Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,978
KOCHA Mkuu wa kikosi cha timu ya wanawake cha Simba, Simba Queens, Sebastian Nkoma tayari ameshatinga kambi ya Simba iliyopo Lilongwe Malawi ili kuliongezea nguvu benchi la timu hiyo inayojiandaa kuivaana Nyasa Big Bullets ya Malawi katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Nkoma aliondoka asubuhi ya leo kwa usafiri wa shirika la ndege la Malawi na taarifa zilizopatikana ni kwamba tayari ameshatimba kambi ya timu hiyo iliyopo hoteli ya President Waltmont kuungana na Juma Mgunda na Seleman Matola waliotangulia mapema.
Taarifa kutoka ndani ya Simba zinasema kuwa Nkoma ameenda kuwa kama kocha wa viungo tofauti na taarifa ya awali iliyotoka klabuni humo ikieleza aliwahishwa huko ili kuokoa jahazi kutokana na sintofahamu ya kocha Mgunda mwenye kiwango cha elimu ya leseni A ya ukocha, japo ilidaiwa cheti chake kilikuwa hakijatoka.
Nkoma aliondoka asubuhi ya leo kwa usafiri wa shirika la ndege la Malawi na taarifa zilizopatikana ni kwamba tayari ameshatimba kambi ya timu hiyo iliyopo hoteli ya President Waltmont kuungana na Juma Mgunda na Seleman Matola waliotangulia mapema.
Taarifa kutoka ndani ya Simba zinasema kuwa Nkoma ameenda kuwa kama kocha wa viungo tofauti na taarifa ya awali iliyotoka klabuni humo ikieleza aliwahishwa huko ili kuokoa jahazi kutokana na sintofahamu ya kocha Mgunda mwenye kiwango cha elimu ya leseni A ya ukocha, japo ilidaiwa cheti chake kilikuwa hakijatoka.

| Kundi la Simba Queens kwenye michuano ya klabu bingwa barani Afrika itakayofanyika nchini Morocco.
Nick Mwenda amemwandikia barua Rais wa FIFA, Gianni Infantino kumwarifu kuwa tayari Mkurugenzi wa mashtaka wa Kenya ameondoa vikwazo dhidi yake na wapo tayari kuanza mazungumzo ya kurejea kwenye soka la kimataifa.
Farhan Jr