Makapuku Forum

Makapuku Forum

Malkia nae alikuwa anapenda 'Ubuyu' kama wewe tu.
Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza John Major (1990-1997) amesema kwamba sio mara zote alipokuwa anakutana na Malkia Elizabeth walikuwa wanazungumzia mambo muhimu ya nchi bali wakati mwingine walikuwa wanakutana kufurahi na kupiga umbeya tu.

Major amesema ilikuwa inashangaza sana jinsi Malkia alivyokuwa anajua mambo ya watu wengi sana karibu kila kona ya Uingereza... lakini Mstaafu huyo hajasema kama Malkia aliwahi kusutwa au la..!hebu na wewe mtag hapa shoga yako mnayekutanaga kwa ajili ya kupiga umbeya tu na hakuna hata cha maana mnachoongeaga
Screenshot_20220909-162346_OGInsta%2B.jpg
 
Huyu ndie Camilla, kutoka mchepuko mpaka Malkia.
Maisha ya ujana ya Chalesi ambaye sasa ni Mfalme wa Uingereza hayakuwa tofauti na maisha ya wanaume wengine.

Licha ya kwamba alikuwa kwenye ndoa lakini alikuwa na mchepuko wake waliyekuwa wamegandana kama ruba. Pengine kabla ya ndoa zao za mwanzo Camilla na Charles wangeowana, hata hivyo wazazi wa mwanaume waliona kwamba Camilla hakuwa mke wa kuolewa na Mfalme mtarajiwa.

Camilla aliolewa na mume wake wa kwanza mwaka 1973. Katika ndoa yake alibahatika kupata watoto wawili. Inadaiwa kwamba wakati Camilla akiwa kwenye ndoa yake bado alikuwa na mahusiano ya nje na Prince Charles.

Migogoro iliibuka kwenye ndoa yao ukizingatia kwamba wote wawili walikuwa kwenye ndoa nyingine za Kikristu, Camilla akiwa na ndoa ya Kikatoliki na Charles ndoa ya Anglikana. Mwaka 1994, Camilla alitalakiana rasmi na mume wake wa kwanza, Andrew, baada ya kuishi kwenye ndoa kwa muda wa miaka 21.

Hata hivyo waliiambia mahakama kwamba walikuwa wametengena kwa muda mrefu. Camilla aliolewa na Charles mwaka 2005. Kwa sasa Camilla ni Malkia. Camilla ana umri wa miaka 75 na Mfalme Charles ana umri wa miaka 73.

Katika hii ndoa yao bado Camilla hajabahatika kupata watoto na Mfalme Charles. Hata hivyo Mfalme Charles ni baba wa ubatizo wa mtoto wa kwanza wa Camilla.
Screenshot_20220909-162513_OGInsta%2B.jpg
 
Baada ya kifo cha Malkia wa Uingereza, Elizabeth II na nafasi yake kurithiwa na mwanawe wa kwanza Mfalme Charles, hali hiyo inabadilisha taswira ya wimbo wa taifa hilo.

Malkia Elizabeth II amefariki jana Septemba 8, 2022 akiwa anapatiwa matibabu kwenye kasri la Balmoral nchini Scotland.

Wakati wa utawala wa kiongozi huyo wa kimila wa Uingereza, wimbo wa taifa hilo uliimbwa 'Mungu mlinde Malkia wetu' maneno ambayo hubadilishwa kulingana na jinsi ya mtawala anayerithi madaraka.
Kwa kuwa mrithi wa kiti hicho kwa sasa ni Mfalme Charles, wimbo wa taifa hilo utabadilika baadhi ya maneno kutoka 'Mungu mlinde malkia' hadi 'Mungu mlinde Mfalme'.
Screenshot_20220909-162823_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom