Makapuku Forum

Makapuku Forum

_126410789_gettyimages-1417084512.jpg

...sio chama langu lakini napenda Liverpool alivyopoteza.
Wiki nzuri huanza namna hii
 
Sitaki Ndoa! (A Short Story)- 1

Jane alikuwa amekaa huku akimuelekea Padre, kushoto kwake alikaa Moses. Moses walikuwa wameishi na Jane kama wandani kwa muda wa miaka 10. Katika hiyo karibu tukae walibahatika kupata mtoto mmoja wa kiume, Haruna.

Jane alipokuwa anapita, mwanaume yoyote yule hasa yale mafisi asingeacha kugeuka. Alikuwa mrefu kidogo, na makalio makubwa kama yale ya sajari za Uturuki. Kwa asili mwanamke huyu alikuwa mweupe lakini sasa weupe wake ulikolezwa zaidi kwa mkorogo. Ngozi yake ilikuwa imeanza kuwa nyekundu na nyembamba mpaka mishipa ya damu kuanza kuonekana kutokana na matumizi ya mkorogo ya muda mrefu. Hakuwa na elimu kubwa sana, bali kidato cha 4.

"Moses umesikia alichosema mchumba wako", Padre alimuuliza Moses, swali lililomstua Moses kutoka kwenye lindi zito la mawazo. Ukweli Moses hakusikia alichosema Jane. Ni mwili tu ndio ulikuwa pale lakini akili yake ilikuwa maili elfu nyingi sana.

Kijana huyu wa Kijita alikuwa mtanashati kama asili ya Wajita ilivyo. Muda wote alikuwa anafunga tai na kalamu kwenye mfuko wa shati utafikiri mwalimu mkuu, kumbe alikuwa anauza spare za magari Ilala. Nywele zake alizinyoa kwa umaridadi sana hali iliyofanya avutie kumuangalia. Aliongea kwa mikogo na alikuwa mtu mwenye masihara muda wote. Watu wengi walikuwa wanafikiri Moses hakuwahi kujua mateso au shida katika maisha yake.

Mapenzi yakikuvuruga mwendo wa kilomita 5 unaweza kuwa mrefu kama safari ya kwenda mwezini. Unaweza kutembea ukatamani hata kuongea na kuku angalau wajue maswahibu yako. Mapenzi yamechukua maisha ya watu wengi sana hapa duniani, na waliobaki hai wengine vichwa vyao vimevurugwa. Hiki ndicho alichokuwa anapitia Moses.

Moses alikumbuka yote. Yote. Jinsi alivyokutana na Jane kwa mara kwanza. Alivyotupa swaga zake za Kijita hadi kumnasa mrembo huyu wa Kinyakyusa.
"Moses sioni siku zangu", alikumbuka maneno hayo kutoka kwa Jane. Jane alikuwa amenasa. Moses aliyakumbuka maneno hayo ya miaka 10 iliyopita kama ameambiwa jana tu. Pengine bila Jane kunasa hiki kinachoongelewa leo kisingekuwepo. Pengine kila mtu angekuwa na njia yake na mtu wake na maisha yake...!

Itaendea....
Visa na Wahusika vyote ni vya Kubuni.
Screenshot_20220825-211405_OGInsta%2B.jpg
 
Sitaki Ndoa-2 ( A Short Story)

"Tunataka harusi yako iwe ya mfano Moses, wewe huwa unajitoa sana kwenye matatizo ya wengine", maneno ya mwenyekiti wa kamati ya harusi ya Moses na Jane yalipita tena akilini mwa Moses. Wakati huu machozi yalikuwa yanamtoka Moses. Mwamba alikuwa analia. Wakati huu kama ungemweka mjusi mbele yake angemuona kama mamba.

Jane alinyanyuka akaenda kumshika begani Moses. "Moses tulia, vumilia wewe sio wa kwanza, yatapita na utazoea", Jane aliongea bila kituo. Moses hakuamini ujasiri wa Jane.

"Lakini kwa nini kama hukutaka ndoa hukusema toka mwanzo. Kwanini ? Mpaka tumeitisha vikao na watu wametuchangia na harusi ni wiki ijayo tu. Kwanini hukusema Jane?", Moses alikuwa akibubujikwa na machozi wakati anayaongea hayo.

Kawaida ya Kanisa Katoliki, kabla harusi haijafungwa huwa inatangazwa Jumapili 3 mfululizo wakati wa Ibada. Matangazo huwa yanasomwa Kanisani maeneo yote ambayo wanandoa waliwahi kukaa, ili kama kuna mtu yeyote anapingamizi atoe taarifa kwa Paroko. Harusi yao ilikuwa imetangazwa maeneo mengi sana Kuanzia kijijini kwa Moses huko Chumwi Majita, Mwananyamala alikoanzia maisha na Tabata ambako sasa wanaishi. Kwa upande wa Jane hakuishi maeneo mengi sana ukiacha kwao Luanda Nzovye na Buza kwa Mpalange kwa dada yake. Mtu aliyeweka pingamizi Kanisani alikuwa Jane mwenyewe. Jane huyu huyu bi harusi mtarajiwa. Kwa sasa Jane haitaki tena ndoa. Hata kama ungempa jua na mwezi wake, Jane hataki kufunga ndoa. Kwa kifupi Jane hataki kuolewa na Moses. Hataki kabisa.

"Jane kwa nini hutaki kufunga ndoa", Padre alimuuliza Jane.

"Father, nimekaa na Moses kwa muda wa miaka 10. Nina mjua, ananijua vizuri, lakini kufunga nae ndoa sitaki ".....

Kwanini Jane hataki tena kufunga ndoa na Moses... Itaendelea
Screenshot_20220825-211405_OGInsta%2B.jpg
 
Sitaki Ndoa!- (A Short Story ) - 3

"Sasa kwa nini hutaki ndoa", aliuliza tena Padre.

"Padre si ukweli unamweka mtu huru?", ilikuwa zamu ya Jane kuuliza sasa.

"Mkitaka niseme ukweli, nitausema", alisema Jane

"Hatuko kituo cha Polisi wala hatuko mahakamani mwanangu Jane", alisema Padre na kuongezea, "Ninyi mmekuwa pamoja muda mrefu, kwa sasa mnachotaka kufanya ni kuyakabidhi maisha yenu mikono mwa BWANA kwa ndoa Takatifu."

"Naelewa Padre, lakini siko tayari" alilisitiza Jane.

Wakati wote huu Moses alikuwa kimya.

"Tatizo ni nini Jane, nimewahi kukupiga, mmewahi kula njaa, nimewahi kushindwa kukupa matumizi", aliuliza Moses.

"Hapana Moses, wewe ni mwanaume na nusu zaidi wewe ni mtu mwema sana na siku zote umekuwa baba mzuri kwa mtoto wetu", alisema Jane

"Tatizo ni nini sasa", aliuliza tena Moses.

"Tatizo ni kwamba sishibi", Jane alidakia.

Padre alishtuka kidogo na kumgeukia Moses, "Moses umekuwa muamini mzuri sana, unashiriki jumuiya, michango yote unatoa, lakini hununui chakula nyumbani kwako"

"Chakula Padre, nenda kwangu friji limejaa vyakula, stoo kuna mchele na mahindi ya kutosha hata miezi 6", Moses alijieleza na kukumbuka maneno kwamba mapenzi yakifika mwisho, hata panya akidondosha glasi unaambiwa ni wewe. Kumbe Jane alikuwa na chakula chake.

"Father, ngoja niseme, nieleweke vizuri. Kwa kweli tangu nianze mahusiano na Moses hajawahi kuniridhisha. Hajawahi kunifikisha kileleni." wakati huu Jane alikuwa ameangalia pembeni.

"Mimi napenda sana kufanya mapenzi, lakini mwenzangu ndio hivyo amekuwa hanifikishi popote. Najuta kwamba katika kipindi chote hicho nimekuwa nikilala na wanaume wengine ili kukata kiu yangu. Hiyo ndio sababu sitaki Ndoa. Sitaki kuzini nikiwa kwenye ndoa. Niko tayari tuishi hivi hivi mpaka tuzikane lakini sio kufunga ndoa." alimaliza na kisha akamgeukia Moses ambaye wakati huu alikuwa ameegea meza.

"Nakupenda Moses, lakini ndoa na wewe sitaki"

Padre alimuita Moses, Moses hakuitika, akampiga piga begani, Moses hakushtuka, Padre akapiga kelele kuomba msaada kisha kumkimbiza hospital ya misioni iliyokuwa mita chache kutoka hapo parokiani.

"Mgonjwa wenu ameishafariki, poleni sana" daktari alisema.
Screenshot_20220825-211405_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom