Makapuku Forum

Makapuku Forum

Baada ya michezo 236 na kukimbiza LA LIGA kwa kucheza mechi zote kwa miaka sita mfululizo, juzi Inaki Williams amepata majeraha ambayo yanaweza kumfanya akae nje kwa muda.

Hatimae rekodi yake ya kutokosa mchezo wowote wa ligi hiyo imefika tamati.

Ikumbukwe Inaki alitembelea Ghana mwaka huu na amechagua kuvaa jezi ya taifa hilo kuelekea Qatar.
Screenshot_20220901-183545_OGInsta%2B.jpg
 
Shaffih Dauda

JARIBU KUTAZAMA MACHAGUO NDANI YA YANGA

Morrison - Mayele - Kisinda
Morrison - Mayele - Moloko
Farid Mussa - Mayele - Nkane - Ambundo

Kwa Mfano tu, Yanga ikaamka ikasema mechi ya leo tunataka tucheze sana mpira, pasi nyingi na kukimbia kidogo.

Yanga wataanza na winga mmoja, Farid Mussa, Winga mwingine Morrison, kati Fiston Mayele.

Kuna siku Yanga itaamka itasema, mechi ya leo tunataka tukimbizane, ni mwendo wa mipira mirefu kwa winga zake za pembeni.

Yanga wataanza na winga moja Tuisila Kisinda, Winga mwingine Moloko, kati ni Fiston Mayele.

Yanga wana machaguo kinachobaki ni kuchagua aanze yupi na nani atasubiri.

Na uzuri wa Yanga hii ya sasa, kila mchezaji yupo na utofauti kwa aina yake ya uchezaji.

Itakua ni mwendo wa ichukue hapa, iweke pale, niiikute kule.

Over to you Coach NABI!
Screenshot_20220901-183636_OGInsta%2B.jpg
 
“Wakati tumecheza na Barcelona 2016, wachezaji wenzangu wote walikuwa wanahitaji kubadilishana jezi na wachezaji wa Barca, mimi sikutaka kubadili na yoyote ila halftime Suarez alinifuata na kuomba tubadilishane”

- Jamie Vardy, mshambuliaji wa Leicester City.
Screenshot_20220901-183747_OGInsta%2B.jpg
 
Baada ya Jordan Henderson kupata majeraha usiku wa jana Liverpool wameulizia uwezekano wa kumpata Kiungo wa Juventus Arthur Melo kwa mkopo.

Inasemekana dili lipo kwenye hatua za mwisho na tayari Melo amepanda ndege kuelekea Liverpool ilo kukamilisha uhamisho huo ikizingatiwa kuwa Liverpool wana majeruhi wengi.
Screenshot_20220901-183833_OGInsta%2B.jpg
 
Mwamba Edison Cavani amesaini kwenye klabu ya Valencia inayoshiriki Laliga nchini Hispania.

Anatambulika kama El Matador ikiwa na maana ya Bullfighter, alipewa jina hilo na Mashabiki wa Napoli ya Italia kutokana na aina yake ya uchezaji.

Cavani amezaliwa jiji moja na Luis Suarez huko nchini kwao Uruguay, jiji linaitwa Salto na wamepishana siku 21 tu, Cavani yupo Hispania ambapo Suarez pia alipita.

Nyota huyo ndie mfungaji bora wa muda wote wa PSG akiwa na mabao zaidi ya 200 klabuni hapo.

Screenshot_20220901-184003_OGInsta%2B.jpg
 
OFFICIAL | Klabu ya Al Ahly imemfuta kazi Kocha Mkuu, Ricardo Soares baada ya miezi miwili tu tangu aajiriwe.

17 - Michezo
09 - Kushinda
05 - Sare
03 - Kupoteza

Al Ahly kazi kazi
Screenshot_20220901-184055_OGInsta%2B.jpg
 
| Pande mbili zipo kwenye mazungumzo ambapo upande wa Tyson Furry na Aleksander Usyk wapo katika hatua za mwisho juu ya pambano la wababe hao wawili.

Usyk alifanikiwa kutetea mikanda yake mitatu ya WBF, WBO na IBF dhidi ya Antony Joshua na sasa anautaka mkanda wa WBC ambapo unashikiliwa na Gypsy King.

Taarifa zinadai kuwa pambano hilo huenda likapelekwa tena Saudi Arabia ijapo Qatar, Falme za Kiarabu na Marekani wanalitaka pia.

Tarehe rasmi ya pambano bado haijawekwa wazi ila inasemekana huenda ni Februari,2023.
Screenshot_20220901-184143_OGInsta%2B.jpg
 
SINGIDA YAMTEMA MWENDWA
.
Klabu ya Singida Big Stars imeachana na aliyekuwa winga wake mshambuliaji, Harrison Mwendwa ikiwa ni mwezi mmoja tu tangu iingie naye mkataba wa mwaka mmoja.
.
Nyota huyo aliyesajiliwa kutoka Kabwe Warriors ya Zambia ili kuongeza nguvu eneo hilo ameachwa rasmi huku ikielezwa sababu kubwa ni majeraha.

……………
Screenshot_20220901-184632_OGInsta%2B.jpg
 
WEZI WAMVUNJA TAYA AUBAMEYANG
.
Supastaa straika, Pierre-Emerick Aubameyang ameripotiwa kuvunjika taya baada ya kushambuliwa na wezi wanne waliovamia nyumbani kwake wikiendi iliyopita. Staa huyo wa Barcelona alipigwa na kipade cha chuma kidevuni wakati akijaribu kupambana na wezi hao wasidhuru familia yake.
.
Na sasa ripoti zinafichua, Aubameyang, 33, aliumizwa taya kwenye tukio hilo. Jambo hilo litamfanya kuwa nje ya uwanja kwa wiki kadhaa na kuna uwezekano akafanyiwa upasuaji.
.
Upasuaji utamfanya mchezaji huyo kupona haraka kuliko akisubiri taya lipone lenyewe. Lakini, jambo hilo linaweza kutibua mpango wa Chelsea kunasa saini ya mshambuliaji huyo wa zamani wa Arsenal ili kurudi kukipiga Ligi Kuu England.
Screenshot_20220901-184739_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Fedha na Mipango Dr. Mwigulu Nchemba leo akiwa Dodoma amekutana na Waandishi wa Habari kutolea ufafanuzi ishu ambayo imekua gumzo nchini kuhusu masuala ya tozo kwenye miamala ya simu na benki ambapo amesema “Mimi nasema tu atakayetaka kutukana atukane tu, hata kama nitakosa Rafiki hata mmoja sawa tu lakini lazima niseme ukweli hata Mtu ana ng’ombe Elfu 12 mnataka Bwawa lake lijengwe kwa kodi ya Nesi au Mwalimu”
GagfatyaujH£#@&"*
Kwahiyo ni vyema huyo mwalimu na nesi akaongezewa kodi zaidi ili kumpata huyo mfugaji!! Akili ya wapi hii🙆🙆🙆
 
Waziri wa TAMISEMI, Innocent Bashungwa leo Dodoma amezielezea faida ya tozo kwenye sekta ya afya, elimu na miundombinu katika nukuu zifuatazo “Tozo zimeboresha miundombinu, kwa kipindi ambacho Rais Samia amekuwa madarakani katika Tarafa 570 tayari tumeshajenga vituo vya afya kwenye Tarafa 207 ndani ya mwaka mmoja wa Rais Samia madarakani”

“Pia kuna maeneo ambayo ni magumu kufikika tuliyabainisha na kwa kipindi ambacho Serikali ya awamu ya sita imekuwa madarakani kupitia tozo za miamala ya simu tumejenga vituo vya afya 234 kwa Bilioni 117 kwenye tarafa nilizozitaja na maeneo magumu kufikika na kila kituo cha afya kimetugharimu Tsh. Bilioni 500, tangu Uhuru na awamu zote za Serikali ambazo zimekuwepo kujenga vituo vya afya 234 sio jambo la kawaida, tunamshukuru sana Rais”

“Vituo vya afya hivi lazima tuvipeleke vifaa vya kisasa Serikali ilituwezesha TAMISEMI Bilioni 149.5 tumeshakamilisha hatua za manunuzi ili tupeleke vifaa tiba kwenye vituo vya afya “

“Watanzania hapa hoja sio nanufaika vipi na tozo ishu ipo kwenye maeneo ambayo Waziri Mwigulu ameyasema, tusingeweza kujenga vituo vya afya 234 ndani ya mwaka mmoja kama sio hizi tozo, tozo hizi zina faida”
View attachment 2342276
Yaani hata waelezee wamevua nguo, hawawezi kueleweka.
 
World Economic Forum imetoa orodha ya nchi 10 duniani zinazowalipa walimu mishahara mikubwa zaidi.

10. Austria : $62,882 (Sawa na TZS 146,640,824)
9. Ireland : $62,906 (Sawa na TZS 146,696,792)
8. Denmark: $64,259 (149,851,988)
7. Mexico: $64,491 (Sawana TZS 150,393,012)
6.United States: $65,248 (Sawa na TZS 152,158,336)
5.Australia: $65,714 (Sawa na TZS 153,245,048)
4: Canada: $71,664 (Sawa na TZS 167,120,448)
3. The Netherlands: $81,064 (Sawa na 189,041,248)
2. Germany: $91,041 (212,307,612)
1. Luxembourg: $109,204 (Sawa na 254,663,728).

Screenshot_20220901-190010_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amesema wananchi ndio walioshauri Serikali ipanue wigo wa tozo za miamala kwa kujumuisha miamala yote ya kielektroniki, ili wananchi wote wachangie maendeleo.

Ameeleza kuwa awali miamala iliyokuwa ikitozwa ni iliyokuwa ikifanyika kwa simu pekee.
Screenshot_20220901-190235_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom