Imeandikwa na @swalehmawele
Taifa Stars vs Algeria ( Afcon 2023 Qualifier ).
Kinyumbani zaidi.

Ni mechi ngumu, Taifa Stars itacheza katika ardhi ya nyumbani lakini inakwenda kuingia kama second team mbele ya Algeria ambayo ina kila kitu katika kikosi chao, quality, uzoefu na
form yao katika mechi zao za hivi karibuni.

Taifa Stars inaweza kufunguka mbele ya Algeria? bila shaka ingawa ni hatari mbele ya timu ambayo ina ubora mkubwa katika kuzitumia side ways ( maeneo ya pembeni ) na ubora wa mtu kama Baghdad Bounedjah katika kucheza aina hiyo ya mpira, Djamel Belmadi anafanikiwa.

Kitu kimoja tu kwa wachezaji wa Taifa Stars, uoga wa mechi unaopelekea mipira mingi kupotea hasa kwenye eneo la kiungo, Algeria ni timu hatari kwenye turn overs ( wanapoupora mpira ), kasi, uwezo wa kufungua patterns za ulinzi kwa wapinzani ndio silaha yao nyingine katika kupata matokeo.

Algeria wameshinda michezo mitatu katika mitano ya mwisho, wamepoteza mmoja na sare moja, wamekuwa bora katika kuzuia wakipata cleansheet nne, inahitaji ubora katika kutumia madhaifu machache yatakayojitokeza, si timu inayokuruhusu uwafikie mara nyingi katika eneo lao la mwisho, mtego wa mechi uko hapa.
Kila la kheri kwa Taifa Stars.