Makapuku Forum

Makapuku Forum

THE ITALIAN JOB

Alipishana na Inter Milan juu ya sera za usajili, hakuwa tayari kushuhudia nyota kadhaa wakubwa wakiondoka, akaamua kuondoka kwakuwa hapendi kuwa sehemu ya kufeli

Akaichukua Tottenham ikiwa chini sana, akaipika anavyotaka na kuongeza majembe kadhaa, kwasasa wapo top five wanapambania nafasi ya kushiriki UEFA

Anataka fungu majira ya kiangazi, tusubiri atamleta nani na nani

Anaitwa ANTONIO CONTE
Screenshot_20220514-044317_OGInsta%2B.jpg
 
EPL: Wanaowania tuzo ya Mchezaji Bora wa Msimu:
.
Trent Alexander-Arnold
Mo Salah
Kevin De Bruyne
João Cancelo
️ Heung Min Son
Bukayo Saka
James Ward-Prowse
Jarrod Bowen
.
Nani anastahili __?
Screenshot_20220514-044905_OGInsta%2B.jpg
 
Klabu ya Manchester City imezindua sanamu la aliyekuwa mchezaji wao Sergio Kun Aguero nje ya uwanja wa Etihad ikiwa ni kumbukumbu ya miaka 10 ya bao lake la dakika za mwisho dhidi ya QPR lililoipa taji timu hiyo mnamo Mei 13, 2012.

Aguero ndani ya miaka kumi ndani ya Man City
Mechi-390
Mabao-260
Assist- 73.
Screenshot_20220514-045101_OGInsta%2B.jpg
 
Winga Bernard Morrison amefunguka baada ya kusimamishwa Simba hadi mwisho wa msimu; "Kwa moyo mzito natangaza kuwa nitakuwa nje hadi mwisho wa msimu kwasababu ya masuala ya kifamilia ambayo huenda yangeathiri kiwango changu ndani ya timu. Kuna mengi ya kusema ila kwenye hili ila niitakie kheri katika mechi zetu zilizobaki. Naimani na naomba yaishe mapema zaidi ili nijiunge tena na timu"

Baada ya kuandika ujumbe huo kwenye akaunti yake ya Instagram aliweka hashtag za Simba 'One team, One dream, nguvu moja' ambazo Mtendaji Mkuu, Barbara Gonzalez alizitumia katika sehemu ya kutoa maoni (comment) kwenye ukurasa wa Morrison.

Screenshot_20220514-045159_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom