Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,978
Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha St. John Dodoma, Winfrida Michael (24), aliyekuwa anasoma Diploma ya Medical Laboratory amefariki dunia baada ya kushambuliwa kwa kuchomwa kisu na Mpenzi wake, Julius Gervas (26), RPC Dodoma Martin Otieno amethibitisha .
Winfrida alifariki wakati anapelekwa Hospitali baada ya kuwa amevuja damu nyingi na Julius baada ya kufanya tukio hilo alijaribu kujichoma kisu tumboni lakini Watu walimuwahi na kumchukua kisha kumpeleka Hospitalini ambako anaendelea na matibabu chini ya ulinzi.
Inaelezwa kuwa Winfrida alikuwa amepanga nje ya Chuo na alikuwa na mahusiano na Kijana huyo kwa muda fulani lakini walikuwa wameachana na Kijana alikuwa anamsumbua Msichama hivyo alimuahidi kuwa akimaliza mtihani atamjulisha.
Juzi Msichana alikuwa amemaliza mtihani wake wa mwisho na kwa mujibu wa Mama mwenye nyumba walikutana wakaongea sana pale ndani na ilipofika saa nne na nusu walitoka nje akawa anamsindikiza ndio lilipotokea tukio la kuchomwa kisu na akawa anaomba msaada na walimchukua na kumpeleka Hospitali lakini akawa amefariki, mwili wa Marehemu umeagwa na kusafirishwa kwenda Ukerewe kwa mazishi.
Winfrida alifariki wakati anapelekwa Hospitali baada ya kuwa amevuja damu nyingi na Julius baada ya kufanya tukio hilo alijaribu kujichoma kisu tumboni lakini Watu walimuwahi na kumchukua kisha kumpeleka Hospitalini ambako anaendelea na matibabu chini ya ulinzi.
Inaelezwa kuwa Winfrida alikuwa amepanga nje ya Chuo na alikuwa na mahusiano na Kijana huyo kwa muda fulani lakini walikuwa wameachana na Kijana alikuwa anamsumbua Msichama hivyo alimuahidi kuwa akimaliza mtihani atamjulisha.
Juzi Msichana alikuwa amemaliza mtihani wake wa mwisho na kwa mujibu wa Mama mwenye nyumba walikutana wakaongea sana pale ndani na ilipofika saa nne na nusu walitoka nje akawa anamsindikiza ndio lilipotokea tukio la kuchomwa kisu na akawa anaomba msaada na walimchukua na kumpeleka Hospitali lakini akawa amefariki, mwili wa Marehemu umeagwa na kusafirishwa kwenda Ukerewe kwa mazishi.


.