Makapuku Forum

Makapuku Forum

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limesema linawasaka watuhumiwa wa wizi wa basi la daladala liliripotiwa kuibwa Agosti 23 mwaka huu maeneo ya Chanika.

Kwa mujibu wa taarifa iliyolewa leo Agosti 29, 2022 na Kaimu Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, Wiliam Mkonda (pichani) imeeleza kuwa, Jeshi hilo pia limewakamata watuhumiwa 15 kwa tuhuma za uvunjaji na kuiba vifaa vya ujenzi katika ghala la Voila Trading Co (T) Ltd lilopo Kiwalani linalomilikiwa na raia wa China.

“Baada ya taarifa hizo Jeshi la Polisi liliendelea na ufuatiliaji ambapo Agosti 25 mwaka huu lilifanikiwa kulipata basi hilo limeegeshwa maeneo ya Tabata.
Screenshot_20220830-042611_OGInsta%2B.jpg
 
Jaji Mkuu mstaafu wa Tanzania, Mohammed Chande Othman, amewasili nchini Kenya kwa ajili ya kuongoza jopo la majaji wengine wa Afrika kutoka katika Jukwaa la Majaji na Wanasheria Afrika watakuwa na kazi ya kutazama mwenendo wa kesi za kupinga matokeo ya uchaguzi wa Rais uliofanyika Agosti 9, 2022.

Katika uchaguzi huo, mgombea wa Kenya Kwanza William Ruto alitangazwa mshindi kwa kupata kura milioni 7.1 akifuatiwa na mgombea wa Azimio la Umoja, Raila Odinga aliyepata kura milioni 6.9

Hata hivyo Odinga amefungua kesi Mahakama ya Juu ya Milimani akipinga matokeo hayo akidai kulikuwa na udanganyifu ulioratibiwa na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) ya Kenya chini ya Mwenyekiti wake Wafula Chebukati.

Chande ameongozana na ujumbe wa wanasheria mashuhuri Afrika ambao ni Lilian Tibatemwa-Ekirikubinza kutoka Mahakama ya Juu ya Uganda, Ivy Kamanga kutoka Mahakama ya juu ya Rufaa ya Malawi, Moses Chinhengo kutoka mahakama ya juu ya rufaa ya Lesotho na Rais wa mahakama ya uchaguzi ya Afrika kusini, Henry Mbha.

Screenshot_20220830-042730_OGInsta%2B.jpg
 
Golikipa Juma Kaseja amechaguliwa kuwa kocha wa makipa wa timu ya Taifa Stars

Screenshot_20220830-042829_OGInsta%2B.jpg
 
Wachezaji wa Yanga wamefanya mazoezi ya gym wakijiweka fit kwa ajili ya mechi zijazo za Ligi Kuu ikiwemo Dar es Salaam Derby dhidi ya Azam Septemba 6.
Screenshot_20220830-042955_OGInsta%2B.jpg
 
Kocha Honour Janza raia wa Zambia na kocha wa Namungo rasmi ametangazwa kuwa Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa Tanzania (Taifa Stars) akichukua nafasi ya Kim Poulsen
Screenshot_20220830-043431_OGInsta%2B.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Pique kama Onyango, Benchi
.
Beki wa Barcelona, Gerrard Pique bado hajapata nafasi ya kucheza mchezo wowote tangu ligi ianze msimu huu
Screenshot_20220830-044235_OGInsta%2B.jpg
 
KIM POULSEN NDO BASI TENA STARS
.
TFF imefikia Makubaliano ya kumuondoa Kocha wa timu ya Taifa "Taifa Stars" Kim Poulsen kwenye benchi la Ufundi pamoja na wasaidizi wake.
.
Kwa wakati huu benchi la ufundi la Taifa Stars litakuwa chini ya Kocha Hanour Janza akisaidiwa na Meck Maxime na Kocha wa magolikipa Juma Kaseja.
Screenshot_20220830-044545_OGInsta%2B.jpg
 
Hakuna ubishi, BRUNO Fernandes ndiye mchezaji muhimu kabisa kwa sasa kwenye kikosi cha Manchester United.
Screenshot_20220830-045113_OGInsta%2B.jpg
 
BISHOO amerejea na moto mpya msimu huu:
.
—4 mechi
️—6 mabao
—6 assists
.
Neymar amehusika katika mabao 12 kwenye mechi 4 tu
Screenshot_20220830-045207_OGInsta%2B.jpg
 
KIPARA ATOA ONYO KALI
.
Kocha wa Manchester City, Mtaalam Pep Guardiola amewaonya wachezaji wake wasitegemee ushindi wa kusawazisha mabao kwani itakuja kuwaletea madhara zaidi, wakiendela na mtindo huo.
.
“Tatizo tunaruhusu mabao mengi sana, tunapata tabu sana kupata matokeo, tumeshinda mechi lakini lazma tujifunze kupitia hili, siku nyingine hatuwezi kurudi tena mchezoni, ningependa ushindi wetu ungekuwa 4-0, lakini kwa mtazamo huu nadhani watajifunza,” alisema Guardiola kwa hasira.
.
“Huu ushindi ulitokana na mawazo yangu ambayo yalibadilisha mchezo mzima, lakini Haaland ameendeleza ubabe wake tangu alipozaliwa, kila mahali anapokwenda anafunga mabao,” aliongeza Guardiola.

………………
Screenshot_20220830-045255_OGInsta%2B.jpg
 
Kwenye mchezo wa FA kati ya Arsenal dhidi ya Liverpool 2002, nyota wa Liverpool Jamie Carragher alipigwa na sarafu ya pauni moja inayoaminika ilirushwa na shabiki wa Arsenal, kwa hasira akaitupa sarafu hiyo jukwaani.

Baada ya kufanya hivyo Jamie alipewa kadi nyekundu, akapigwa faini ya Pauni 40,000 na kufungiwa kwa muda timu ya taifa ya England.

Hasira hasara
Screenshot_20220830-045829_OGInsta%2B.jpg
 
Baada ya Erling Halaand kupiga mabao matatu dhidi ya Crystal Palace amesema wazi kuwa anaifukuzia rekodi ya Baba yake ambapo alifunga mabao 18 jumla na sasa amesalia na mabao 12 aifikie rekodi hiyo

Halaand amefunga mabao sita kwenye mechi nne za EPL na assists moja huku akiwa kwenye kiwango bora sana dhidi ya vijana wa Patrick Viera

“Nina furaha kubwa kwangu na familia yangu kuifukuzia rekodi ya Baba yangu ambaye alikuwa akinitania kuwa ana mabao mengi ya EPL kuliko Mimi hivyo napambana kuifikia” alisema Halaand
Screenshot_20220830-045938_OGInsta%2B.jpg
 
Sidhani kama dirisha moja tu la usajili lina majibu ya maswali yote ya Azam FC, nadhani wanahitaji madirisha mengine mawili to the maximum ili kupata kitu.

Huenda dirisha hili wakapata wachezaji wawili wa maana wakafit kwenye timu kisha dirisha lijalo wakapata watatu jumla watano ndipo hapo timu itakuwa imeunganika ipasavyo na tayari kwa mapambano.

Bado Simba na Yanga nawaona ni mlima mrefu kwa Azam kwakuwa wote wanaenda kwenye usajili kuziba wakati Azam anaenda kusajili ili kujenga kikosi.
Screenshot_20220830-050202_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom