Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mtoto Jovin Simon (10) Mkazi wa Mtaa wa Elimu Wilaya ya Geita amefariki dunia baada ya kushambuliwa kwa kupigwa na teke tumboni na Haruna Amini (16) Mkazi wa Mtaa wa Elimu.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita, Ally Kitumbu amesema Jovin alifariki dunia wakati akiendelea na matibabu katika Hospitali ya Mkoa wa Geita huku akisema chanzo cha tukio hilo ni ugomvi kati yao wawili .

"Huyu Mwanafunzi alikimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita na alifariki dunia wakati akiendelea na matibabu na kiini cha tukio ni ugomvi mwili umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti kwa ajili ya uchunguzi wa Daktari”

Aidha Kaimu Kamanda amewaomba Wazazi kuhakikisha wanawakanya Watoto wao kucheza michezo isiyokuwa na staha wawapo majumbani na kusema mwili wa Mtoto huyo umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Rufaa ya Geita.
Screenshot_20220831-210430_OGInsta%2B.jpg
 
Mtoto Simon Seleman anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 11-13, Mwanafunzi wa darasa la nne Shule ya Msingi Ligundo amefariki dunia baada ya kugongwa na gari katika Kata ya Lulembela barabara ya Ushirombo Wilayani Geita.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita, Ally Kitumbu amesema Dereva wa gari lenye namba T.152 DMB. Khamis Daniel (33) Mwalimu Mkazi wa Kijiji cha Lulembela amemgonga Mwanafunzi huyo ambaye alikuwa akiendesha baiskeli na kumsababishia majeraha sehemu za mwili hali iliyopelekea kufariki dunia.

Kamanda Kitumbu amesema chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi wa Dereva wa gari huku akisema mara baada ya kijana huyo kugongwa alikimbizwa katika Hospitali ya Mkoa wa Geita kwa matibabu lakini kwa bahati mbaya amefariki dunia akiwa anaendelea na matibabu.
Screenshot_20220831-210624_OGInsta%2B.jpg
 
Mwanamke mmoja wa Melbourne nchini Australia aitwae Thevamanogari Manivel ametakiwa kulipa kiasi cha dola za kimarekani zaidi ya milioni sita (Tsh. zaidi ya bilioni 16) kwa kampuni moja iitwayo CRYPTO ya nchini Singapore baada ya kampuni hiyo kukosea muamala na kumuwekea fedha hizo kwenye account yake ya benki.

Baada ya kuziona pesa hizo kwenye account yake Manivel alivumilia kwa muda wa miezi saba bila kuzitumia ambapo baada ya kuona kipindi hicho kimepita bila Mtu yoyote kujitokeza kuzidai alimua kuzitoa na kuzinunulia nyumba ya ndoto zake huku nyingine akizigawanya kwenda kwenye akaunti za ndugu zake wapatao sita.

Manivel alitumia dola laki 9 za kimarekani ambazo ni zaidi ya Tsh. bilioni 2 kununulia nyumba hiyo ya ndoto zake ikiwa na vyumba vitano ambapo baada ya hiyo miezi saba Kampuni hiyo iligundua makosa hayo na kuanza taratibu za kisheria mwezi February na kumfungulia Manivel mashitaka ya kutaka alipe pesa zote pamoja na riba.

Jaji wa Mahakama Kuu ya Victoria nchini Australia James Elliott, licha ya kuamuru kulipwa kwa fedha hizo alishangazwa na Walalamikaji kwa kutotambua makosa hayo ya malipo kwa muda wa miezi saba ambapo hata hivyo aliagiza Manivel kulipa fedha zote ikijumuisha asilimia 10 ya riba na ada za kisheria.

Akili ya auntie yangu Espy Atoto View attachment 2341243
Sasa wakosee wao, mwingine ashtakiwe!! Huu ni uonevuuu 🤣🤣🤣🤣
 
Halmashauri ya Wilaya ya Makete mkoani Njombe imepiga marufuku Watu kuchinja Nguruwe na kula nyama yake (kitimoto) kwa muda usiojulikana kutokana na taarifa za uwepo wa ugonjwa wa homa ya nguruwe.

Afisa Mifugo na Uvuvi wa Wilaya hiyo Aldo Mwapinga ametoa taarifa ya katazo hili kutokana na vifo vya nguruwe 21 Wilayani humo na amenukuliwa akisema "Kata ya Tandala kumeripotiwa dalili za ugonjwa wa homa ya Nguruwe kwahiyo tunaendelea na jitihada za kuhakikisha tunashirikiana na Watendaji kuanzia ngazi ya Kata hadi Vitongoji kutoa taarifa juu ya hali inavyoendelea"

Amesema Serikali imepiga marufuku hiyo hususani katika kata ya Tandala huku pia akizuia utoaji wa Nguruwe kutoka kwenye zizi moja kwenda jingine kwa ajili ya kupandisha kwa jike, vilevile amewataka Watu kuacha kufukua Nguruwe waliofukiwa baada ya kufa (mizoga) na kuwachinja kisha kwenda kuuza nyama hizo vilabuni nyakati za usiku, hii ni baada ya taarifa za namna hiyo kuripotiwa hivi karibuni.

waione auntie yangu Makiwendo na huyu mzee mtu chake hawa hawatakubali watasema bora wafe tu View attachment 2341152
Huyu kiumbe wanamkosea sana aiseee....

Wampakazie watakavyoweza... ila sikomi...

Kuna mtu aliniambie mafuta yake ndiyo kiboko sasa.. kupikia mboga za majani na kukaangia chipsi Auntieunaambiwa utajilambaaaa...
 
Na uroho wangu wotee hii nyama imenishinda haipiti hata
Dooh pole sana

Lakini sikushangai mwaya maana hata mimi pamoja na watu wengi kupenda nyama ya mbuzi ila mie ile nyama imenishinda kabisaaa sijawahi kuipenda yani

Mimi kwenye mdudu, ng'ombe, kuku na samaki (wenye magamba tu lakini) yani hapo ndio umenifikisha
 
Dooh pole sana

Lakini sikushangai mwaya maana hata mimi pamoja na watu wengi kupenda nyama ya mbuzi ila mie ile nyama imenishinda kabisaaa sijawahi kuipenda yani

Mimi kwenye mdudu, ng'ombe, kuku na samaki (wenye magamba tu lakini) yani hapo ndio umenifikisha
Ndio mimi kwa kitimoto yaani nitakufa na njaa yangu
 
Kwanini kila siku Ufaransa? Baada ya sakata zito la Mathieu Valbuena na Karim Benzema, juu ya mkanda wa ngono ambapo inasemekana Benzema alihusika kumtapeli Mathieu, ikaigawa timu ya taifa ya Ufaransa.

Sasa ni zamu ya Paul Pogba na Kylian Mbappe, baada ya Kaka yake Pogba kusema Mdogo wake anatumia Mwalimu wa diin ya Kiislam kumroga Kylian Mbappe.

Didier Deschamps ana miezi miwili tu kuelekea Qatar na tayari mezani ana jambo zito kama Kocha.
Screenshot_20220901-093817_OGInsta%2B.jpg
 
Makocha waliopoteza ajira zao baada ya kufungwa na Jurgen Klopp wa Liverpool.

Guidolin (Swansea)
Bilic (West Ham)
Jokanovic (Fulham)
Mourinho (United)
Silva (Everton)
Parker (Bournemouth)

Chelsea mnasemaje
Screenshot_20220901-093919_OGInsta%2B.jpg
 
Shaffih Dauda

Yanga wapo zao Avic Town, wanapambana kujiweka fit kuelekea michuano ya ndani na ya kimataifa, wanaamini Avic ni sahihi kwao.

Ni hapo hapo Avic paliwapa Premier League, FA Cup na Ngao mbili, wameendelea kupaamini wala hakuna tatizo kwakuwa ni chaguo lao na pendekezo lao.

Binafsi naamini Yanga kwasasa wanalihitaji zaidi taji la Premier, taji la FA na Ngao kwakuwa wameyakosa kwa muda mrefu sana, wanapaswa kuendelea kuyabeba.

Msimu huu bado sitowadai chochote Yanga kimataifa, ila msimu ujao au miwili nawaona wanapaswa kupambania huko.
Screenshot_20220901-094019_OGInsta%2B.jpg
 
Inasemekana Paul Pogba, Cristiano Ronaldo na Raphael Varane walimfuata aliyekuwa Kocha wa Manchester United wakati huo Ralph Rangnick na kumwambia wazi kuwa Harry Maguire ni tatizo na hapaswi kucheza.

Rangnick nae aliwaambia kwakuwa wamemfuata ofisini ni vyema waseme mbele ya Harry Maguire kuwa yeye ni tatizo.

Wajerumani

[ Chanzo: Daily Mail ]
Screenshot_20220901-094130_OGInsta%2B.jpg
 
Msimu wa 2016/17 Man United walitoa kibunda cha maana kuipata saini ya Paul Pogba - Pound Milioni 115 na Ushee!

Kwangu mimi naona Pogba amecheza kawaida sana kipindi akiwa Man United ukilinganisha na Dau alilonunuliwa.

2019/20, Man United ikaona isiwe tabu, wakaingia tena sokoni wakachukua beki la dunia, Harry Maguire kwa gharama ya pound milioni 95, Lakini perfomance ya maguire wote tunaielewa, hapa naomba nisiseme sana.

2021/22, Man U wakapanda ndege mpaka Borrusia Dortmund, kama kawaida yao wakaweka mzigo mezani, na kumbeba Sancho mzima mzma kama alivyo kwa Pound milioni 93.50, perfomance yake mpaka sasa wote tunaielewa, Kama umeme wa Tanesco.

Soon, Man United watamtangaza Kinda Antony, huyu nae kwa taarifa zilizopo Man united wametoa karibia Pound milioni 104.5

Lakini, Ukiangalia vizuri hizi sajili za gharama za Man United mwisho wa siku haziwi na perfomance nzuri inayotegemewa na Mashabiki.

Ni kama vile Man United wanazitupa pesa zao bure, Inasikitisha sana.

Kumbuka hapo sijaongelea Usajili wa Angel Di Maria, Casemiro pamoja na Anthony Martial.
Screenshot_20220901-094243_OGInsta%2B.jpg
 
Atletico Madrid wanapaswa kuilipa Barcelona Euro Million 40 endapo Antoine Griezman atacheza kwa zaidi ya dakika 45 kwenye 50% ya mechi zake klabuni hapo.

Ikumbukwe Griezman yupo kwa mkopo Atletico, tayari pichani ndio takwimu zake mpaka sasa.
Screenshot_20220901-094339_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom