Huyu ndie Princess Diana, sasa hivi ndie angekuwa Malkia.
Sio pesa wala ukuu unaoweza kufanya ndoa yako idumu, bali heshima na upendo. Kama ungekuwa ukuu au pesa basi ndoa ya Diana na Charles isingekufa. Princess Diana alikutana kwa mara ya kwanza na Prince Charles akiwa binti mdogo kabisa mwenye umri wa miaka 16, wakati huo Prince Charles alikuwa anatoka na dada yake Diana. Diana alimpenda Charles, wakafanya mafekechee wakazama penzini japo kwa siri. Baadae wakahalalisha mahusiano yao na kufunga ndoa mwka 1981, Diana akiwa na miaka 20.
Sio kwamba Diana alitoka katika familia isiyokuwa na heshima, hapana, familia yake ni mojawapo ya familia zenye hadhi ya juu nchini Uingereza. Baada ya ndoa Diana alikuwa ni mwanamke wa Tatu mwenye heshima nchini Uingereza, baada ya Malkia na Mama yake Malkia.
Licha ya ukuu aliokuwa nao lakini Princess Diana hakuwa na furaha kwenye ndoa yake. Mume wake kuwa na mahusiano ya nje ilimtesa sana Diana. Mimba ya mtoto wake wa kwanza ikiwa na wiki 12, Diana alijirushwa kutoka kwenye ngazi na kuanguka, hata hivyo mimba haikurabika. Diana alisema alifanya hivyo kwa sababu alikuwa mpweke sana. Baada ya kujifungua mwanae wa kwanza Diana aliugua ugonjwa wa Sonona.
Baada ya miaka 5 ya ndoa kulikuwa na migogoro mikubwa sana ambayo haswa ilichangiwa na tofauti ya umri. Diana alikuwa na mchepuko wake wakati huo mumewe pia mahusiano yake na Camilla yalikuwa yamenoga. Migogoro na utofauti iliendeleq kukuwa na kupelekea ndoa yao kuvunjika miaka 15 baadae.
Akizungumza na mwandishi wa BBC, Diana alisema waliamua kutengena kwa sababu mahusiano yao yalikuwa kama ofisi ya umma, siku hizi mnasema Azam Burudani kwa Wote. Pia Diana alisema alikuwa ana mashaka sana kama Prince Charles alikuwa anafaa kuwa Mfalme wa Uingereza.
Baada ya kutengana Princess Diana alinasa kwenye penzi zito la mtoto wa Kiarabu, penzi lao halikudumu sana. Princess Diana alifariki dunia kutokana na majeraha aliyopata kutokana na ajali ya gari. Alifariki mwaka 1997, ikiwa ni mwaka mmoja baada ya kutalakiana na Charles. Princess Diana alifariki akiwa na umri wa miaka 36, katika ndoa yao walibahatika kupata watoto wawili ambao ni Prince William na Prince Harry.
View attachment 2351711