Makapuku Forum

Makapuku Forum

PHIRI is RED

Nyieeee mmesika huku Simba ni lidule flaniii hivi
Screenshot_20220615-165119_OGInsta%2B.jpg
 
"Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zimekubaliana kuongeza Ushuru wa Forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 35 kwenye nywele bandia zinazotambulika kwa
Heading 6704"

"Hatua hii inalenga kulinda wazalishaji wa ndani wa bidhaa hizo, kuongeza ajira pamoja na kuongeza mapato ya Serikali" ——— Dr. Mwigulu

hata mkiweka 100% tutanunua tuView attachment 2261648
Sasa Auntie hapa itakuwaje? Maana ndiyo mambo yako haya

Mimi nitabaki kwenye para langu hili hili....
 
KIUNGO YANGA NDO BASI TENA
.
Ikiwa imebakiza mechi nne tu kumaliza Ligi Kuu, Yanga imepata pigo baada ya kuumia kwa kiungo Zawadi Mauya atakayekaa nje ya uwanja hadi msimu ujao.
.
Mauya aliumia goti kwenye mazoezi ya timu hiyo siku chache zilizopita yanayofanyika kambini kwao Avic Town, Kigamboni.
Screenshot_20220615-165819_OGInsta%2B.jpg
 
Boxer, Kaseke wote wajichomoa Yanga
.
Taarifa kutoka ndani ya Singida zimethibitisha nyota wawili wanaocheza Yanga, Deus Kaseke na Paul Godfrey ‘Boxer’ wamesainishwa mikataba ya miaka miwili kila mmoja.
.
Kwa mujibu wa kigogo mmoja wa Singida Big Stars amesema Boxer na Kaseke kila mmoja amesaini mkataba wa miaka miwili na tayari pesa zao za usajili wameshawekewa kwenye akaunti zao.
Screenshot_20220615-170309_OGInsta%2B.jpg
 
Chelsea Yatua kwa Sterling Kisa Lukaku
.
Chelsea ipo kwenye hatua nzuri ya kumuuza straika wao, Romelu Lukaku kwenda Inter Milan na tayari imeshaanza kutafuta mbadala wake kwa kuanza mazungumzo na wawakilishi wa straika wa Manchester City, Raheem Sterling ili kumsainisha katika dirisha hili.
.
Mkataba wa Sterling unamalizika mwaka 2023 na ameonyesha anahitaji kuondoka kwa sababu haoni ikiwa atapata nafasi kwenye kikosi cha kwanza kwa msimu ujao kutokana na maingizo mapya.
.
Msimu uliopita alionyesha kiwango bora akicheza mechi 47 za michuano yote, akafunga mabao 17 na kutoa asisti tisa.
Screenshot_20220615-173256_OGInsta%2B.jpg
 
VLAHOVIC AIZODOA ARSENAL
.
Straika anayekipiga Juventus, Dusan Vlahovic ameichimba mkwara Arsenal kuwa hakukaribia kujiunga na timu hiyo, kipindi cha usajili majira ya kiangazi mwaka jana, licha ya kuhusishwa.
.
“Mawazo yangu yalikuwa Juventus sio Arsenal. Sina kingine cha kusema. Najisikia furaha kujiunga na timu hii. Nina furaha ninapovaa jezi ya Juventus. Hakika nimefiti katika klabu hii. Unapokuja hapa hupaswi kukata tamaa, unatakiwa kucheza kwa juhudi kila wakati" amesema Vlahovic.
.
Awali, taarifa zilidai kuwa Arsenal ilionyesha nia ya kumsajili Vlahovic mwaka huu kwenye dirisha dogo, hata hivyo nyota huyo akaipiga chini ofa hiyo na kujiunga na Juventus.
Screenshot_20220615-173423_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom