Makapuku Forum

Makapuku Forum

Farhan Jr

Washikaji zangu huwa wananiuliza sana kwanini NEYMAR JR ndie Mchezaji wako bora wa muda wote?

Jibu langu jepesi huwa ni SIMPLICITY!

Hata wanaponiuliza kwa Simba nani huwa unaenjoy kumtazama?? Huwa nawaambia ni RALLY BWALYA, wakiuliza kwanini huwa nawaambia ni SIMPLICITY!

Napenda sana wachezaji wanaofanya mpira uwe kitanda kizuri cha hotel ya five star, uchezaji wao ni kama nipo na Miss Tanzania, Millen Happy Magese

If football is an art, then Bwalya is the artist! SIMPLICITY IS THE KEY
Screenshot_20220512-062224_OGInsta%2B.jpg
 
Imeandikwa na @swalehmawele

FT: Simba SC 2-0 Kagera Sugar

Ilikuwa ni mechi ya Simba na walifanikiwa kuimaliza katika dakika 45 za kipindi cha kwanza, wali-dominate ( kumiliki ) kwa dakika nyingi zaidi, walitengeneza nafasi nyingi zaidi tatizo likawa katika usahihi tu wa matumizi ya nafasi, nyingi zilipotea kuliko walizozitumia.

Kitu kimoja tu kwa Kagera, walikosa quality ya kuonyesha madhaifu ya Simba hasa baada ya kipindi cha pili kuanza, Simba hawakucheza katika spidi ileile ya kipindi cha kwanza, walikuwa taratibu, hawakulazimisha matukio kutokea, kama unacheza vile dhidi ya timu yenye quality unajiweka katika mazingira ya kudondosha alama.

Kagera waliwatega Simba kwenye counter pressing, walianza kuwakabia kwenye eneo lao, Simba walifanikiwa kuutegua mtego, wakafika kwenye zone ya mwisho mara nyingi, Rally Bwalya kama kiungo wa kati mshambuliaji ( CAM ), alikuwa free kushuka chini ili kuweka link up kwenye eneo la mwisho.

Pablo Franco alifanya home work yake vizuri, alifahamu ubora wa Kagera wanapokuwa na mpira, kitu alichokifanya ni kuziwinda space ambazo wataziacha baada ya timu kusogea juu, wawaache wacheze kwenye zone yao ila wanapovuka mstari wa kati wa-press kisha wapige pasi za haraka wakati ambao mtego wao wa ukabaji ( defensive patterns ) umetawanyika.

Dickson Mhilu na Abdallah Seseme, wow, kwangu nikiambiwa nichague man of the match upande wa Kagera nitamchagua mmoja kati yao.

Rally Bwalya, alikuwa na mchezo mzuri hasa katika kipindi cha kwanza, leo aliyamudu vyema majukumu ya kiungo wa kati mshambuliaji.

Kibu Dennis, aongeze utulivu na umakini, atakuwa mchezaji mzuri sana.
Henock Inonga, eh! kama juzi kama jana, alicheza vyema katika eneo la kiungo.
Screenshot_20220512-062445_OGInsta%2B.jpg
 
Baraza Kuu la CHADEMA chini ya Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe leo Alhamisi limezitupilia mbali rufaa za Halima Mdee na wenzake 18 za kupinga kufukuzwa uanachama na Kamati Kuu ya Chama hicho.
Screenshot_20220512-062943_OGInsta%2B.jpg
 
Mbunge Halima Mdee kwa niaba ya wenzake 18 ameelezea kutokubaliana na uamuzi wa Baraza Kuu la CHADEMA chini ya Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe wa kutupilia mbali rufaa zao za kupinga kufukuzwa uanachama na Kamati Kuu ya Chama hicho akisema kilichofanyika ni uhuni.

"Nakwepa kuzungumza maneno makali kwasababu naheshimu Viongozi wangu lakini sikujua CHADEMA umeanza kufanyika uhuni kwa kiwango hicho, Mimi ni CHADEMA naendelea kuwa CHADEMA lakini kilichofanyika pale uhuni wa kiwango cha hatari , nitaongea siku nyingine lakini kilichofanyika pale hata Mbowe anajua ni uhuni"
Screenshot_20220512-063045_OGInsta%2B.jpg
 
Baada ya Mbunge Halima Mdee kwa niaba ya wenzake 18 kutokubalina na uamuzi wa Baraza Kuu la CHADEMA chini ya Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe wa kutupilia mbali rufaa zao za kupinga kufukuzwa uanachama na Kamati Kuu ya Chama hicho akisema kilichofanyika ni uhuni, Mbowe amemjibu na kuwaambia wao ndio waache uhuni.

“Nimesikitika hatujafurahia hali hiyo ila imebidi, maamuzi ya kuwafukuza yalifanyika tangu mwaka juzi kwenye kikao cha Kamati Kuu, kura zimepigwa mbele yao waache mambo ya kihuni”
Screenshot_20220512-063138_OGInsta%2B.jpg
 
Baraza Kuu la CHADEMA chini ya Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe leo Alhamisi limezitupilia mbali rufaa za Halima Mdee na wenzake 18 za kupinga kufukuzwa uanachama na Kamati Kuu ya Chama hicho.
View attachment 2221205
Hii kesi ya kina mdee ilijulikana mapema labda muda ndio ulikuwa bado na haina utofauti na ya jpm na membe kilicho tokea ndani ya CCM

Huwezi kuamua tofauti na maamzi yako ya awali


Huwezi kutuhumiwa ukampa mtuhumiwa Uhuru wa kushinda

Huwezi kuwa mwenyekiti ukawa mtuhumiwa ukawa jaji ukawa kiongozi wahesabu matokeo ukahesabu maumivu kwako

Kinacho tumaliza kwenye siasa ni katiba zinazo ishi nyumbn kwa viongozi wetu
 
- Awali kabla ya mabadiliko ya ratiba mechi hii ilipangwa kupigwa JUNI MOSI, ndio ratiba ambayo wamiliki wa uwanja wa Jamhuri walikuwa nayo

-Ila baada ya mabadiliko klabu ilifikisha taarifa kwa Meneja wa uwanja wa Jamhuri, alipaswa yeye kuandikia mechi ya Dodoma vs Yanga itapigwa MEI 15, bahati mbaya hakufikisha taarifa hiyo

- Hii ilipelekea Wamiliki kukodisha uwanja kwa matumizi mengine ya kiserikali ambapo kuna Wizara ina shughuli yake hapo, MEI 16!

Harakati zinaendelea ila iwapo wakikwama basi viwanja vingine viwili vya DODOMA JIJI ambavyo waliviandika kuweza kuvitumia ni JAMHURI, MOROGORO na SAMORA, IRINGA

-Taarifa nilizonazo ni kuwa uwezekano mkubwa mechi itapigwa SAMORA, IRINGA

-Ila harakati za kupambania mechi kupigwa Dodoma zinaendelea, TUTAJUZANA ZAIDI kwakuwa vikao bado vinaendelea Dodoma kati ya DJFC, Yanga, TPLB, Wamiliki wa uwanja na Wizara
Screenshot_20220513-085648_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom