Makapuku Forum

Makapuku Forum

MORRISON NDO BASI TENA MSIMBAZI
.
Za Ndani Kabisa: Inaelezwa Uongozi wa Simba umepanga kupitisha panga kubwa katika kikosi chake cha sasa na awali vigogo wa klabu hiyo waligawanyika ambapo wapo waliotaka winga mtukutu, Bernard Morrison abakie na wengine aondoke lakini mwenendo usioridhisha wa nidhamu yake, umewafanya vigogo wa Simba waamue kutomuongezea mkataba mpya, hivyo Morrison Anaondoka Simba.
.
Screenshot_20220513-085807_OGInsta%2B.jpg
 
SAIDO BADO HAKIJAELEWEKA !!
.
Yanga imeanza kuwaongeza mikataba wachezaji wake lakini hatima ya nyota wake Said Ntibanzokiza ‘Saido’ kubaki au kuondoka kikosini hapo haijafikiwa.
.
Saido (36) mkataba wake umefika tamati mwezi huu lakini licha ya mazungumzo kuhusu hatima yake ndani ya chama hilo kufanyika baina ya pande zote mbili kwa zaidi ya mara tatu lakini inashindwa kumalizika kutokana na kuwa na malumbano ya hoja kati ya viongozi wa Yanga wakiwepo wanaotaka nyota huyo abaki na wengine wakitaka aondoke na kusajili mashine nyingine.
.
Taarifa zinaeleza kuwa uhusiano wa Saido na wadhamini GSM ni kati ya mambo yanayoweza kumbakiza Jangwani.
Screenshot_20220513-085907_OGInsta%2B.jpg
 
PIGO: LUIS MIQUISSONE NJE MWEZI MZIMA
.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika klabu ya Al Ahly, imethibitisha kwamba winga Luis Miquissone atakuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha mwezi mmoja baada ya kusumbuliwa na maumivu ya misuli ya nyuma ya paja.
.
Luis anatajwa kuwa mbioni kurejea kwa mkopo katika klabu yake ya zamani ya Simba SC.
Screenshot_20220513-085958_OGInsta%2B.jpg
 
Baadhi ya Watuhumiwa Vijana kutoka kwenye Kundi la Panya road wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala Kinyerezi jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za unyang'anyi wa kutumia silaha (mapanga).

Mtuhumiwa wa kwanza Daud Abdallah miaka 22, mzaramo, dereva na mkazi wa Tungini na wenzake 16 walifikishwa mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Fadhili Luvinga kusomewa mashtaka nane yanayowakabili.

Waendesha Mashtaka, Mawakili wa Serikali Michael Ng'hoboko, Avelina Ombock na Nancy Mushumbusi walidai kuwa Watuhumiwa kwa pamoja walitenda makosa hayo tarehe 24/04/2022 maeneo ya Chanika Ilala jijini Dar es Salaam na bado wengine wanatafutwa.

Waendesha Mashtaka wamedai kuwa upelelezi wa shauri hilo umekamilika na waliomba tarehe kwa ajili ya kusikiliza hoja za awali ambapo hata hivyo Watuhumiwa wote walikana mashtaka yao na kesi ikaahirishwa mpaka tarehe 27/5/2022 huku Watuhumiwa hao wakipelekwa rumande kutokana na makosa waliyoshtakiwa nayo kutokuwa na dhamana.
Screenshot_20220514-041515_OGInsta%2B.jpg
 
Chuo kimoja katika jimbo la Sokoto kaskazini magharibi mwa Nigeria kimefungwa kwa muda usiojulikana baada ya Mwanafunzi wa kike chuoni hapo kuuawa kwa madai ya kukufuru dini ya kiislamu.

Mwanafunzi huyo ambaye jina lake halijatajwa alishtakiwa kwa kumtusi Mtume Muhammad jambo ambalo lilisababisha baadhi ya Wanafunzi waislamu kumshambulia na kumchoma moto na kusababisha kifo chake ndani ya eneo la Chuo jana alhamisi.

Gavana wa jimbo la Sokoto Aminu Tambuwal aliamuru kufungwa kwa chuo hicho na kuagiza Wizara ya elimu ya juu na Vyombo husika vya usalama kuchunguza tukio hilo na kuwataka Watu wa jimbo hilo kuwa watulivu na kudumisha amani kwani Serikali itachukua hatua zinazofaa kuhusu matokeo ya uchunguzi.
Screenshot_20220514-041715_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa amezindua shamba la bangi kwa ajili ya dawa lenye thamani ya dola za kimarekani milioni 27.

Shamba hilo limewekewa kiwanda cha kisasa cha usindikaji ambacho bangi yake itatumika kama suluhisho la matibabu ya kibaiologia na bidhaa za dawa katika soko la ndani na la kimataifa ambapo mradi huu ni kwa ushirikiano na Serikali ya Uswizi kupitia kiwanda cha Swiss Bioceuticals na Serikali ya Zimbabwe.

Rais Mnagangwa amesema kuwa ushirikiano huo unaonyesha imani ya Uswizi katika kuwekeza ndani ya uchumi wa Zimbabwe huku akisema kuwa taifa hilo la Ulaya tayari limeshirikiana na Zimbambwe katika miradi mingine kama vile viwanda, usindikaji wa chakula na ujenzi wa taasisi.
Screenshot_20220514-042018_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali Mwinyi leo amekutana na kufanya mazungumzo na Raia saba kutoka Oman @dream_team_explorers waliopata mwaliko wa kutembelea Vivutio vya Zanzibar chini Wizara ya Utalii kupitia Kamisheni ya Utalii Zanzibar.

Itakumbukwa December 2020, Raia wawili kati ya Raia hao saba waliwahi kuitembelea Tanzania kwa kutumia gari kutoka Oman hadi Tanzania kwa kupita nchi tisa na sasa wamekamilisha nchi 10 kwa kuitembelea Tanzania.

“Nichukue fursa hii kuwashukuruni kwa utayari wenu kwa kufanya kazi na sisi kuongeza Watilii wanaokuja Tanzania kutoka Oman kuja kwao itatusaidia sana” Rais Mwinyi.
Screenshot_20220514-042141_OGInsta%2B.jpg
 
Mechi ya Namungo FC dhidi ya Mbeya Kwanza imeshindwa kuchezwa katika uwanja wa Ilulu Lindi, baada ya Mbeya Kwanza kugoma kuanza kwa Mechi hiyo kutokana na kutokuwepo kwa gari la kubebea wagonjwa (Ambulance) kama kanuni zinavyotaka uwepo wa gari hilo na Wataalamu wa huduma ya kwanza.

Baada ya mgomo huo gari la wagonjwa likaletwa saa 10:23 jioni wakati mechi ilikuwa ianze saa 10:00 jioni, Timu zimeondoka uwanjani na sasa yanasubiriwa maamuzi ya Mamlaka za Soka nchini.
Screenshot_20220514-042239_OGInsta%2B.jpg
 
Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Justine Masejo kwa niaba ya Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania amesema Polisi wameanzisha kitengo maalumu cha Utalii na Diplomasia ambacho kipo kwa ajili ya kuwahudumia Watalii na Wanadiplomasia wanaofika Tanzania, hii ni baada ya Rais Samia kuzindua filamu ya Royal Tour.

Kamanda Masejo amesema kwa Mkoa wa Arusha ambao ni kitovu cha utalii nchini kumeanzishwa kituo cha Polisi maalumu kwa ajili ya kuhudumia Watalii na Wanadiplomasia ambapo Askari wake wamepatiwa mafunzo ndani na nje ya Nchi kuhusu namna bora ya kuhudumia Watalii.

Pia amesema kuwa kuna magari maalumu ambayo hutumiwa na kituo hicho kwa ajili ya doria mbalimbali ikiwemo kwenye vivutio vya utalii, hoteli za kitalii pamoja na maeneo mengine ambayo wageni hupenda kutembelea ambapo sambamba na hilo kuna vituo vidogo vya Polisi vilivyopo katika Wilaya ya Arumeru, Monduli, Longido na Karatu ambapo magari ya utalii hufika kwa ajili ya kupata taarifa za kitalii pamoja na ukaguzi wa usalama wa magari hayo "Jeshi la Polisi litaendelea kumuunga mkono Rais wa Samia katika kuutangaza utalii kwa kuboresha mazingira ya kiusalama kwa Watalii"
Screenshot_20220514-042402_OGInsta%2B.jpg
 
Simba SC. imesema imempa mapumziko ya hadi mwisho wa msimu Mchezaji wake Bernard Morrison baada ya pande zote mbili kukubaliana apumzike ili ashughulikie mambo yake binafsi.

“Simba inamshukuru Morrison kwa mchango wake kwa kipindi chote alichohudumu ndani ya Klabu yetu, tunatambua mchango wa Morrison miaka miwili aliyoitumikia Club, Simba inamtakia kila la kheri Morrison katika mapumziko yake na safari yake ya soka hapo baadae” ——— Simba SC.
Screenshot_20220514-042517_OGInsta%2B.jpg
 
Wazazi nchini India wamewasilisha kesi Mahakamani dhidi ya Mtoto wao wa kiume na Mke wake baada ya kukaa kwenye ndoa kwa miaka 6 bila kuwapatia Mjukuu.

Sanjeev na Sadhana Prasad wanadai ‘manyanyaso ya akili’ kwani inadaiwa walitumia akiba yao yote kwaajili ya malezi ya mtoto wao ila bado yeye na mke wake hawawapatii mjukuu wa kucheza nao katika mda wao wa kustaafu na sasa wanadai walipwe fidia ya karibu $650,000 (Tsh. Bilioni 1.5) ikiwa Wanandoa hao hawatazaa ndani ya mwaka mmoja ujao.

Prasad anadai $65,000 zilitumika kumpeleka mtoto wao Marekani mwaka 2006 ili apate leseni yake ya urubani…. limeandika gazeti la The Times of India kwamba alirudi India mwaka uliofuata na kupoteza kazi yake lakini Wazazi hawa walimsaidia kifedha kwa miaka miwili iliyofuata hadi alipopata kazi tena.

Mwaka 2016 Wazazi hawa waliandaa ndoa yake na Shubhangi Sinha na kulipia gharama kadhaa kama sherehe nzima ya harusi, gari la kifahari la $80,000 (Tsh. milioni 185) na honeymoon yao na sasa ikiwa ni miaka sita imepita Wazazi hawa wanataka kurudisha pesa wanazoamini kuwa zilipotea bila Mjukuu kuonekana ambapo Mahakama inatarajia kusikiliza kesi yao baadaye mwezi huu.
Screenshot_20220514-042654_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu (U.A.E) Sheikh Khalifa bin Zayed Al Nahyan amefariki, shirika la habari la Imarati WAM limeripoti muda mfupi uliopita na kusema amefariki akiwa na umri wa miaka 73.

"Wizara ya Masuala ya Rais ilitangaza kuwa kutakuwa na siku 40 za maombolezo rasmi na bendera nusu mlingoti na siku tatu kufungwa kwa Wizara na Mashirika rasmi katika ngazi ya shirikisho na Serikali za mitaa na sekta ya kibinafsi” taarifa imeeleza.

Sheikh Khalifa ambaye amekuwa akiugua kwa miaka kadhaa kulikosababisha kwa muda mrefu aache kujihusisha na shughuli za kila siku alimuachia mikoba kaka yake ambaye ni Mwanamfalme wa Abu Dhabi Mohammed bin Zayed ambaye ndiye ameonekana kama Mtawala kwa muda huo.

Sheikh Khalifa ambaye ni nadra kuonekana kwenye picha rasmi au kwenye hafla za umma kwa miaka mingi, alimrithi Baba yake na Mwanzilishi wa UAE Sheikh Zayed mnamo mwaka 2004, alipata kiharusi muongo mmoja baadaye na kumweka mbali na Watu tangu wakati huo.
Screenshot_20220514-042822_OGInsta%2B.jpg
 
"Kuna tatizo kubwa la ubakaji si Zanzibar tu hata vitoto vinabakwa vya kike na vya kiume lakini sauti haijaja juu sana kwenye hili kama ambavyo mmekua mkitetea haki za wanasiasa,"Rais Samia.
Screenshot_20220514-042952_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba, amesema kuwa Serikali itawasiliana na Mamlaka za Kenya ili kutatua changamoto ya malori yanayopeleka bidhaa nchini humo kutumia muda mrefu kupata vibali vya kuvuka mpaka wa Horohoro-kuingia Kenya.
Screenshot_20220514-043050_OGInsta%2B.jpg
 
Elon Musk amesema leo Ijumaa kuwa amesimamisha kwa muda mpango wake unaosubiriwa kwa hamu wa kuinunua Twitter, na kusababisha thamani ya hisa za mtandao huo mkubwa wa kijamii kuporomoka.

"Mpango wa Twitter kwa muda umesimama kutegemea taarifa za mahesabu kwamba akaunti hewa au za kughushi zinawakilisha chini ya asilimia 5 ya watumiaji," ameandika katika akaunti yake ya Twitter.
Screenshot_20220514-043151_OGInsta%2B.jpg
 
Shirika la ndege la Tanzania (ATCL) na kampuni ya Marekani ya kutengeneza ndege ya Boeing wameingia mkataba wa makubaliano ya kushirikiana katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyakazi wake ili kuleta tija zaidi katika biashara.

Hii ni mara ya kwanza kwa kampuni hiyo kubwa ya kimataifa ya utengenezaji wa ndege kuingia mkataba wa namna hiyo na mteja wake.

Akizungumza wakati wa utiaji saini mkataba huo murugenzi mkuu wa ATCL, Ladislaus Matindi amesema mafunzo yatakayoanza hivi karibuni yatawalenga mameneja wakuu, mameneja wa kati na wasimamizi
Screenshot_20220514-043310_OGInsta%2B.jpg
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imepanga Mei 23, 2022 kutoa uamuzi wa kesi ya aliyekuwa
Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu nchini Tanzania (CWT), Deus Seif na Mwekahazina wa chama hicho, Abubakari Allawi kama wanakesi ya kujibu au la.

Seif na Allawi wakabiliwa na mashtaka mawili likiwemo la kutumia madaraka yao vibaya kwa kuchepusha fedha kiasi cha Sh 13.9milioni ambacho ni mali ya CWT.

Washtakiwa hao wanadaiwa kutumia fedha hizo kwa ajili ya safari ya ndege kwenda Cape Verde, kuangalia mpira wa miguu, kati ya Taifa Stars na timu ya Cape Verde, kinyume cha sheria.

Uamuzi huo umetolewa leo, Mei 13, 2022 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Richard Kabate, baada ya upande wa mashtaka kufunga ushahidi wao mashahidi 9 na vielelezo 11, walivyotoa mahakamani hapo dhidi ya washtakiwa .

" Upande wa mashtaka wamefunga ushahidi wao hivyo nahitaji muda kidogo ili niweze kupitia na kuja kutoa uamuzi, hivyo Mei 23, kesi hii itakuja kwa ajili ya kutoa uamuzi" Amesema Hakimu Kabate.

Kabla ya kuahirishwa kwa kesi hiyo upande wa mashtaka ukiongozwa na Iman Nitume akishirikiana na Veronica Chimwada, walikuwa na shahidi mmoja, Faustine Mashauri, ambaye ni Mtaalamu wa Maandishi kutoka Jeshi la Polisi.

" Mheshimiwa hakimu baada ya shahidi wetu huyu( Faustine) kumaliza kutoa ushahidi wake leo, naomba kuieleza mahakama kuwa upande wa mashtaka tumefunga ushahidi wetu" amedai wakili Nitume.

Nitume baada ya kueleza hayo, hakimu Kabate aliahirisha kesi hiyo hadi Mei 23, 2022 itakapoitwa kwa ajili ya mahakama kutoa uamuzi.

Katika kesi ya msingi, Seif na Allawi, wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 39/2021.
Screenshot_20220514-043417_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia Suluhu Hassan akipokea ujumbe maalumu kutoka kwa Rais wa Rwanda, Paul Kagame uliowasilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje Rwanda, Vincent Biruta Ikulu jijini Dar es Salaam leo Ijumaa Mei 13, 2022.
Screenshot_20220514-043528_OGInsta%2B.jpg
 
Chama cha Soka Ulaya (Uefa) kimetangaza mfumo mpya wa mashindano yake yote matatu, huku kikisema kuwa mradi wa kuanzisha Super League sasa umezikwa "kwa angalau miaka 20".

Baada ya kikao cha mkutano mkuu uliofanyika jijini Vienna, Australia jana, rais wa Uefa, Aleksander Ceferin alisema baada ya mashauriano ya muda mrefu hatimaye wamefikia uamuzi wa kupanua mashindano hayo matatu kwa kuongeza timu nne na kuondoa hatua ya makundi na kwamba mfumo huo utaanza msimu wa mwaka 2024/25.

Uamuzi huo wa mkutano mkuu ni mwendelezo wa uamuzi uliofanyika Aprili 19 wa kuanzisha mfumo unaoitwa “Swiss system”.

Mabadiliko makubwa katika mfumo huo ni kupunguza idadi ya mechi kutoka 10 hadi nane katika hatua ya ligi ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya na kubadili vigezo vya kutoa nafasi mbili kati ya nne za nyongeza za kucheza ligi hiyo kubwa.
Screenshot_20220514-043625_OGInsta%2B.jpg
 
Shaffih Dauda

Taarifa zilizonifikia hivi punde ni kwamba, Pamba SC imemfuta kazi Kocha Mkuu @MwetaWillibert

Baada ya kupewa taarifa za kufutwa kazi, Kocha Mweta alifika kambini kuwapa taarifa wachezaji kwamba kesho hatakuwa sehemu ya benchi la ufundi wakati Pamba itakapokuwa ikicheza dhidi ya Simba kwenye mchezo wa Azam Sports Federation Cup.

Bado sababu za kufutwa kazi kwa Kocha Mweta hazijawekwa wazi hadi sasa.
Screenshot_20220514-044105_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom