Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,081
- 464,013
Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Petroli nchini Kenya (EPRA) imetangaza kupanda kwa bei ya mafuta kwa Ksh. 9 (Tsh. 178.47) katika ukaguzi wake wa kila mwezi.
Kwa muda wa mwezi mmoja ujao lita moja ya petroli jijini Nairobi itagharimu Ksh.159.12 ( Tsh. 3,160.70), dizeli Ksh. 140 (Tsh 2,785.65) na mafuta ya taa Ksh. 127.94 (Tsh. 2,541.35).
EPRA imesema Serikali itatumia Hazina ya Maendeleo ya Petroli (PDL) kuwaepusha watumiaji kutokana na bei hizo za juu ambapo badala ya Watumiaji kulipia gharama yote husika, Serikali italipa sehemu ya ongezeko kupitia ruzuku.
Kwa sasa Madereva wa Nairobi wanalipa Ksh. 159.12 (Tsh 3,160.70) kwa lita moja ya petroli lakini walipaswa kulipa Ksh.184.68 (Tsh.3,668.41) na imepungua kutokana na Serikali kuwasaidia kulipa Ksh.25.76 (Tsh. 511.69) kupitia ruzuku, kwa upande wa diesel Serikali inalipia Ksh. 48.19 (Tsh. 957.23)
kwa lita kupitia ruzuku na mafuta ya taa ruzuku inayolipwa na Serikali ni Ksh. 42.43 (Tsh.957.23) kwa lita na kwamba bei hizi zinajumuisha kodi na zimerekebishwa ili ziendane na mfumuko wa bei.
Kwa muda wa mwezi mmoja ujao lita moja ya petroli jijini Nairobi itagharimu Ksh.159.12 ( Tsh. 3,160.70), dizeli Ksh. 140 (Tsh 2,785.65) na mafuta ya taa Ksh. 127.94 (Tsh. 2,541.35).
EPRA imesema Serikali itatumia Hazina ya Maendeleo ya Petroli (PDL) kuwaepusha watumiaji kutokana na bei hizo za juu ambapo badala ya Watumiaji kulipia gharama yote husika, Serikali italipa sehemu ya ongezeko kupitia ruzuku.
Kwa sasa Madereva wa Nairobi wanalipa Ksh. 159.12 (Tsh 3,160.70) kwa lita moja ya petroli lakini walipaswa kulipa Ksh.184.68 (Tsh.3,668.41) na imepungua kutokana na Serikali kuwasaidia kulipa Ksh.25.76 (Tsh. 511.69) kupitia ruzuku, kwa upande wa diesel Serikali inalipia Ksh. 48.19 (Tsh. 957.23)
kwa lita kupitia ruzuku na mafuta ya taa ruzuku inayolipwa na Serikali ni Ksh. 42.43 (Tsh.957.23) kwa lita na kwamba bei hizi zinajumuisha kodi na zimerekebishwa ili ziendane na mfumuko wa bei.


: VILABU BORA 20 AFRIKA