Makapuku Forum

Makapuku Forum

Wizara ya Afya imetoa taarifa kwa umma kuhusu mwenendo wa Covid-19 nchini katika kipindi cha kuanzia tarehe 05 Mei hadi 03 Juni 2022 ambapo kipindi hicho, jumla ya maambukizi mapya 161 yamethibitika ikilinganishwa na maambukizi 68 kwa kipindi cha tarehe 02 Aprili hadi 4 Mei 2022.

Ongezeko hili ni sawa na asilimia 137, Aidha, katika kipindi cha miezi miwili mfululizo hakuna kifo kilichoripotiwa, halii hii inaashiria kuwa maambukizi yameanza kuongezeka katika jamii.

"Mchanganuo wa idadi ya waliothibitika katika kipindi cha tarehe 05 Mei hadi 03 Juni 2022 inaonesha kuwa Mkoa wa Dar es Salaam uliripoti maambukizi 130, Arusha (10), Mwanza (5), Shinyanga (4), Mtwara (3), Dodoma (2), Mara (2), Morogoro (1), Simiyu (1), Katavi (1), Kilimanjaro (1) na Mbeya (1), jumla ya wagonjwa watatu (3) waliothibitika kuwa na Covid-19 walilazwa na wote walikuwa hawajapata chanjo"

"Kwa takwimu hizi, inaonyesha kuwa, chanjo ni kinga dhidi ya madhara ya Covid - 19, Serikali imeendelea kutoa huduma za chanjo nchini ili kuwezesha wananchi kupata kinga dhidi ya ugonjwa huu"

"Kuanzia tarehe 05 Mei hadi 03 Juni 2022 jumla ya wananchi waliopata dozi kamili ya chanjo ya Covid 19 ni 775,680, Wizara inaendelea kuwasisitiza wananchi kupata na kukamilisha dozi za chanjo ili kuzuia kupata ugonjwa mkali hata kifo pale Mtu anapopata maambukizi" Mganga Mkuu wa Serikali Dr. Aifello Sichwale
Screenshot_20220608-033527_OGInsta%2B.jpg
 
Mbunge wa Mbogwe, Nicodemas Henry Maganga akichangia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 ameitaka Serikali kufungulia zaidi pesa ili hata wale Wanyonge wapate.

"Kweli tunasema hali sasa hivi ina unafuu lakini hali bado ni ngumu Waziri wa fedha angalia kama kuna sehemu yoyote fungulia pesa ili kusudi zifunguke hata kwa wanyonge zijae mifukoni maana kwenye kampeni huwa tunasema tunawapigania wanyonge sasa wanyonge hawajapata hela bado"

"Tunashukuru kwa jitihada mnazozifanya, tumeona kwa watumishi mmeongeza mishahara, watumishi wanafurahi lakini kuna wengine hawana nafasi ya kuingia kwenye manufaa haya, kwa hiyo ni vyema Waziri kwa kuwa wewe ni msomi mzuri jaribu kufikiria jinsi gani unaenda Taifa kulisaidia ili kila mtu apate haki yake" ——— Mbunge Nicodemus Maganga.
Screenshot_20220608-033916_OGInsta%2B.jpg
 
Jeshi la Polisi mkoani Kigoma limetaja majina tisa ya watuhumiwa waliokutwa na viungo vilivyodhaniwa kuwa vya binadamu katika taarifa iliyotolewa mnamo Juni 02, 2022 ikiwa viungo hivyo ni mbavu na mguu mmoja.

Majina hayo yalihifadhiwa kwa lengo la kuondoa hofu ya kuharibu upepelezi wa kesi hiyo iliyoanza kufanyiwa kazi Mei 30,2022 lakini sasa RPC Kigoma ACP James Manyama amewataja Watuhumiwa waliokuwa ndani ya gari aina ya Probox T948 DQU kuwa ni Miraji Nyambi (45) ambaye ni Mwalimu wa sekondari ya Mwandiga Kigoma, dereva wa gari hilo Thobias Fundo (33) mkulima kutoka Muyama wilayani Buhigwe pamoja na Mathayo Ndayishimiye (40) Mganga wa kienyeji kutoka Katue nchini Burundi.

Waliopatikana wakati wa upepelezi ni pamoja na Bankana Zakayo (41) mwalimu wa sekondary ya Mwandiga ambaye kwa sasa anaishi Nyehunge wilayani Sengerema, Ramadhan Abrahaman (52) mganga wa kienyeji kutoka Swaga mkoani Mwanza, Nguno Manyanza kutoka wilaya ya Geita na Kelvin Fedha mkazi wa Nyehunge.

Kamanda amewataja wengine kuwa ni Adizino John (62) mkazi wa Matiazo mkoani Kigoma, James Kibeba (68) kutoka Kasulu.

"Kaburi lilifukuliwa kuwa ni lla Bilihanyuma Suminda (90) aliyefatiki mnamo January 2022 wilayani katika kijiji cha Migongo wolayani Buhigwe, alifariki kwa marazi ya kawaida na kwa tukio hilo tumewashikilia jumla ya washitakiwa Tisa na tunakamilisha taratibu ili watuhumiwa waweze kufikishwa mahakamani."
Screenshot_20220608-034536_OGInsta%2B.jpg
 
Mbunge wa Ukonga Dar es salaam @JerrySilaa amesema kuna haja ya kero ya Watu kupata TIN namba kwenye Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ishughulikiwe haraka ili vitu vifanyike kama inavyotakiwa.

“Kumekuwa na kilio kirefu cha wafanyabiashara wanapoenda kutafuta TIN namba, Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) inataka kuwe na makadirio ya mapato na akipewa TIN namba ile anatakiwa robo ya kwanza alete marejesho anazitoa wapi na hajaanza biashara, hivi kuanza na assessment ya zero tunapata tatizo gani? ili mtu akianza biashara aje aseme mapato ndio aanze kulipa sasa unapompa mtu TIN namba leo na maskini ya Mungu inawezekana kastaafu au hana ajira kapata usajili unamwambia utaleta laki nne kwa mwaka na robo ya kwanza ulete laki moja anaitoa wapi? hiki ni kilio kikubwa kwa wajasiriamali na wafanyabiashara wa nchi hii, tunaomba sana Serikali iliangalie" ——— Mbunge wa Ukonga, Jerry Slaa akichangia mjadala wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023.
Screenshot_20220608-034905_OGInsta%2B.jpg
 
Mahakama ya Wilaya ya Iringa imemuhukumu kifungo cha mika 30 na fidia ya Tsh. Milioni 1 Mfanyabiashara Kaloli Mkusa (30) mkazi wa kijiji cha Msisina kwa kosa la kumbaka Mama yake Mzazi, hata hivyo Mtuhumiwa na Baba yake Joseph Mkusa ambaye alimuwekea dhamana wametoweka kusikojulikana na hati ya kukamatwa tayari imetolewa.

Akitoa Hukumu hiyo Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama hiyo Emmy Msangalufu amesema Mtuhumiwa alifanya tukio hilo May 07,2021 ambapo siku ya tukio Mtuhumiwa alikwenda nyumbani kwa Mama yake majira ya usiku na kuvunja mlango huku akiwa ameshika panga na kumtisha kumkata kwa kumpiga na ubapa wa upanga.

Licha ya Mama yake kumsihi asifanye hivyo lakini Mtuhumiwa aliendelea na kumbaka Mama yake mpaka alipomaliza, baada ya tukio Mama alitoa taarifa kwa majirani baadae Serikali ya Kijiji ndipo taratibu za kumkamata zikafanyika.

Tukio Hilo linasadikiwa ni kutokana na Imani za kushirikiana kutokana na biashara ya Mtuhumiwa kuyumba, Mtuhumiwa alikuwa akifanya biashara zake Tunduma Mkoani Songwe na alirudi akafikia kwa Baba yake ambaye anaishi nyumba tofauti na Mama yake kutokana na kupeana talaka.

Hata hivyo hati ya kukamatwa ilitolewa Tareh 09/03/2022 lakini mpaka Sasa Mtuhumiwa pamoja na Baba yake aliyemuwekea dhamani hawajulikani walipo, kwa mujibu wa Mahakama kifungo hicho kitaanza kutumika pindi Mtuhumiwa atakapokamatwa.
Screenshot_20220608-035016_OGInsta%2B.jpg
 
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Jokate Mwegelo akiwa ameambatana na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Elihuruma Mabelya na Kaimu Meneja wa TARURA, QS. Adelhard Kweyamba, wamefika eneo la Mwembeyanga ,ambapo unatarajiwa kutekelezwa mradi wa uboreshaji maeneo ya wazi kupitia Mradi wa Uendelezaji Jiji la Dar es Salaam(DMDP).

DC Jokate amesema amefurahishwa na ujio wa mradi huo wa uboreshaji uliopewa jina la 'Mwembeyanga Memorial Gardens and Sports Grounds' kwakuwa utakua fursa katika ukusanyaji mapato ya Manispaa na eneo la burudani kwa wakazi wa Temeke.

"Tumekuja hapa kwenye eneo maarufu lenye historia ya kipekee, Timu ya Yanga chimbuko lake ni hapa kwa ambao hawajui, hii ni fursa kwetu kuendeleza eneo na kuliweka katika hadhi, likiwa ni lengo la Serikali kuboresha maeneo yote ya wazi yaweze kutumika vizuri, Temeke kuna vipaji vingi, ukija hapa jioni utakuta vijana wanacheza mpira wa miguu, boxing, mazoezi ya viungo, tuna vipaji vinavyohitaji mazingira wezeshi, tutaboresha pia kwa ajili ya michezo ya Watoto wetu".

DC Jokate amesema uboreshaji wa eneo hilo ni utekelezaji wa maagizo ya Rais Samia na RC Amos Makalla "Katika kampeni ya Safisha Pendezesha DSM inaakisi matamanio ya Viongozi wetu kwamba ni lazima tusafishe na tupendezesha jiji letu, sio tu kwa kufagia bali kwa kuyafanya maeneo yaliyowazi kuendana na hadhi ya DSM"
Screenshot_20220608-035223_OGInsta%2B.jpg
 
Wizara ya TAMISEMI imetoa ufafanuzi kuhusu mapato ya jumla ya Stendi ya Magufuli ambapo imesema yameongezeka kutoka shilingi 7,165,100 hadi shilingi 8,244,100 kwa siku na sio Milioni 1 kama ilivyosomeka taarifa yake ya jana.

TAMISEMI imesema hili ni sawa na ongezeko la Shilingi 1,079,000 kwa siku na limetokana na ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Innocent Bashungwa alipofanya ziara yake Mei 30,2022 na kutoa maelekezo mahususi kuhusu uboreshaji wa mapato ya Stendi hiyo.

Maeneo yanaonekana kufanya vizuri ni viingilio vya Getini, ushuru wa choo pamoja na adhabu mbalimbali.

Wakati huo huo Ofisi ya Rais - TAMISEMI wameielekeza Manispaa hiyo kuboresha usimamizi na kuboresha huduma katika kituo hicho ili mapato yanapatikana yaende sambamba na huduma bora na usimamizi makini.
Screenshot_20220608-035334_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Fedha na Mipango Dr. Mwigulu Nchemba Bungeni leo amesema "Katika mwaka 2021/22, Bodi ya Michezo ya Kubahatisha ilipanga kutoa leseni 11,367 kwa waendesha michezo ya kubahatisha, ambapo kati ya hizo 7,408 ni leseni mpya na 3,959 ni leseni zitakazohuishwa na kufanya ukaguzi kwa waendesha michezo ya kubahatisha 76 waliosajiliwa ili kudhibiti uvunjifu wa sheria na taratibu"

"Hadi Aprili 2022, Bodi imefanikiwa kutoa jumla ya leseni 6,974, ambapo leseni 4,799 ni mpya na 2,175 zimehuishwa, vilevile Bodi imeweza kufanya ukaguzi kwa waendesha michezo ya kubahatisha 65 na kuunganisha mifumo ya michezo ya kubahatisha na mfumo wa GEPG, BRELA na mifumo ya Mamlaka ya Mapato Tanzania -TRA"

"Katika mwaka 2022/23, Bodi ya Michezo ya Kubahatisha inatarajia kutoa leseni 7,697 kwa waendesha michezo ya kubahatisha, ambapo 1,923 ni leseni mpya na 5,774 ni leseni zitakazohuishwa, kufanya ukaguzi kwa waendesha michezo ya kubahatisha 83; kufanya mapitio ya Sheria na Kanuni za Michezo ya kubahatisha; na kurejesha Bahati Nasibu ya Taifa"
Screenshot_20220608-035530_OGInsta%2B.jpg
 
Serbia na Urusi zimethibitisha kuwa ziara iliyopangwa ya Waziri wa mambo ya kigeni wa Urusi Sergei Lavrov katika nchi hiyo ya eneo la Balkan haitafanyika.

Tangazo hilo limefuatia ripoti kuwa nchi jirani na Serbia ambazo ni Bulgaria, Macedonia Kaskazini na Montenegro, zimekataa kuiruhusu ndege ya Lavrov kupita katika anga yao kwenda Serbia.

Urusi imekemea hatua hiyo huku Lavrov akisema katika kikao cha waandishi wa habari kuwa taifa huru limenyimwa haki yake ya kuendesha sera zake za kigeni.

Rais wa Serbia Aleksandar Vucic alikutana na Balozi wa Urusi nchini Serbia ambaye alimfahamisha kuwa Lavrov asingeweza kusafiri kwa sababu ndege yake ilinyimwa ruhusa za kupita kwenye anga za Umoja wa Ulaya na Jumuiya ya Kujihami ya NATO.
Screenshot_20220608-035706_OGInsta%2B.jpg
 
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Mtwara na TAKUKURU kuhakikisha wanafuatilia na kuwachukulia hatua baadhi ya Watumishi wa Mamlaka ya Mapato (TRA) Mkoani humo ambao wamekuwa sio waadilifu na kuwanyanyasa Wafanyabiashara kwa kuwafungia biashara zao.

Shaka ameyasema hayo katika kikao cha majumuisho ya ziara yake ya siku nne Mkoani Mtwara.

"Mkuu wa Mkoa huko TRA kuna mambo inabidi mkayaangaliee, Rais alipoingia madarakani jambo moja kubwa alilolifanya ni kufungua uchumi wa nchi, kuna biashara zilifungiwa Rais alipoingia zikafunguliwa"

"Kuna Watu wanafungia Watu biashara lakini TAKUKURU tusaidieni mkitaka tuwasaidie tutawapa baadhi ya Watumishi wa TRA vitendo wanavyofanya haviendani na maadili ya kazi zao"

"Kumekuwa na wimbi la kufunga biashara za Watu kwa makosa madogomadogo ambayo hayana msingi hatuwezi kuona dhamira njema ya Rais inakwamishwa baadhi ya Watu wanataka kumkwamisha Rais Samia"
Screenshot_20220608-035813_OGInsta%2B.jpg
 
Idadi ya vifo nchini Nigeria imepanda hadi Watu 100 kufuatia shambulizi la kikatili kwenye kanisa moja la Kikatoliki huku Watoto wengi na Wanawake wajawazito wakiwa miongoni mwa waliofariki.

Watu waliokuwa na silaha walilivamia Kanisa la Mtakatifu Francis katika mji wa Owo hapo jana, wakati wa ibada ya asubuhi na kuwafyatua risasi kiholela Waumini.

Serikali imeanzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo, makundi ya itikadi kali na ya uhalifu yamefanya mashambulizi mengi kwenye Makanisa katika upande wa kaskazini mwa Nigeria wenye wakaazi wengi Waislamu katika miaka ya karibuni.

Upande wa kusini wenye wakaazi wengi Wakristo haujashuhudia mashambulizi ya aina hiyo.
Screenshot_20220608-040000_OGInsta%2B.jpg
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi mkoani Kilimanjaro imeahirisha kesi ya uhujumu uchumi inayomkabilia aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wanne hadi Juni 20 mwaka huu.

Wakiwa mahakamani hapo leo, mawakili wa utetezi wameiomba mahakama kuahirisha kesi hiyo ili Sabaya apelekwe hospitali kutibiwa kutokana na kuwa na uvimbe kichwani.

Wakili Hellen Mahuna amemwambia Hakimu Mkazi Mfawidhi, Salome Mshasha kuwa mshtakiwa namba moja ambaye ni Sabaya ni mgonjwa na anatakiwa kwenda kufanyiwa upasuaji.

Amedai mshtakiwa huyo alipata uvimbe huo akiwa kazini, hivyo mawakili wanaomba kesi hiyo iahirishwe ili akafanyiwe upasuaji.
Screenshot_20220608-040200_OGInsta%2B.jpg
 
"Tumepokea wasifu wa makocha zaidi ya 100 kutoka sehemu mbalimbali duniani ambao wengi wao ni kutoka barani Ulaya na Amerika Kusini. Mchakato wa mchujo unaendelea na tunategemea utakamilika ndani ya wiki mbili zijazo.

Tunahitaji kocha anayejua vizuri soka la Afrika. Pia, tungefurahi kupata kocha ambaye ni mzawa wa bara hili lakini mpaka sasa bado hawajatuma wasifu, na aliyetuma ni mmoja na vigezo vyake havitoshi."- Mkurugenzi Mtendaji wa Simba SC, Barbara Gonzalez
Screenshot_20220608-040421_OGInsta%2B.jpg
 
Serikali imetoa msamaha wa malimbikizo ya riba iliyotozwa kwenye michango iliyocheleweshwa kulipwa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF).

Msamaha huo unahusu michango yote iliyocheleweshwa hadi Agosti 2021, na waajiri wanatakiwa kulipa madeni ya michango kabla ya Juni 30, 2022
Screenshot_20220608-040529_OGInsta%2B.jpg
 
Kama wewe ni shabiki wa Simba, basi zikufikie tu taarifa, mabosi wa klabu hiyo mezani kwao wana majina wanne ya viungo washambuliaji ambao mmoja wao atashushwa mambo yakikamilika ambaye ni Morlaye Sylla anayekipiga kwa sasa AC Horoya ya Guinea.

Sylla aliyewahi kucheza soka la kulipwa Ureno, ni moja kati ya machaguo matatu ya kwanza katika majina hayo manne na Mtendaji Mkuu wa klabu hiyo, Barbara Gonzalez amewatuliza mashabiki wa timu hiyo akiwaambia kuna mambo mazuri yapo njiani.

Chanzo makini kutoka ndani ya Simba, kimelidokeza Mwanaspoti, raia huyo wa Guinea anapigiwa hesabu na mabosi wa Simba kutokana na kumfuatilia kwa muda mrefu ili kumshusha Msimbazi, akiwa ni chaguo la tatu.

Kiwango anachoonyesha Sylla kwenye timu ya taifa pamoja na klabu yake ya Horoya kinatajwa ndicho kilichowavutia mabosi wa Simba na kuanza mchakato wa kumfuatilia kwa kutafuta taarifa zake mbalimbali.

Screenshot_20220608-040643_OGInsta%2B.jpg
 
YANGA inaendelea na mazoezi ya kujiandaa na mechi za kumalizia msimu wa Ligi Kuu Bara pamoja na pambano lao na fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC), huku kocha wao Nasreddine Nabi aliyetimkia kwao kwa mapumziko mafupi amemtumia salamu nzito mshambuliaji wake kutoka DR Congo, akimpa dili moja gumu la dakika 360.

Mshambuliaji aliyepewa masharti hayo na kutakiwa kurekebisha mambo ili mambo yamnyookee Jangwani ni Chico Ushindi, ambaye bado hajasomeka vyema kwa mashabiki tangu asajiliwe kutoka TP Mazembe kupitia dirisha dogo la usajili akipishana na Mukoko Tonombe.
Akizungumza na Mwanaspoti, Kocha Nabi alisema bado anaumizwa kichwa na Ushindi ambaye hajafanikiwa kuwasha moto walioutarajia wakati wanamchukua kwa mkopo kutoka Mazembe.
“Sijaanza kumjua Ushindi hapa Yanga, namjua muda mrefu lakini kuna maisha aliyapitia Mazembe ambayo yanatupa shida kuweza kuona kile alichonacho, unapomwona mazoezini ni tofauti na kwenye mechi,” alisema Nabi na kuongeza;

“Angalau mechi ya mwisho aliyocheza pale Mwanza kuna kitu kidogo alifanya, lakini kitu kibaya tunaelekea mwisho wa msimu, nafikiria kumpa hizi mechi zilizobaki kama ataweza kurudisha ubora wake.”

Ushindi alisajiliwa kwa mkataba wa miezi sita inayomalizika mwishoni mwa msimu huu, huku akiwa hajafunga bao lolote kwenye michuano hiyo ya Ligi na ASFC, lakini kocha Nabi alisema kuna vitu ameviona kwenye miguu yake katika mechi chache alizomtumia.
Screenshot_20220608-040754_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom