenshot_20230322_040311_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema uchunguzi wa Maabara ya Taifa umethibitisha uwepo wa virusi vya Marburg ambavyo vinasababisha ugonjwa wa Marburg Virus Disease (MVD) katika Mkoa wa Kagera ambao umesababisha vifo vya Watu watano hadi sasa ambapo amesema Ugonjwa huo hauna tiba mahususi bali hutibiwa kwa dalili anazokuwa nazo Mgonjwa.

Akiongea leo Dar es salaam, Ummy amesema “Uchunguzi ambao tumeufanya katika Maabara yetu ya Taifa ya Afya ya Jamii umethibitisha uwepo wa virusi vya Marburg ambavyo vinasababisha ugonjwa unaojulikana kama Marburg Virus Disease(MVD)”

“Kwa mujibu wa taarifa za Shirika la Afya Duniani (WHO), ugonjwa huu wa Marburg uligundulika kwa mara ya kwanza Ujerumani mwaka 1967 katika Mji wa Marburg na ndio asili ya jina la ugonjwa huu, ugonjwa huu ulishawahi kuripotiwa katika Nchi mbalimbali za Afrika na Ulaya”

“Ugonjwa huu huambukizwa kutoka kwa Binadamu mmoja kwa mwingine hususani kwa njia ya kugusa majimaji ambayo yanaweza kuwa mate , mkojo, damu, machozi au kinyesi yatokayo kwenye maiti au Mgonjwa mwenye dalili, maambukizi pia yanaweza kutoka kwa Wanyama kwenda kwa Binadamu iwapo Mtu atakula au kugusa mizoga au Wanyama walioambukizwa”

Itakumbukwa siku tano zilizopita Serikali kupitia Wizara ya Afya ilitoa tahadhari juu ya uwepo wa ugonjwa ambao bado ulikuwa haujajulikana Mkoani Kagera katika Wilaya ya Bukoba Vijijini ambapo Watu 7 walisadikika kupata dalili za homa, kutapika, kutokwa damu maeneo mbalimbali ya mwili na figo kushindwa kufanya kazi na Watu watano kati yao wakaripotiwa kufariki.
Screenshot_20230322_040414_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom