Makapuku Forum

Makapuku Forum

Magazeti ya leo January 13 2023
Screenshot_20230113_061839_Opera%20Mini.jpg
 
MAJI YA SHINGO
.
—Dhidi ya Southampton, Manchester City juzi ilishindwa kupiga hata shuti moja lililolenga lango. Hii ilikuwa ni mara ya kwanza katika mechi 275 ilizocheza ndani ya siku 1743, tangu City ilipokumbana na kipigo cha mabao 3-0 dhidi ya Liverpool katika mechi yao ya Ligi ya Mabingwa Aprili 2018.
Screenshot_20230113_063918_OGInsta%2B.jpg
 
SEY KUILIPA GEITA GOLD SH 150,000
.
Klabu ya Dodoma Jiji imekamilisha usajili wa mshambuliaji wa zamani wa Namungo, Mghana Stephen Sey kwa ajili ya kuongeza nguvu huku ikitakiwa kuilipa Geita Gold kiasi cha Sh150,000, ikiwa ni nauli yake ya usafiri aliyopewa.
.
Sey alishindwana na Namungo katika dakika za mwishoni kwa kile kilichoelezwa kupandisha dau lake la usajili tofauti na lile walilokubaliana mwanzo, hivyo viongozi kuamua kuachana naye licha ya kupendekezwa na benchi la ufundi.
.
Wakati viongozi wa Namungo wakiachana na mpango huo, Geita Gold nayo ikajitosa kuhitaji saini ya Mghana huyo na rasmi ikamtumia nauli sh 150,000 alianza safari ya kwenda Geita ndipo akapokea simu ya mabosi wa Dodoma Jiji walioihitaji saini yake.
.
Wakala wa Sey anasema Kutokana na ofa waliyopokea wakaamua kujiunga na Dodoma Jiji, na kwakuwa wao ni waungwana watarudisha zile Sh150,000 ambazo viongozi wa Geita Gold walitutumia kama nauli ya kwenda kule.
Screenshot_20230113_064204_OGInsta%2B.jpg
 
SINGIDA YAMTEMA CEO
.
Uongozi wa Singida Big Stars umeachana na aliyekuwa Ofisa Mtendaji wake Mkuu, Dismas Ten baada ya kufikiwa uamuzi huo na viongozi.
.
Ten aliyekuwa Ofisa Habari wa Yanga aliteuliwa rasmi kuchukua cheo hicho Julai 26 mwaka jana, akichukua nafasi ya Muhibu Kanu aliyehamishiwa kitengo cha Mkurugenzi wa Masoko na Fedha na kuiwezesha kupata wadhamini wengi.
Screenshot_20230113_064252_OGInsta%2B.jpg
 
Mshambuliaji wa Simba, Moses Phiri ameanza mazoezi mepesi baada ya kuwa nje kutokana na majeraha aliyoyapata kwenye mechi ya ligi kuu.

Endapo atarejea mapema Simba wataongeza upana eneo la mwisho na ushindani wa mabao utaendelea.
Screenshot_20230113_064444_OGInsta%2B.jpg
 
Atletico Madrid wamemtumia barua rasmi Kipa wao wa zamani Thibaut Courtois ambaye kwasasa anakipiga Real Madrid kuwa abadili mitazamo na kauli zake dhidi yao endapo ataendelea basi watafuta jina lake na thamani yake kwenye klabu yao.
Screenshot_20230113_064700_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Nipe simulizi nzuri, simulizi kuhusu Kinjikitile na risasi kugeuka maji hiyo Hapana! Simulizi ya Chief Mangungo wa Msovero kuhusu mikataba na Carl Peters achana nayo, nipe simulizi nzuri.

Simulizi ambayo itaishi daima mbele ya Wajukuu zako, simulizi ambayo machozi yatakutoka na utakumbuka mchana wa jua kali Dar Es Salaam au usiku adhimu wa CAF Champions League wakati Mzambia akiwa uwanjani, tunaweza pata hizo simulizi?

Achana na simulizi za vita ya coursework za DS pale Mkwawa kwa Doctor Mlungu! Sahau kuhusu maisha ya Wema na Wanaume Mastaa! Simulizi ya Hamisa kuwa na watoto wawili wa Matajiri achana nazo, simulizi za Buga HAPANA kubaya huko.

Nipe simulizi nzuri za kueleweka, simulizi nzuri kama Mashairi ya Cheka Cheka, simulizi isiyouma kama Watoto wa Mama Ntilie, simulizi nzuri ya uhakika kama mshale wa saa na sekunde, nipe hizo simulizi nipo pae nimekaa.

Naileta hii hadithi wala sitaki mseme uongo uje na utamu ukolee! Bali mpira uje kwake na pass zitembee, hadithi nzuri na simuliI ya kuishi milele kuhusu Mwamba kutoka Kusini mwa Afrika, ardhi ya Keneth Wa Kaunda.

Ni simulizi ya kweli na uhakika! Kama ukisikia kikohozi na Konde Boy Mjeshi! Kama ukisikia Umepoa na Mwijaku, ubunifu na @cloudsfmtz ni simulizi ya kweli na uhakika katikati mwa miaka ya 2000 ni simulizi ya kweli kuhusu hiki kipaji.

Mnisamehe wajukuu zangu niwaachieni hii picha iliyopigwa na Bandeko wa Kigoma @rabbihume kumbukumbu anazo mpiga picha.

CHAMA 10:17-18 “Basi endeleeni kuzitama clip zake Azam TV, habari zake Simba App na picha zake magazetini ndio urithi wenu na faraja kwenu, alikuja kwetu kwa ajili ya soka, tukapendezwa nae mtazameni yeye” @realclatouschama

Kama umeupenda wimbo huu, bonyeza nyota utakuwa wa kwako! MMEENJOY
Screenshot_20230113_064832_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom