Makapuku Forum

Makapuku Forum

Magazeti ya leo January 14 2023
Screenshot_20230114_062122_Opera%20Mini.jpg
 
OLD TRAFFORD KUBOMOLEWA
.
Uwanja wa Old Trafford utabomolewa na kujengwa upya kwa teknolojia za kisasa kufuatia mapendekezo yaliyotolewa, kwa mujibu wa ripoti.
.
Gharama za ujenzi za uwanja mpya wa Old Trafford inatajwa kuwa ni Pauni 2 bilioni (Sh 5.7 trilioni) hadi utakapokamilika.
.
Watendaji wa United waliwasilisha mapendekezo mawili. Pendekezo la kwanza ni kuufanyia ukarabati Uwanja wa Old Trafford huku pendekezo jingine ni kuuuvunja kabisa na kujenga uwanja mpya wa kisasa. Mchakato wa ukarabati ulitakiwa kuanza tangu mwaka jana lakini walizingatia gharama kwasababu jambo hilo litagharimu pesa ndefu na ndio sababu wanaona kama vipi uvunjwe ujengwe wa kisasa.
.
Hata hivyo, mpango huo umesimama
hadi mmiliki mpya atakapopatikana baada ya klabu hiyo kuwekwa sokoni na familia ya Glazers. Uwanja wa Old Trafford una uwezo wa kuingiza mashabiki 74,310 na mwaka uliopita 2022 ndo umeongoza kwa kuwa na wastani wa kuingiza idadi kubwa ya mashabiki katika Ligi 5 kubwa Ulaya.
Screenshot_20230114_063236_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan JR

KENNEDY MUSONDA, ving’amuzi viwe tayari, mitaa iwe tayari na banda umiza mpaka Buza kwa Ujugu wawe tayari! The streets have to get used to this name, amewasili kwenye Premier League! Ni Muisrael wa mpira aliyevushwa na Musa wa soka Hersi Said kuja nchi ya ahadi, you feel me?

Mazembe walisukuma kete yao atue Lubumbashi lakini dakika kadhaa za Uwanja wa ndege wa Simon Mwansa Kapwewe alizoketi na Engineer wakati ana tiketi yake kuelekea Lubumbashi ilitosha kumwona Dar Es Salaam, nyumbani kwa visingeli na Mahindi ya kuchoma kwa chumvi.

Wakati Hersi anakata tiketi kuelekea Zambia hakuna aliyeamini pale Salamander, atawezaje kuinasa saini ya Mchezaji mwenye mkataba na Power Dynamos? Hakueleweka kirahisi mission ngumu inayohitaji wagumu! Atawezaje kumleta Mchezaji ambaye TP Mazembe walishatuma nauli wakisubiri text ya “Nishukie wapi?”

President wa Yanga na imaan yake kama Daniel dhidi ya Simba alishacheza movie kali na akaibuka starring ile The Thriller in Abdijan na Aziz Ki akatua JK Nyerere kama mateka, he knew the principles of the game, he followed the rules and won the game.

Ameenda vizuri amecheza vizuri niliwahi kumpa kisa cha dunia ya Maengineer, nikampa kisa cha Luis Campos The Wizard of the Capital Gain, usiruhusu aongee na Mchezaji wako ndio makosa ambayo Musonda aliyafanya, kumpa tu sikio

Dakika tano alizopewa ya kwanza ilikuwa kumwonesha anamhitaji sana, ya pili ilikuwa ni project kubwa ya Yanga, ya tatu ni utayari wake wa kumalizana na Power Dynamos na kuvunja mkataba, ya nne ni PESA na tano ni PESA, hakuwa na pa kurukia Musonda! Hakuwa na neno kama IFM na watoto wakali, SUA na msuli au @official_simalengatz na watu wake wa Songwe.

Nataka kupumzika ila acha niseme! Imepigwa Mazembe kwenye ofa, ukavunjwa mkataba na klabu yake ya Power Dynamos, akala Air Tanzania mpaka Tanzania na amesaini na Wananchi, karibu sana Musonda kwenye ardhi ya Mwalimu Mzanaki wa Butiama, karibu Tanzania nchi ya Wachambuzi.

Screenshot_20230114_063551_OGInsta%2B.jpg
Screenshot_20230114_063607_OGInsta%2B.jpg
 
FT| NAPOLI 5-1 JUVENTUS

Osimhen ana mabao 12 anaongoza mbio za kiatu na Napoli wanaongoza mbio za ligi wamemwacha Milan kwa alama 10.
Screenshot_20230114_064553_OGInsta%2B.jpg
 
Amerejea tu kutoka kwenye mapambano dhidi ya saratani, Sebastian Haller leo hii amefunga mabao matatu ndani ya dakika nane tu dhidi ya FC Basel kwenye mchezo wa kirafiki.

The Hunter is back
Screenshot_20230114_065134_OGInsta%2B.jpg
 
Cristiano Ronaldo na familia yake wamepewa mualiko maalum na Real Madrid kuitazama fainali ya Spanish Supercup kati ya miamba hiyo dhidi ya Barcelona.

Licha ya kuwa Ronaldo alifika mazoezini na kuonana na staff nzima ya Madrid, lakini baadae wachezaji walienda Gym alipo CR7 na kupata nae picha za ukumbusho.
Screenshot_20230114_065300_OGInsta%2B.jpg
 
Metacha Mnata amejiunga na Yanga kwa mkopo akitokea Singida BS ambapo ataitumikia miamba hiyo ya Jangwani mpaka mwishoni mwa msimu kutokana na kuwa Golikipa namba mbili Abou Msheri ni majeruhi na atakuwa nje kwa muda kidogo.
Screenshot_20230116_043255_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom