Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mwanamke mmoja wa Melbourne nchini Australia aitwae Thevamanogari Manivel ametakiwa kulipa kiasi cha dola za kimarekani zaidi ya milioni sita (Tsh. zaidi ya bilioni 16) kwa kampuni moja iitwayo CRYPTO ya nchini Singapore baada ya kampuni hiyo kukosea muamala na kumuwekea fedha hizo kwenye account yake ya benki.

Baada ya kuziona pesa hizo kwenye account yake Manivel alivumilia kwa muda wa miezi saba bila kuzitumia ambapo baada ya kuona kipindi hicho kimepita bila Mtu yoyote kujitokeza kuzidai alimua kuzitoa na kuzinunulia nyumba ya ndoto zake huku nyingine akizigawanya kwenda kwenye akaunti za ndugu zake wapatao sita.

Manivel alitumia dola laki 9 za kimarekani ambazo ni zaidi ya Tsh. bilioni 2 kununulia nyumba hiyo ya ndoto zake ikiwa na vyumba vitano ambapo baada ya hiyo miezi saba Kampuni hiyo iligundua makosa hayo na kuanza taratibu za kisheria mwezi February na kumfungulia Manivel mashitaka ya kutaka alipe pesa zote pamoja na riba.

Jaji wa Mahakama Kuu ya Victoria nchini Australia James Elliott, licha ya kuamuru kulipwa kwa fedha hizo alishangazwa na Walalamikaji kwa kutotambua makosa hayo ya malipo kwa muda wa miezi saba ambapo hata hivyo aliagiza Manivel kulipa fedha zote ikijumuisha asilimia 10 ya riba na ada za kisheria.

Akili ya auntie yangu Espy Atoto
Screenshot_20220831-205028_OGInsta%2B.jpg
 
Mwanamke mmoja wa Melbourne nchini Australia aitwae Thevamanogari Manivel ametakiwa kulipa kiasi cha dola za kimarekani zaidi ya milioni sita (Tsh. zaidi ya bilioni 16) kwa kampuni moja iitwayo CRYPTO ya nchini Singapore baada ya kampuni hiyo kukosea muamala na kumuwekea fedha hizo kwenye account yake ya benki.

Baada ya kuziona pesa hizo kwenye account yake Manivel alivumilia kwa muda wa miezi saba bila kuzitumia ambapo baada ya kuona kipindi hicho kimepita bila Mtu yoyote kujitokeza kuzidai alimua kuzitoa na kuzinunulia nyumba ya ndoto zake huku nyingine akizigawanya kwenda kwenye akaunti za ndugu zake wapatao sita.

Manivel alitumia dola laki 9 za kimarekani ambazo ni zaidi ya Tsh. bilioni 2 kununulia nyumba hiyo ya ndoto zake ikiwa na vyumba vitano ambapo baada ya hiyo miezi saba Kampuni hiyo iligundua makosa hayo na kuanza taratibu za kisheria mwezi February na kumfungulia Manivel mashitaka ya kutaka alipe pesa zote pamoja na riba.

Jaji wa Mahakama Kuu ya Victoria nchini Australia James Elliott, licha ya kuamuru kulipwa kwa fedha hizo alishangazwa na Walalamikaji kwa kutotambua makosa hayo ya malipo kwa muda wa miezi saba ambapo hata hivyo aliagiza Manivel kulipa fedha zote ikijumuisha asilimia 10 ya riba na ada za kisheria.

Akili ya auntie yangu Espy Atoto View attachment 2341243
wakosee na huku kwetu
 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi ameshiriki maziko ya Kaka yake Hassan Ali Hassan Mwinyi yaliyofanyika Mangapwani, Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Maziko hayo yalihudhuriwa pia na Alhaji Mzee Ali Hassan Mwinyi, ambaye ni Baba Mzazi wa Marehemu.

Wengine waliohudhuria ni Viongozi mbalimbali wa Dini, Siasa, Serikali na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama.
Screenshot_20220831-205807_OGInsta%2B.jpg
 
Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dr. Albina Chuwa amesema hadi leo asubuhi tarehe 31 Agosti 2022 kiwango cha Watu waliohesabiwa nchi nzima kimefikia asilimia 99.93 na wamebakiza kiwango cha asilimia 0.07 ya kaya zote zote nchi nzima.

Dr. ameongeza kuwa asilimia 0.07 iliyobaki wataendelea kuhesabu hadi tarehe 5 September 2022 ambapo simu zilizotolewa zitatumika kuwafikia ambao hawajahesabiwa kwakuwa utaratibu maalumu ulishaandaliwa wa namna ya kuzifikia kaya hizo.
Screenshot_20220831-205908_OGInsta%2B.jpg
 
Ikiwa leo ni August 31 2022, Benki ya NMB @nmbtanzania imewakumbusha Watanzania kuwa tarehe rasmi ya ile siku moja ambayo hutokea mara moja kwa mwaka ni tarehe 24 kwenye Viwanja vya Leaders, Kinondoni Dar es salaam ambako NMB Marathon 2022 itafanyika ikiongozwa na maneno matatu mazito ambayo ni "mwendo wa upendo".

Kwanini mwendo wa upendo ? ni kwa sababu pesa zote zitakazopatikana zitakwenda kurejesha matabasamu kwa Wanawake mbalimbali wa Tanzania ambao wamekua kwenye mateso kutokana na ugonjwa wa fistula lakini sasa watakwenda kutibiwa kwenye Hospitali ya CCBRT Jijini Dar es salaam ambako pesa zote za marathon hii zitapelekwa.

Benki ya NMB imewaomba Watanzania kuungana nayo ili kufanikisha hili lengo la mwendo wa upendo na kurejesha tabasamu na kusisitiza pia kwamba siku za kujiandikisha zimebaki 23 pekee na hata kama Mtu hatoweza kushiriki siku hiyo lakini ameguswa na hiki kilichoanzishwa na benki hii basi anaweza pia kujiandikia kwenye website https://marathon.nmbbank.co.tz
Screenshot_20220831-210105_OGInsta%2B.jpg
 
Polisi wa India wameanza uchunguzi wa kifo cha Msichana aitwae Ankita aliyechomwa moto na Mwanaume ambaye alimkatalia ombi lake la ndoa ambapo Polisi wamesema Mwanaume huyo alimmwagia mafuta ya taa kupitia dirishani akiwa amelala na kumchoma moto.

Imeelezwa kwamba Ankita alifariki akiwa hospitalini siku tano baadaye kutokana na majeraha makubwa ya moto aliyokuwa nayo huku Msemaji wa Polisi wa eneo la Jharkhand kulikotokea tukio hili akisema Mshtakiwa na Mshtakiwa mwenzake wamekamatwa.

Vishva Hindu Parishad au Baraza la Wahindu Ulimwenguni lilisema Wahindu walio wengi wataingia barabarani kuandamana ikiwa hatua zinazofaa hazitochukuliwa dhidi ya kifo cha Ankita.

"Baada ya ukatili aliofanyiwa Ankita, kifo chake kimefanya kila Mhindi kuinamisha kichwa chini kwa aibu, kuna haja kubwa ya kuweka mazingira salama kwa Wanawake nchini" ameandika kwenye twitter Rahul Gandhi, Kiongozi wa Chama Kikuu cha Upinzani cha Congress.
Screenshot_20220831-210200_OGInsta%2B.jpg
 
Gazeti la Financial Times limeripoti kuwa Kampuni ya Yankee Global Enterprises ya Marekani ambayo ndio kampuni mama ya timu ya MLB na kampuni ya uwekezaji ya ‘Main Street Advisors’ ya Los Angeles, Marekani ambayo ina Wawekezaji mbalimbali wakiwemo LeBron James na Drake, wanakaribia kufikia makubaliano ya kuinunua Club ya AC MILAN kwa kiasi cha zaidi ya dola za kimarekani bilioni 1.2.

Mkataba huo utawafanya LeBron na Drake kuwa Wawekezaji waliowekeza fedha jijini Milan nchini Italia lakini kupitia kampuni ya ‘Main Street Advisors’ hivyo hisa zao hazitokuwa za moja kwa moja katika klabu hiyo.

Hii sio mara ya kwanza kwa Staa wa mpira wa kikapu LeBron James kuwekeza katika biashara ya michezo ambayo imezidi kumtajirisha kwani June 2022 alikua Mchezaji wa kwanza wa ligi ya NBA aliye hai kufikia hadhi ya kuwa Bilionea akiwa tayari anamiliki hisa za Boston Red Sox, Pittsburgh Penguins na Klabu ya Soka ya Liverpool.
Screenshot_20220831-210321_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom