Imeandikwa na @swalehmawele
FT: Simba SC 2-0 Kagera Sugar

Ilikuwa ni mechi ya Simba na walifanikiwa kuimaliza katika dakika 45 za kipindi cha kwanza, wali-dominate ( kumiliki ) kwa dakika nyingi zaidi, walitengeneza nafasi nyingi zaidi tatizo likawa katika usahihi tu wa matumizi ya nafasi, nyingi zilipotea kuliko walizozitumia.

Kitu kimoja tu kwa Kagera, walikosa quality ya kuonyesha madhaifu ya Simba hasa baada ya kipindi cha pili kuanza, Simba hawakucheza katika spidi ileile ya kipindi cha kwanza, walikuwa taratibu, hawakulazimisha matukio kutokea, kama unacheza vile dhidi ya timu yenye quality unajiweka katika mazingira ya kudondosha alama.

Kagera waliwatega Simba kwenye counter pressing, walianza kuwakabia kwenye eneo lao, Simba walifanikiwa kuutegua mtego, wakafika kwenye zone ya mwisho mara nyingi, Rally Bwalya kama kiungo wa kati mshambuliaji ( CAM ), alikuwa free kushuka chini ili kuweka link up kwenye eneo la mwisho.

Pablo Franco alifanya home work yake vizuri, alifahamu ubora wa Kagera wanapokuwa na mpira, kitu alichokifanya ni kuziwinda space ambazo wataziacha baada ya timu kusogea juu, wawaache wacheze kwenye zone yao ila wanapovuka mstari wa kati wa-press kisha wapige pasi za haraka wakati ambao mtego wao wa ukabaji ( defensive patterns ) umetawanyika.

Dickson Mhilu na Abdallah Seseme, wow, kwangu nikiambiwa nichague man of the match upande wa Kagera nitamchagua mmoja kati yao.

Rally Bwalya, alikuwa na mchezo mzuri hasa katika kipindi cha kwanza, leo aliyamudu vyema majukumu ya kiungo wa kati mshambuliaji.

Kibu Dennis, aongeze utulivu na umakini, atakuwa mchezaji mzuri sana.

Henock Inonga, eh! kama juzi kama jana, alicheza vyema katika eneo la kiungo.