Makapuku Forum

Makapuku Forum

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteuwa Mzee Ramadhan Nyamka kuwa Kamishna wa Magereza akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Suleiman Mzee ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Uteuzi wa Nyamka umeonyesha mwelekeo mpya katika teuzi za wakuu wa chombo hicho kinachorekebisha nidhamu za wahalifu, ambapo miaka ya karibuni waliteuliwa kutoka nje ya jeshi hilo.

Nyamka amepandishwa kutoka Kaimu Kamishna wa Magereza Huduma za Urekebu, kinyume na mtangulizi wake Brigedia Jenerali Suleiman Mzee aliyetokea Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ).

Screenshot_20220826-203001_OGInsta%2B.jpg
 
#TEKNOLOJIA: NIGER KUANZA KUTENGENEZA MVUA KUKABILIANA NA UKAME
-
#Niger imeanza kutumia Teknolojia ya kutengeneza Mvua inayolenga kupunguza athari za ukame ili kuongeza uzalishaji wa vyakula baada ya kukabiliwa na vipindi virefu vya ukame
-
Mkuu wa Taasisi ya Kitaifa ya Hali ya Hewa, Katiellou Gaptia Lawan, amesema Teknolojia hiyo inahusisha kutumia Ndege kunyunyiza Kemikali kwenye Mawingu
-
Unyunyiziaji huo unalenga maeneo yanayojishughulisha na Kilimo.
-
Screenshot_20220826-203127_OGInsta%2B.jpg
 
Habibu Anga (6)

Sasa ufanyikaji wa tukio lile ni mfano mzuri wa matumizi ya stadi ya ‘phising’ na ‘uhandisi jamii’ katika utapeli. Nitaeleza..

Utapeli wa dizaini hii ni adhimu mno na watu wachache sana ambao wana weledi wa kutosha kuweza kuutekeleza kutokana na ugumu wake na kuhitaji kiwango kikubwa cha maarifa na akili.

Lakini ukifanikiwa kuutekeleza basi utavuna mabilioni ya mapesa. Ndio maana waona watu kama akina Mompha na Hushpuppi walikuwa wanaishi maisha ya anasa kama Wafalme.

Utapeli huu huwa una hatua tano katika utekelezaji wake. Hatua ya kwanza ni Identification (kutambua target), hatua ya pili ni ‘Grooming’, hatua ya tatu ‘Observation’, hatua ya nne ‘Exchange of information’ na hatua ya tano ni ‘funds transfer’.

Sitaki kufundisha vijana wetu utapeli lakini nifafanue kwa mifano halisi utapeli huu adhimu wa BEC namna gani ambavyo akina Hushpuppi na Mompha walikuwa wanafanya na kuvuna mabilioni ya fedha.

Makala hii inapatikana yote kwa ukamilifu kwa members wa Group langu la WhatsApp.

Kuwa mwanachama wa Group unalipia shilingi elfu tano tu kwa mwezi na utapata Makala hii pamoja na Makala nyingine nyingi kwa muda wa mwezi mzima.

Fanya malipo ya shilingi elfu tano kwenda MPESA 0759181457 HABIBU ANGA kisha nijulishe nikuunge na uanze kupokea simulizi.

Unaweza pia kubofya link kwenye bio yangu ambayo itakuleta moja kwa moja inbox whatsapp.View attachment 2335750
Mwendelezo
 
Farhan Jr

Maproo hao hapo wa timu ya taifa ya Zambia na mwingine huyo Malawi hatujui kuhusu mishahara wanayolipwa ila bila shaka ni mikubwa sana, timu imesafiri ugenini Sudan kwa ajili ya Mini Tournament na ukumbuke imetoka Misri pia kwa Pre Season.

Kumbuka hatua zote za CAF unacheza kula, kulala na usafiri ni bajeti yenu huo mzigo wa kuvuka zile hatua muhimu unatolewa baada ya msimu kuisha, maana yake bajeti lazima iwe nono.

Ila ukisikia watu wanavyomjadili MO Dewji, yani wanamchukulia kawaida sana yani ni kama wanahisi anainyonya sana Simba, ila vitu kama hivi ni ngumu wao kujadili wakuu Image building sio kitu rahisi, wakina MO wanaumia sana hamjui tu.

Hapo sijataja bonus zao, hapo sijataja hata vile ‘vizinga’ anavyopigwa maana ni kawaida tu kwa Maboss

Screenshot_20220829-101425_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Niliandika kitu kuhusu MO Dewji kisha nikazima data nikapumzika kwakuwa ilikuwa usiku sana, naamka napitia comments, Insta mpaka WhatsApp nahisi hatujaelewana.

Naomba siku moja nikipata wasaa nitawapa vitu kutoka kwenye kitabu kimoja nachomalizia kukisoma “FOOTBALL IS NOTHING THAN A PRESTIGIOUS GAME”

Ni kitabu kizuri sana kinachozungumzia mpira kuanzia Pre Bosman na Post Bosman era, kinazungumzia kuwa mpira sio biashara kama ambavyo wengi wanadhani bali ni Mchezo wa sifa tu.

Kitabu kinasema Matajiri wanaowekeza kwenye mpira au Matajiri wanaosimamia mpira wameingia kama sehemu ya sifa kwa timu zao na kuhakikisha timu zinapata furaha kwakuwa ni furaha yao pia.

Leo hii watu wanasema Simba ina Wadhamini ambao wanahesabika wote, lakini duniani kuna klabu kama Real Madrid na Barcelona, Manchester United na bado zina madeni, unafahamu ni kwanini? Hiyo ni homework.

Leo hii Real Madrid ili uwe mgombea wa Urais lazima uwe na sifa ya kukopesheka kwenye benki zinazotambulika na mamlaka, ambazo ni EURO MILLION 124 ambayo ni sawa na 15% ya bajeti ya Real Madrid kwa mwaka, unafikiri ni kwanini? Homework hiyo naiacha.

Juzi Rais wa Barcelona Joan Laporta na Mhazini wa klabu Ferran Olive walitoa zaidi ya Pauni Million 20 ambazo ni pesa zao binafsi, ili Jules Kounde asajiliwe kwenye mfumo wa LA LIGA, unafikiri ni kwanini? Simply ni kuwa mpira bado sio biashara mnayoisema na hauna hela hivyo.

Nachomaanisha ni kuwa sahau kuhusu hizo pesa za Wadhamini ambazo zinatoka kwa mkupuo sio zote kwa pamoja, sahau kuhusu TV rights, sio rahisi kuendesha timu za mpira na zikapata matokeo, ukihitaji timu ipate matokeo lazima uende nje ya bajeti, huo ndio ukweli.

Kwa mwaka Simba bajeti yao ni BILLION 12, hiyo ni bajeti ya kwenye makaratasi tu tena ya timu moja ya Kiume, hujataja Simba Queens na timu za vijana, can you imagine? Hizo pesa zinatoka wapi?

Ni rahisi sana kumwondoa MO kwenye equation kwasababu zenu binafsi ila mpira sio biashara duniani kote, FOOTBALL IS A PRESTIGIOUS GAME.

Screenshot_20220829-101555_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Acha sasa nifunge mjadala wangu kwa mfano mwepesi na wa mwisho kabisa, mfano mnaposikia Mdhamini Mkuu atatoa BILLION 26, sio kwamba yote inatolewa bali ni INSTALLMENTS yani kwa mikupuo, mfano billion 4 kwa mwaka.

Lastly, Roman Abramovich alikuwa ni Mmiliki wa Chelsea narudia alikuwa MMILIKI wa Chelsea na Chelsea wana wadhamini wengi na mikataba mikubwa sana ila Roman amesamehe deni lake alilokuwa anaidai Chelsea.

Sasa kwanini tunaposema mpira bado sio biashara hatuelewani?? Roman licha ya kumiliki Chelsea bado alikuwa anatoa pesa zake nje ya mfuko wa Chelsea kwakuwa pesa haikidhi mahitaji ya timu.

Hivi kununua Mchezaji Million 200 kisha unakuja kushindania kombe lenye thamani ya Million 100 mnadhani kuna faida? Mbona tunaposema football is a non profit organization hatuelewani?

Wanakuja sasa Wamarekani kwenye mpira ndio hao sasa wanataka kuupa taswira mpya mpira na kuwa biashara, mpaka pale ambapo Franchise system ikitumika kwenye mpira ndipo pesa yake itaonekana.

Franchise ni mfumo ambao timu hazishuki daraja, mpaka labda uwekezaji udorore ndipo mwingine achukue nafasi! Mfano IHEFU wanawekeza na walishuka daraja, umefikiria hiyo hasara waliyopata?

Mmesema kuhusu FFP na wengine mkasema kuhusu mfumo wa LA LIGA, je mmesoma vyema ARTICLE 92 of the Financial Control inasemaje? Au tunabishana tu

Naishia hapo! MPENI HESHMA YAKE MO, wapeni heshma Matajiri wote wanaoweka pesa zao kwenye huu mpira.

Screenshot_20220829-132757_OGInsta%2B.jpg
 
Mkoa wa Tabora unaongoza Mikoa ya Kanda ya Kati kwa Tanzania Bara kwa uwiano mkubwa kati ya Wakazi wa Mkoa huo na laini za simu zilizosajiliwa, kwa mujibu wa takwimu za hivi karibuni za mawasiliano nchini, hadi Juni 2022 laini 3,000,849 za simu zilikuwa zimesajiliwa Mkoa wa Tabora, wenye Wakazi wanaokadiriwa kuwa zaidi ya Milioni mbili.

Takwimu hizo za kila robo mwaka, zilizotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), zinaonyesha kwamba Singida ni ya pili kwa wingi wa laini zilizosajiliwa, kwa Kanda ya Kati ikiwa na laini 1,397,359, aidha takwimu hizo zinaonesha kwamba jumla ya laini 56,153,097 zilikuwa zimesajiliwa hadi Juni 2022 kwa nchi nzima; huku mikoa 10 ikisajili zaidi ya laini milioni mbili kila mmoja.

Baadhi ya Idadi ya laini zilizosajiliwa kwenye mikoa hiyo, ni Tabora 3,000,849, Kigoma 1,257,318, Singida 1,397,359, Mbeya 2,961,516, Morogoro 2,945,790, Dodoma 2,864,302, Kilimanjaro 2,211,867, Tanga 2,098,929, na Geita 2,050,124.

Hata hivyo, ifahamike kwamba idadi ya laini zilizosajiliwa hailingani na idadi ya Watumiaji, ambao ni wachache zaidi kwakuwa kuna Watu wenye laini zaidi ya moja, kanuni zinaruhusu Mtu kusajili hadi laini tano (5) kwa matumizi mbalimbali, kwa mfano intaneti.

Vilevile, kuna sababu nyingi zinazofanya Watu kuwa na zaidi ya laini moja; zikiwemo kutokupatikana huduma za mtandao husika eneo fulani au utaratibu wa baadhi ya ofisi ambamo Watumishi wanapewa namba za kazini na wanakuwa na za binafsi.
Screenshot_20220830-040309_OGInsta%2B.jpg
 
Mkazi wa kijiji cha Chioli, Kata ya Songolo Wilayani Chemba, Dodoma, Nada Songo ( 45 ) amefariki dunia baada ya kujeruhiwa kwa risasi maeneo ya kifuani na mguu wa kulia na Askari Polisi wakati akiwashambulia Askari hao kwa mishale inayodhaniwa kuwa ya sumu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno ambapo amesema Mtuhumiwa huyo alijeruhiwa kwa risasi baada ya kukaidi kukamatwa kuhusuiana na kosa ambalo alikuwa anatuhumiwa nalo la kutishia kuua kwa silaha za jadi (mishale).

Otieno amesema Mtuhumiwa alihatarisha amani katika Kitongoji cha Manyata Kijiji cha Chioli kwa kushambulia Watu kwa mishale yenye sumu na Polisi walipokwenda kwa ajili ya ukamataji, alitoroka na kukataa amri halali ya kukamatwa kuhusiana na makosa yake.

“August 28, 2022 Polisi walipata taarifa ya kurejea kwa Mtuhumiwa huyo huku akiendelea kutishia usalama wa Watu katika Kitongoji hicho, Askari walipokwenda kumkamata aliwashambulia kwa mishale ambayo inadhaniwa ina sumu na kumjeruhi askari namba H.9377 PC William, tumboni upande wa kushoto na Askari wa akiba aitwaye Madodo Juma ambaye amejeruhiwa kwa mshale mguu wa kulia”
Screenshot_20220830-040728_OGInsta%2B.jpg
 
Siku moja baada ya Tanzania kupoteza kwa kufungwa 1-0 dhidi ya Uganda katika mchezo wa kuwania kufuzu CHAN, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetangaza kumuondoa Kocha Mkuu wa Taifa Stars Kim Poulsen Raia wa Denmark pamoja na Wasaidizi wake.

Poulsen anaondoka katika nafasi ya Ukocha Mkuu Taifa Stars na kusalia katika Timu za Vijana hadi mkataba wake utakapomalizika, nafasi ya Kim itachukuliwa na Hanour Janza, akisaidiwa na Meck Mexime huku Juma Kaseja akiwa Kocha wa Magolikipa.
Screenshot_20220830-041236_OGInsta%2B.jpg
 
Club ya Azam FC imetangaza kuachana na Kocha wake Mkuu Abdihamid Moallin pamoja na Msaidizi wake Omar Nasser na sasa Timu itakuwa chini ya Kocha wa Makipa Daniel Cadena mwenye leseni ya UEFA Pro.

Hata hivyo Azam FC imetangaza kuwa Moallin na Omar hawataondoka Azam FC badala yake watapangiwa kazi nyingine, Azam FC hadi sasa msimu huu imecheza mechi 2, imeshinda moja na sare 1
Screenshot_20220830-041346_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia amewaaapisha Majaji na Kamishna Jenerali wa Magereza leo Ikulu Chamwino, Dodoma ambapo amesema “Nakutaka Kamishna Jenerali wa Magereza uende ukaiongoze Taasisi hii kwa weledi mkubwa, Taasisi hii iliacha njia, ile kazi ya msingi ya kurekebisha tabia na kulinda haki za Watuhumiwa/Wafungwa wakiwa kule”

“Wafungwa ni Wanadamu kama Binadamu wengine, wanatakiwa kupata hewa safi, wanatakiwa kupata mavazi na chakula kizuri, sio kwamba Wahalifu na adhabu ziwe nyinginyingi, ile tu kumuweka kule peke yake ni adhabu, kwahiyo Kamishna nenda kalinde haki zao”

“Changamoto za Magereza zilizojitokeza nawe Kamishna ni Mchangiaji wa changamoto hizo kwasababu uko humo muda mrefu, kwahiyo nenda kakae, tafakari na wenzio, mna changamoto zipi nenda karekebishe changamoto hizo, karekebishe utawala bora, ikibidi mpeleke Watu mafunzo”

“Sio wote wanaoletwa kule ni Mihalifu iliyokubuhu, tunatoa misamaha ya Wafungwa lakini Mtu anasamehewa leo baada ya siku mbili yuko Mahakamani anarudi tena, wakiulizwa kwanini anasema ‘sasa nifanye nini huku nje?’ anafanya kosa makusudi ili arudi lakini mngemrekebisha na kumfundisha cha kufanya akitoka huyu Mtu asingetamani kurudi tena kule”
Screenshot_20220830-041438_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia amewaaapisha Majaji na Kamishna Jenerali wa Magereza leo Ikulu Chamwino, Dodoma ambapo amesema “Ukiingia mitandaoni na ukisikiliza malalamiko ya Wananchi lawama dhidi ya Mahakama zimepungua sana, Majaji sasa wanafanya kazi vizuri, maboresho ya kiutendaji yaliyofanywa Mahakamani vinachangia hili, pia weledi wa Mahakimu na kwasababu tumeongeza idadi ya Majaji Wanawake”

“Majaji Wanawake pamoja na weledi, mnasoma wote, sifa mnazo wote lakini wanakuwa weledi zaidi, wanakuwa waadilifu zaidi, dhambi ambazo utazishika kwa Majaji Wanaume huzikuti kwa Majaji Wanawake lakini anahukumu kwa moyo, Jaji Mwanamke, kama ni Mtoto anamuangalia yeye kama Mama, pamoja na kufuata sheria, Jaji Mwanamke anakuwa amekaa vizuri kwenye mila, desturi na mambo mengine ya Kitanzania”

“Jaji Mwanaume unaletewa Mtu kapigwa kachakazwa huko halafu unamuuliza wewe kabila gani ‘Mkurya’ unajibu ‘sasa si ndio ya kwenu hayo sasa unakuja kufanyaje hapa?’, kwahiyo Majaji Wanawake wanakaa vizuri zaidi kwenye kuhukumu kuliko Wanaume”

“Lengo langu ni kuelekea 50/50 ili Mahakama ya Tanzania tukae vizuri zaidi, kwahiyo Majaji Wanawake siwateui tu kwamba ni Wanawake, napima sifa na uwezo wako na yale yote ambayo Tume itapendekeza kwangu, hongereni Majaji Wanawake, msiende kuniangusha, mkikaa kwenye kiti nyinyi sio Wanawake ni Majaji”
Screenshot_20220830-041600_OGInsta%2B.jpg
 
Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi 2022, Anne Makinda akiwa Dar es salaam leo amesema Serikali imepanga pia kufanya Sensa ya majengo mara tu baada ya kukamilika kwa zoezi la kuhesabu Watu.

“Sensa hii itajumuisha kukusanya taarifa za majengo yote ya makazi na yasiyo ya makazi nchi nzima kwa ajili ya kuboresha Sera na kupanga mipango ya kimkakati ya kuboresha sekta ya nyumba nchini”

“Zoezi hili litafanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 30 Agosti, 2022 hadi tarehe 01 Septemba, 2022, natoa wito kwa Wananchi wote kuendelea kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Makarani waliowahesabu katika maeneo yenu kwa kutoa taarifa sahihi za majengo.

“Makarani waliofanya Sensa ya Watu na Makazi ndio hao hao watapita kwenye majengo yote yaliopo kwenye maeneo ya kuhesabia Wati ili kukusanya taarifa za majengo”

“Napenda kuwashukuru tena Wananchi wote kwa mwitikio mkubwa walioonesha katika kipindi chote cha maandalizi na wakati wa kuhesabu Watu, ni lazima ujivunie kama Mtanzania kuwa umehesabiwa na kuwa umejumuishwa katika mipango ya maendeleo ya nchi yako”
Screenshot_20220830-041942_OGInsta%2B.jpg
 
Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi 2022, Anne Makinda akiwa Dar es salaam leo amesema endapo itatokea Mtu hajahesabiwa hadi kufikia leo tarehe 29 Agosti, 2022 ambayo ni tarehe ya mwisho ya zoezi hilo, bado atakuwa na nafasi ya kuhesabiwa.

Makinda amesema “Katika kufanikisha hili, Mwananchi unashauriwa uende moja kwa moja kwenye Ofisi za Serikali za Mitaa onana na Mwenyekiti au Mtendaji wa Mtaa unaoishi na hakikisha unawachia namba ya mawasiliano ili Karani akufuate ulipo na kuanza kazi ya kukuhesabu”

“Kwa maeneo ya Vijijini Mwananchi ambaye hajahesabiwa aende kwenye Ofisi ya Mwenyekiti wa Kitongoji anachoishi acha namba ya mawasiliano ili Makarani wakufuate ulipo ili wakuhesabu”

“Ofisi ya Taifa ya Takwimu imeandaa Namba maalumu za mawasiliano (Call Centre) kwa ajili ya Wananchu ambao hawajahesabiwa kupiga simu moja kwa moja makao makuu Dodoma ili utaratibu wa kupeleka karani eneo husika ufanyike kwa wakati, namba hizo ni:- 0753665491; 0764443873; 0626141515; 0784665404 na 0656279424”

“Namba hizi zitaanza kutumika tarehe 30 Agosti, 2022 hadi tarehe 5 Septemba, 2022, ikiwa ni muda wa siku 7 wa ziada ili kumwezesha mwananchi kupata haki yake ya msingi ya kuhesabiwa, nawasihi Wananchi busara itumike ya kutumia hizi namba kwa lengo tu la kufanikisha Sensa na siyo vinginevyo”
Screenshot_20220830-042042_OGInsta%2B.jpg
 
Mshambuliaji wa Afrika ya Kati mwenye asili ya Congo DR Cezar Manzoki (25) amejiunga na Club ya Dalian Pro ya China akitokea Vipers SC ya Uganda kwa mkataba wa miaka mitatu.

Manzoki aliyekuwa anahusishwa na Simba SC kwa kiasi kikubwa hadi uvumi kusema ameshasaini Simba SC, amejiunga na Dalian Pro kwa ada ya uhamisho ya USD 400,000 (Tsh Milioni 932).

Manzoki alikuwa Mchezaji bora wa Uganda 2021/2022 na alikuwa Mfungaji bora pia wa Ligi Kuu Uganda msimu huo kwa kufunga magoli 18, Mchezaji bora wa Wachezaji na Mshambuliaji bora wa msimu.
Screenshot_20220830-042254_OGInsta%2B.jpg
 
Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi 2022, Anne Makinda akiwa Dar es salaam leo amesema zoezi la kuhesabu Watu lililoanza usiku wa kuamkia tarehe 23 Agosti 2022 hadi kufikia tarehe 29 Agosti, 2022 linaendelea vizuri ambapo kiwango cha kaya ambazo zimehesabiwa kimefikia asilimia 93.45.

Makinda amesema”Haya ni mafanikio makubwa yaliyotokana na utayari mkubwa wa Wananchi kushiriki kuhesabiwa kwa ajili ya maendeleo ya Nchi, kulingana na ratiba ya zoezi la kuhesabu Watu ambalo linatakiwa kuhitimishwa tarehe 29 Agosti, 2022 lilitakiwa lifanyike kwa siku 7 kuanzia tarehe 23 hadi 29 Agosti, 2022”

“Aidha, taarifa zilizokwishakusanywa zinaonesha kuwa bado kuna asilimia 6.55 ya kaya ambazo hazijahesabiwa, inawezekana tusiweze kufikia kaya zote zilizobaki kwa leo na lengo letu ni kuhakikisha kila mtu anahesabiwa”

“Kutokana na hali hiyo, napenda kutoa wito kwa Wananchi wote ambao hawajahesabiwa wahakikishe wanatoa ushirikiano wa kutosha kwa Makarani wa Sensa waliopo katika maeneo yao ili wahesabiwe kabla ya leo jioni ya tarehe 29 Agosti, 2022 jioni”

“Makarani wa Sensa wapo wa kutoka katika maeneo ambayo bado kaya nyingi hazijahesabiwa, Waratibu wa Sensa katika Wilaya wamefanya utaratibu wa kuongeza Makarani kutoka maeneo ya jirani ambapo wamekamilisha kuhesabu kwenda kwenye maeneo yenye uhitaji ili kazi hiyo ikamilike kwa wakati”
Screenshot_20220830-042351_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom