Makapuku Forum

Makapuku Forum

Watu watano wamefariki dunia na wengine 54 wamejeruhiwa baada ya basi kugongana na lori katika eneo la Ibadakuli katika eneo la Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga, Leonard Nyandahu amesema ajali hiyo imetokea usiku wa kuamkia leo Jumamosi Septemba 3, 2022 ikihusisha basi kampuni ya Super Najimunisa likitokea Dar es salaam kuelekea jijini Mwanza na lori likitokea Mwanza kwenda Dar es salaam likiwa na mzigo wa dagaa.

Nyandahu amesema chanzo cha ajali hii ni uzembe wa dereva wa basi kwa kutozingatia vibao vya usalama barabarani na kuendesha mwendokasi.

Screenshot_20220903-194526_OGInsta%2B.jpg
 
Kituo cha Mafuta cha Bageni kimevamiwa na Majambazi saa saba usiku wa kuamkia leo katika Kijiji cha Ikina Kata ya Bukoli Mkoani Geita na kumjeruhi kichwani Mlinzi Obedi Stephano (22) akiwa katika majukumu ya kikazi kisha Majambazi hapo wakaiba zaidi ya Tsh. Milioni 8.

Mkuu wa Wilaya ya Geita, Wilson Shimo amefika katika eneo hilo huku akiwatahadharisha Wafanyabiashara kutohifadhi fedha ndani ya nyumba na badala yake wapeleke Benki, Kituo hicho kina Walinzi wawili ambapo mmoja walifanikiwa kumdhibiti na kumfunga na kamba.

Mmiliki wa kituo hicho cha mafuta Mayengo Bageni amesema walikuwa wamehifadhi kiasi cha zaidi ya Tsh. Milioni 8 katika sanduku la chuma la kuhifadhia fedha ambalo limevunjwa na pesa kuchukuliwa.

Mlinzi Obedi Stephano (22) amepatiwa matibabu katika Kituo cha Afya cha Geita na kuruhusiwa “Nilivamiwa majira ya saa 7 usiku na Watu 8 ambapo walinipiga na panga kichwani nikadondoka chini halafu wakaniburuza ndio maana unaona mdomo na shavu vimebabuka”
Screenshot_20220903-195128_OGInsta%2B.jpg
Screenshot_20220903-195148_OGInsta%2B.jpg
Screenshot_20220903-195209_OGInsta%2B.jpg
Screenshot_20220903-195229_OGInsta%2B.jpg
Screenshot_20220903-195246_OGInsta%2B.jpg
 
Serikali imekanusha taarifa za uzushi zilizotolewa kuhusu tarehe ya Shule kufunguliwa iliyotolewa na baadhi ya Watu wasiokuwa na nia njema na sekta ya elimu nchini.

Taarifa hiyo imeenea katika mitandao mbalimbali ya kijamii ikieleza kuwa Shule zitafunguliwa tarehe 21 Septemba 2022 jambo ambalo sio sahihi na hakuna muongozo wala maelekezo hayo.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amekanusha uvumi huo leo tarehe 3 Septemba 2022 wakati akizungumza na Wajumbe wa Bodi ya Skuli ya Ole Sekondari iliyopo katika Mkoa wa Kusini Pemba wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya siku moja Mjini Pemba.

Waziri Mkenda ameeleza kuwa ratiba ya kufunguliwa Shule ipo vilevile kwa mujibu wa waraka wa elimu Na 2 wa mwaka 2022 kuhusu mihula ya masomo uliotolewa na Kamishna wa elimu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt Lyabwene Mtahabwa.

“Naomba mpuuze jambo hili kwanza aliyesambaza anatumia nembo ya Kampuni moja ambayo Kampuni hiyo haijui na haihusiki na tangazo hilo, kwahiyo hakuna maelekezo yoyote zaidi ya yale yaliyotolewa na Kamishna wa Elimu”
Screenshot_20220903-202343_OGInsta%2B.jpg
 
FT: Uganda 3-0 Tanzania (Waiswa 16’P Basangwa 54’ Mato 76’) (agg 4-0) Tanzania imeondolewa katika mbio za kuwania kufuzu CHAN
Screenshot_20220903-202447_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa zamani wa Sri Lanka aliyeondolewa madarakani Gotabaya Rajapaksa, huenda akakamatwa baada ya kurejea nyumbani Sri Lanka hapo jana.

Rajapaksa aliikimbia nchi hiyo chini ya ulinzi wa Jeshi mnamo mwezi Julai mwaka huu, baada ya umati wa Wananchi kuvamia makaazi yake rasmi kufuatia miezi kadhaa ya maandamano dhidi ya Serikali yake.

Mwanasiasa huyo alitangaza kujiuzulu akiwa nchini Singapore na kutumia wiki kadhaa chini ya kizuizi cha nyumbani katika hoteli moja mjini Bangkok, akisubiri kuruhusiwa kurudi nyumbani.

Viongozi walioongoza maandamano, wamesema Rajapaksa ambaye amepoteza kinga ya Urais baada ya kuondoka madarakani, anapaswa kufikishwa Mahakamani, Serikali yake ilishutumiwa kwa usimamizi mbovu wakati uchumi wa Sri Lanka ukizidi kudorora.

Mgogoro huo ulishuhudia uhaba mkubwa wa chakula, kukatika kwa umeme kwa muda mrefu na foleni ndefu katika vituo vya mafuta.
Screenshot_20220903-202641_OGInsta%2B.jpg
 
Mwili wa Amina Iddy (34) Mkazi wa Lukirini Mkoani Geita ambaye amefariki dunia kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali sehemu za tumboni, ubavuni na mkononi na Mume wake aitwaye Mashaka Jeremia umeagwa leo Geita na unatarajiwa kusafirishwa kwa ajili ya kwenda kuzikwa Chamwino Mkoani Dodoma.

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita ACP. Ally Kitumbu, baada ya Amina kuchomwa na kitu chenye ncha kali alikimbizwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita lakini alifariki dunia wakati anapatiwa matibabu.

Kamanda Kitumbu amesema Mtoto wao Debora Mashaka mwanafunzi wa kidato cha kwanza ambaye ni Mtoto wa marehemu alikuwa akishuhudia tukio hilo na kueleza kuwa Baba yake baada ya kutenda hilo kosa alikimbilia kusikojulikana

Msemaji wa Familia, Bakari Hamza amesema wamesikitishwa na kitendo cha kinyama kilichofanywa huku akiliomba Jeshi la polisi Mkoani humo kufuatilia ili sheria ifuate mkondo wake ambapo ameiomba Serikali kushirikiana na Familia kusafirisha mwili wa Amina.
Screenshot_20220903-202747_OGInsta%2B.jpg
Screenshot_20220903-202803_OGInsta%2B.jpg
 
Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Albert Chalamila amezitaja sababu zinazopelekea Mkoa huo kutoendelea kwa haraka ambapo amesema miongoni mwa sababu hizo ni kila Mtu kujifanya ni Mwanasheria, ubishi na kuongea kiingereza kingi kisicholeta maendeleo.

Chalamila amewashauri Wahaya na Watu wengine wa Kagera kutumia elimu zao kuleta maendeleo Mkoani humo badala ya kuendekeza kiingereza kingi kisicho na faida.

"Kila mmoja Kagera huwa ni Mwanasheria tunapenda sana kubishana, mambo mengi wanapenda kiingereza kingikingi, sasa nawaomba niwaambie sitaki kiingereza wala makaratasi nataka jinsi gani utakavyoitumia elimu yako kuibadilisha kuwa maendeleo kwa Wana kagera”

Chalamila amesema hayo Mjini Bukoba wakati akimkaribisha Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Abdulrahman Kinana wakati akizungumza na Wananchi na Wanachama wa CCM Kagera.
Screenshot_20220903-205319_OGInsta%2B.jpg
 
Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Albert Chalamila amezitaja sababu zinazopelekea Mkoa huo kutoendelea kwa haraka ambapo amesema miongoni mwa sababu hizo ni Wafanyabiashara kuchelewa kufungua biashara zao mapema.

Chalamila amesema ili kuendana na kasi ya ushindani wa kimaendeleo Wakazi wa Mkoa huo wanapaswa kufungua biashara mapema “Ni rukhsa hata Jumamosi kufungua soko hata saa 11 alfajiri mkitaka kufungua fungueni lakini zingatieni usafi”

“Mkoa huu hauendelei kwa haraka sababu zipo nyingi ila sababu kubwa ni Ndugu zangu Wahaya na wengine mnaoishi hapa, bado hatujatambua kwamba tupo kwenye ushindani, mpaka saa tatu maduka hayajafunguliwa, ina maana mnalala sana au kitu gani?, badilikeni fungueni maduka mapema”

Chalamila amesema hayo Mjini Bukoba wakati akimkaribisha Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Abdulrahman Kinana wakati akizungumza na Wananchi na Wanachama wa CCM Kagera.
Screenshot_20220903-205432_OGInsta%2B.jpg
 
Watu watano wamefariki dunia na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa baada ya Basi la Kampuni ya Super Najimunisa lililokuwa likitokea Dar es salaam kuelekea Mkoani Mwanza kugonganga uso kwa uso na Fuso katika eneo la Ibadakuli, Manispaa ya Shinyanga usiku wa kuamkia leo.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga Leonard Nyandahu amesema chanzo cha ajali ni uzembe wa Dereva wa Basi kutofuata sheria za barabarani na kuendesha kwa mwendokasi

“Ajali imehusisha Basi la Kampuni ya Super Najimunisa lente namba za usajili T.413 DAY likitokea Dar es salaam kuelekea Mwanza, na Fuso lenye namba za usajili T.123 DJH likitokea Mwanza kwenda Dar es salaam likiwa limebeba mzigo wa dagaa”

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa mkoa wa Shinyanga Dk. Luzila John amethibitisha vifo vya Watu watano pamoja na majeruhi zaidi ya 50 ambao wanaendelea na matibabu anbapo amesema Watu hao ambao wamepoteza maisha bado hawajatambuliwa majina yao, na wamehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti Hospitalini hapo.
Screenshot_20220903-205534_OGInsta%2B.jpg
 
Daniel Pascal (23) Mkazi wa Kijiji cha Guse kata ya Dabil Mkoani Manyara amehukumiwa kifungo cha maisha kwenda jela kwa kukutwa na kosa la kumbaka Mtoto wa miaka mitano, Mwanafunzi wa darasa la kwanza.

Mtuhumiwa anadaiwa kutenda kosa hilo July 03,2022 katika Kijiji cha Mandi ambapo alimkuta Mtoto huyo akielekea dukani na Kaka yake (7), Mwanafunzi wa darasa la pili wakiwa na Tsh. 500 ndipo akawarubuni kwa kuwapa Tsh. 1000 na yeye kuchukua hiyo 500 kisha kuondoka na Mtoto huyo katika shamba la mahindi kumbaka na baada ya Mtoto kupiga kelele aliokolewa na Wasamaria wema na Mtuhumiwa kufikishwa Ofisi ya Kijiji na baadaye Mahakamani.

Mwendesha mashtaka wa Serikali Grace Mgaya amesema baada ya vipimo vya Daktari imeonesha Mtoto huyo amebakwa hivyo akaomba Mahakama hiyo kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hizo.

Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu wa Mahakama hiyo ya Wilaya ya Babati Victor Kimaro ambapo Mshtakiwa anayo haki ya kukata rufaa ndani ya siku 30 kuanzia sasa, huku Mshtakiwa akiiomba Mahakama impunguzie adhabu kwa kuwa ana ugonjwa wa moyo.
Screenshot_20220903-205702_OGInsta%2B.jpg
 
Mahakama ya Wilaya ya Iringa imemuhukumu kifungo cha miaka 30 Petro Mgimwa aliyekuwa akiishi katika Kijiji cha Ifunda kwa kosa la kubaka Mtoto mwenye umri wa miaka 9 aliyekuwa akisoma darasa la nne.

Petro (41) alikuwa akifanya kazi ya ulinzi na ukulima ambapo alimrubuni Mtoto huyo kwa kumpa maembe na baada ya kumaliza kumbaka akampa Tsh. Elfu 1.

Kwa Mujibu wa Mahakama tukio hilo lilitokea March 06,2022 ambapo Binti alikwenda kuchuma maembe katika nyumba ambayo Petro alikuwa akilinda ndipo Petro akamrubuni na kumuingiza ndani ya chumba Kisha kumbaka.

Baada ya kumaliza Binti alipokwenda nyumbani Dada yake alimgundua kwa sababu alikuwa anatembea tofauti na alivyomzoea ndipo akamhoji na akaambiwa kuwa alikuwa amebakwa.

Kesi hiyo iliyosimamiwa na Mwendesha mashtaka wa Serikali Penzia Nochombe ilikuwa na Mashahidi 6 akiwemo Daktari aliyemfanyia uchunguzi Binti huyo na kubaini kuwa alikuwa amebakwa, akisoma hukumu hiyo Hakimu Mkazi Mkuu Zabibu Mpangule amesema Mtuhumiwa amekutwa na hatia kutokana na mashahidi wote kumthibitisha kuwa Petro Mgimwa alimbaka Mtoto huyo na hivyo amehukumiwa miaka 30 Jela.
Screenshot_20220903-205811_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom