Makapuku Forum

Makapuku Forum

Florentin Perez ameshinda mataji 50 akiwa Rais wa Real Madrid

Kuna Marais wa mpira kisha kuna Don Perez
Screenshot_20220430-214127_OGInsta%2B.jpg
 
Mwaleh Mawele

Nafikiri wengi tunakubaliana kuwa Thadeo Lwanga ni kiungo mzuri mkabaji ( defensive midfielder ), nadhani wote tunajua alikuwa na umuhimu gani ndani ya kikosi kabla hajaanza kusumbuliwa na majeraha.

Tumtazame Pablo Franco kisha tumuangalie na Thadeo, mwamba yupo fiti, unapotaja kiungo wa ulinzi katika kikosi cha Simba hakuna anaefikia ubora wa Thadeo, nadhani anafurahia zaidi kuzuia anapokuwa ndani ya kiwanja.

Kwenye double pivot ya Simba katika system ya 4-2-3-1 yupo Jonas Mkude na Sadii Kanoute, Mkude anacheza kama holding midfielder na Sadio anacheza kama box to box midfielder.

Thadeo si mzuri akicheza kama box to box midfielder kutokana na uwezo wake mdogo wa kupiga pasi za mbele ( forward pass ) na kukokota mpira kuitafuta space ( dribbling ), kwa maana nyengine ni rahisi kwa Thadeo kuchukua namba kwa Mkude kuliko Sadio.

Mkude si mzuri sana katika kukaba kama utamlinganisha na Thadeo, Mkude ni passer, anaweza kupiga pasi tatu za mita 40 na zote zikafika, hapa tu ndipo anakuwa muhimu katika kikosi cha Pablo, kupiga pasi ndefu zinazoiharakisha timu kwenda katika zone ya mwisho.

Siamini kama Thadeo ni mchezaji mbaya lakini Jonas Mkude anatoa kitu extra, uzuri ni kwamba timu haipo kwenye risk kwa sababu anapewa bima ya kukabiwa eneo kubwa na Sadio ambae anafanya mikimbio baina ya maboksi mawili.

Kama mambo yataendelea kubaki hivi inawezekana huu ukawa ni msimu wa mwisho wa Thadeo ndani ya jezi ya Simba, bado ana sehemu ya kuweza kuisaidia timu lakini hapa kwetu hatuamini kama inafaa kuwa na mchezaji wa aina yake katika benchi.

Acha tuone movie inavyokwenda.
Screenshot_20220430-215628_OGInsta%2B.jpg
 
Ali kamwe

Mambo 10 nilioyaona YANGA vs SIMBA

1: DAKIKA 180 za KARIAKOO DERBY BILA BAO, KWENYE LIGI MSIMU HUU. Ni Derby iliyotunyima Bao Lakini imetupa Jibu la Ubingwa wa NBC PREMIER LEAGUE.. Yanga watasherehekea Kombe lao, Simba watabaki na Heshima yao

2: Tactically, Makocha wote walikuwa na wasiwasi kwenye mipango yao. Ni kama waliwaza zaidi hatima zao baadae kuliko pointi 3 mbele ya Mtani .. Kivipi?

3: Timu zote zilikwenda na mfumo wa 4-2-3-1 Lakini Tofauti ikawa kwenye utekelezaji tu. Yanga wakaseti mtego wao kwenye Counter Attack.. Simba wakatafuta pasi mpenyezo nyuma ya ukuta wa Dickson Job na Mwamnyeto.. Wapi walifeli?

4: Moloko hakuwa kwenye Form yake. Hakuweza kutumia faida ya Mayele kusimama katikati ya Henock na Onyango.. Simba walikosa 'Movements' za Mugalu ili kutengeneza nafasi kwenye 'Half Spaces' ili Sakho na Morrison kutumia

5: Kuna funzo Henock na Onyango wamelitoa kwa mabeki wengine jinsi ya kudeal na Mayele. Kivipi? Jinsi ya kuziba nafasi ya nyuma ya mwenzako.. Asilimia kubwa Mayele alijikuta anafanya 'mikimbio' yake katikati ya Mabeki wawili wa Simba.. Ikapunguza kabisa madhara yake

6: Heshima kwa Shomari Kibwana Mwili wa Primary, Ukatili wa Guantanamo Bay! What A Kid. Ameicheza 'Derby' kwa miguu, kichwa na Moyo wake. Ujasiri wake.. Kasi na Timing nzuri ya kupokonya mpira, iliwapa Yanga nguvu kwenye kujilinda

7: Mkude.. Ukitafuta kwa makini nini kilipunguza ukali wa Feisal kwenye 'zone ya 14' ya kiwanja anaposhambulia.. Utaiona kazi kubwa ya Jonas Mkude.. Sio kwa ajili ya kukata. Ni kwenye 'Brain' ya kukaba zone

8: YANGA wamecheza Dakika 90 bila Shot On Target. Why? Kuna ubora wa Pablo Tactically kwenye kujilinda Lakini kwa kiasi fulani Uongozi wa Yanga umejua ni Quality gani ya kuongeza kwenye kikosi chao kudeal na 1v1

9: Well Done Ramadhan Kayoko na Wasaidizi wake. Kiasi fulani mechi ilikuwa na presha kubwa. Kama wasingekuwa Fit na makini, kadi zingeweza kuwa nyingi zaidi

10: Shomari Kapombe Mchango mzuri Muzamir Yassin! Hongera kwa Mwamnyeto na Dickson Job.. Mechi nzuri kwa Perfomance zao

Nb: Kumbe inawezekana bila kuwasha moto
Screenshot_20220430-221124_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom