Makapuku Forum

Makapuku Forum

Nini kimetokea Auntie?
Mashangazi tumefanyaje tena?Mweh!!!

Maana mahali niko saa hii hata kumwambia mtu "muone" siwezi
Hata kumwambia mtu muone huwezi auntie nimecheka sanaaa

Bwana juzi kati nilikuwa chit chat nimepita tu kimyakimya kuna thread mtu anajipongeza kafikisha miaka kadhaa jf akataja forum za jf makapuku ikiwepo auntie

Sasa akatokea mkuu anaitwa poker acha atuseme vibaya ooh makapuku ilikuwa zamani sasa hivi wamejazana mashangazi wameiteka forum tu uko wanapiga tu story zao hakuna cha maana nikajisemea tu kimya kimya hivi hata magazeti na habari tofauti zinazopostiwa hazioni

Na hapohapo huyu poker anakuja sana makapuku kusoma habari zinazopostiwa nilivyoona likes zake imebidi tu nimwambie kama kuna tulichomkosea mashangazi wa makapuku tunamuomba msamaha sana halafu asiwe na roho ya kuchukia watu ambao hawajui wala hawajamkosea chochote sisi mashangazi wa makapuku hatunaga shida na mtu tunaishi kwa upendo na furaha na yeyote yule
 
Liz Truss: Waziri Mkuu aliyewaona Malkia na Mfalme ndani ya Wiki moja.

Ukisoma historia ya Taifa la Uingereza, utaona jinsi mapenzi yalivyo livuruga Taifa hilo. Mara kadhaa viongozi wakuu wa Taifa walivurugwa na mapenzi. Mfalme George VI alichepuka na mke wa mtu, aliposakamwa akaachia Ufalme akakimbia Marekani kuishi na mchepuko wake.

Hali kadhalika Waziri Mkuu wa sasa wa Uingereza Liz Truss mwkaa 2005 ilikuwa chupli chupli ndoa yake ivunjike baada ya kuchepuka na mbunge mwenzake. Ingawa ndoa yake haikuvunjika na mume wake kumsamehe lakini ndoa ya mchepuko wake ilisambaratika na sababu iliyotajwa ni kuwa na mahusiano nje ya ndoa.

Wakati Liz anapata kashfa ya kuchepuka alikuwa bado mbunge kijana na ndoa yake ilikuwa bado changa sana. Liz akaendelea na mapambano, hakukubali makosa yake yamrudishe nyuma.

Miaka ikaenda, bahati ya mtende hii hapa. Waziri Mkuu wa Uingereza akajiuzuru, chama chake kikampitisha kuwa Waziri Mkuu.

Jumanne ya Wiki hii Malkia akamteuwa Liz kuwa Waziri Mkuu. Siku mbili baadaye Malkia akafariki. Leo Liz amekula kiapo cha utiifu kwa Mfalme Charles. Liz ana umri wa miaka 46, na ni mama wa watoto wawili..!
Screenshot_20220911-050022_OGInsta%2B.jpg
 
Ni habari ambayo haijulikani sana, lakini ndiyo ukweli kwamba, miaka 70 iliyopita tangu Princess Elizabeth alipoambiwa kuhusu kifo cha baba yake, George VI akiwa safarini nchini Kenya katika hoteli ya Treetops.

Hoteli ya Treetops katikati mwa msitu wa Kenya inajulikana kama mahali ambapo Princess Elizabeth alipokea habari kwamba baba yake amefariki dunia na kwamba angekuwa Malkia wa Uingereza.

Wakati binti mfalme akiwa Treetops usiku ambao baba yake, George VI, alifariki dunia miaka 70 iliyopita, Jumatano ya Februari 6, 1952, hakuambiwa habari hizo hadi alasiri iliyofuata, wakati ambao alikuwa amerudi kwenye nyumba ya wavuvi iitwayo Sagana, umbali wa maili 20, ambayo alikuwa amepewa kama zawadi ya harusi.

Ilikuwa hapo, kando ya mkondo wa maji katika vilima vya Mlima Kenya, ambapo Prince Philip alitangaza habari hiyo.
Screenshot_20220911-050238_OGInsta%2B.jpg
 
Mazishi ya Malkia Elizabeth II wa Uingereza, yatafanyika Jumatatu ya Septemba 19, 2022 katika eneo la Westminster Abbey huko London.

Mwili wa Malkia utalala siku nne katika Ukumbi wa Westminster kuanzia Jumatano Septemba 14, ofisa mwandamizi katika Jumba la Kifalme amesema
Screenshot_20220911-050357_OGInsta%2B.jpg
 
Bondia Mtanzania @HassanMwakinyoJR_ amesema begi lake ambalo lilipotea Airport, Amsterdam likiwa na viatu vyake na vifaa vingine, limepatikana, itakumbukwa usiku wa Septemba 3, 2022 Mwakinyo katika pambano dhidi ya Muingereza Liam Smith lililochezwa Liverpool, England alipoteza kwa TKO round ya 4 katika pambano la round 12 ambalo hata hivyo lilikuwa gumzo kutokana na jinsi lilivyomalizika kwa utata.

Baada ya pambano hilo Mwakinyo akasema “Hujuma ambayo imetokea juzi wakati nafika Airport Watu wote walipata mabegi Mimi langu sikulipata karibu masaa matatu nimelisubiri baadaye wakaniambia begi langu limesahauliwa Amsterdam kwahiyo nikae pale masaa matano walilete au nitoe anuani ya napokaa watalituma baada ya siku mbili"

"Niliwasiliana na Promota akaniambia njoo uendelee na mambo mengine sisi tutashughulikia masuala ya begi lako, begi halijakuja juzi, jana na leo siku ya pambano wamenipa vifaa vingine vyao, viatu ambavyo nimevaa sijawahi kuvaa kupigania kuna muda nilipiga goti nikamwambia Refa nimepata ankle akaniambia unaweza kuendelea nikasema naweza kuendelea"

"Mara ya pili nikasikia ankle inakuja tena, nikatema mouth guard chini, sheria ukitema mouth guard Refa anatakiwa amrudishe nyuma Boxer unayepigana nae akuulize kuna tatizo gani au akuhesabia nikamwambia nina ankle akamaliza pambano"

Bondia Mtanzania Mwakinyo amesema kutokana na Refa wa pambano hilo kuwa ‘unfair’ kwake, Promota Benjamin Shalom amekubali pambano hilo lirudiwe January 2023 vs Liam Smith.
Screenshot_20220911-050633_OGInsta%2B.jpg
 
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeanza utaratibu wa kuwarejesha Watoto wa mitaani kuungana na Familia zao ili kupunguza wimbi la ongezeko la Watoto hao kwenye maeneo ya mijini kwa lengo la kuhakikisha kuwa wanapata malezi stahiki .

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima, amesema hayo wakati wa ziara ya kushtukiza aliyoifanya maeneo ya Ubungo mkoani Dar es Salaam ambapo alikutana na kikundi cha Watoto wa mitaani wanaoishi na kuombaomba maeneo hayo ya barabara na kulazimika kulala pembezoni mwa barabara hiyo ikiwemo juu ya miti kwa kufunga viota na kulala juu mithili ya ndege.

Akizungumza na Watoto hao wenye umri kati ya miaka 12 hadi 17, Waziri Dkt. Gwajima amesema Watoto hao wamechoka kuishi maisha ya kuombaomba na wako tayari kurejea mikoa waliyotoka ili kuungana na Familia zao kwa kuwa kupitia maisha hayo wamekutana na changamoto mbalimbali ikiwemo kutumiwa na baadhi ya Wananchi kuwafanyia biashara na kuwapa ujira mdogo, kujiunga na makundi ya Wavuta bangi na Watumiaji wa madawa ya kulevya, kushiriki vitendo vya wizi, ulawiti, ubakaji na kupata magonjwa mbalimbali ambayo yanahatarisha afya na kupoteza ndoto za maisha yao ya baadae..

Amewataka Watoto wote wa mitaani waliopo maeneo mbalimbali nchi nzima kutoa ushirikiano kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii ili Serikali kwa kushirikiana na wadau wengine ikiwemo wamiliki wa vyombo vya usafiri na Jeshi la Polisi kuwasafirisha watoto hao ili waungane na Familia zao.

Waziri Dkt. Gwajima amewataka Wazazi kusikiliza ndoto za Watoto wao na kubaini wanachohitaji ili waweze kusoma na kufikia malengo yao badala ya kuwapotezea malengo waliyonayo kwa ajili ya maisha yao ya baadae.
Screenshot_20220911-050734_OGInsta%2B.jpg
 
Polisi Mkoani Njombe wanamshikilia Happiness Mkolwe (27) Mkazi wa Ihanga Halmashauri ya Mji wa Njombe kwa tuhuma za kumuua Jackson Kihungo (6) Mtoto wa Shule ya Msingi Ihanga anayedaiwa kuwa ni Mtoto wa Mwanamke anayehusishwa kuwa na mahusiano na Mume wake (Mchepuko wa Mumewe).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Hamis Issah amesema Mwanamke huyo alimchukua Mtoto alipokuwa akitoka salumi na kumsababishia kifo na kumfukia kwenye takataka za mbao kabla ya kushtukiwa alipokuwa akichimba shimo kwa ajili ya kumfukia.

“Alivyomsababishia kifo alimvua nguo na kumpeleka kwenye takataka za mbao alikochimba na kumfukia kwasababu ni laini lakini haikutosha aliamua kuchimba kaburi pembeni ili amfukie, Mama huyu alishindwa kuendelea kwakuwa Watu waliona”

Kamanda Issah amesema sababu ya Mwanamke huyo kutekeleza mauaji hayo ni wivu wa mapenzi kutokana na kupewa taarifa kuwa Mume wake aliyetengana nae kwa muda anakunywa pombe na Mwanamke mwingine.
Screenshot_20220911-050835_OGInsta%2B.jpg
 
Anaitwa Conan Ledesma ni Golikipa wa Cadiz ambaye aliwahi mapema sana kuchukua hatua baada ya Shabiki kupata tatizo la moyo akiwa jukwaani, alikimbia kwa haraka mpaka kwa watu wa huduma ya kwanza na kubeba baadhi ya vifaa kisha akavitupa jukwaani ili huduma ya kwanza ianze.

Kumbuka hapo tayari ameshafungwa mabao mawili.

Respect 🫡 Conan!
Screenshot_20220911-050949_OGInsta%2B.jpg
 
Poker habari yako mkuu wangu hivi sisi mashangazi wa makapuku nini tumekukosea tukuombe hata msamaha kuna sehemu tuliona umetusema sana vibaya kupiga kwetu story ni shida kwako je hata habari tunazopost we huzioni kweli usiwe unatuchukia bila sababu mkuu usiwe na roho hiyo ya kuchukia watu tu mkuu sio vizuri kama kuna sehemu tuliwahi kukukosea sisi mashangazi wa makapuku tunaomba utusamehe.

Usimchukie hata siku moja mtu usiyemjua watu wenyewe tunaishi jf kwa I'd fake chuki ni kirusi kibaya sana mkuu kemea hiyo roho kama we ni mristo ikuondoke.
it's amazing, kumchukia mtu hapa Jf tena ndani na fake I'd naona ni kiwango kikubwa cha chuki , sijui huko kwenye jamii inayo mzunguka kwenye watu halisi kiwango cha chuki kwa mtu huyo kitakuwa vipi!!
 
OFFICIAL: Kocha Mkuu wa timu ya Singida Big Stars, Hans van der Pluijm amechaguliwa kuwa Kocha Bora wa mwezi Agosti wa Ligi Kuu ya NBC.
.
Pluijm amewashinda Zoran Maki wa Simba na Nasreddine Nabi wa Yanga.
Screenshot_20220911-051623_OGInsta%2B.jpg
 
it's amazing, kumchukia mtu hapa Jf tena ndani na fake I'd naona ni kiwango kikubwa cha chuki , sijui huko kwenye jamii inayo mzunguka kwenye watu halisi kiwango cha chuki kwa mtu huyo kitakuwa vipi!!
Inashangaza sana mkuu halafu huyo mtu ni mwanaume anayetusema sisi mashangazi wa makapuku ukimuuliza kwa nini anatuchukia hivyo jibu hana anabaki kimya na kila siku yupo makapuku kusoma habari zinazopostiwa acha tuishi nao hivyohivyo
 
Polisi Mkoani Njombe wanamshikilia Happiness Mkolwe (27) Mkazi wa Ihanga Halmashauri ya Mji wa Njombe kwa tuhuma za kumuua Jackson Kihungo (6) Mtoto wa Shule ya Msingi Ihanga anayedaiwa kuwa ni Mtoto wa Mwanamke anayehusishwa kuwa na mahusiano na Mume wake (Mchepuko wa Mumewe).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Hamis Issah amesema Mwanamke huyo alimchukua Mtoto alipokuwa akitoka salumi na kumsababishia kifo na kumfukia kwenye takataka za mbao kabla ya kushtukiwa alipokuwa akichimba shimo kwa ajili ya kumfukia.

“Alivyomsababishia kifo alimvua nguo na kumpeleka kwenye takataka za mbao alikochimba na kumfukia kwasababu ni laini lakini haikutosha aliamua kuchimba kaburi pembeni ili amfukie, Mama huyu alishindwa kuendelea kwakuwa Watu waliona”

Kamanda Issah amesema sababu ya Mwanamke huyo kutekeleza mauaji hayo ni wivu wa mapenzi kutokana na kupewa taarifa kuwa Mume wake aliyetengana nae kwa muda anakunywa pombe na Mwanamke mwingine.
View attachment 2353140
binti mdogo sana lakini amefikia maamuzi mabaya yanayoweza kugharimu furaha ya maisha yake yote!
 
Inashangaza sana mkuu halafu huyo mtu ni mwanaume anayetusema sisi mashangazi wa makapuku ukimuuliza kwa nini anatuchukia hivyo jibu hana anabaki kimya na kila siku yupo makapuku kusoma habari zinazopostiwa acha tuishi nao hivyohivyo
niliona hio comment ya huyo ndugu , na hata hakukua na sababu ya kusema hivyo kwenye mtiririko wa commet za ile mada, ila ni binadamu tulivyo ! tusipo sameheana na kuvumiliana hatufiki popote, so msamehe na kusonga mbele .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom