Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,077
- 464,004

Farhan JrKuna wakati ilionekana ngumu kusema upo timu gani kati ya miamba miwili, SIMBA na YANGA, binafsi sijawahi kuona ugumu kwakuwa huwezi kuchambua mpira bila kuwa Shabiki
Kama unapenda pepo usiogope kufa, huwezi kwenda Msikitini au Kanisani kusali kwa ajili ya kufika mbinguni, kama hautaki kufa
Sijawahi kupata tabu yoyote kwenye kazi yangu tangu nimeanza IRINGA as long as nasimama kwenye ukweli, Alhamdulillah nina Rafiki zangu wanacheza Yanga na Simba, nina Viongozi ambao ni Yanga ila ni watu wangu, haijawahi kuwa shida
Basi kwasasa kama FARHAN SHABIKI wa mpira, naitakia kheri timu yangu SIMBA, tushinde dhidi ya Yanga, tukose ubingwa sawa ila tuwalize leo, maana Ndugu zangu haswa Kaka na Dada zangu nyumbani wananitesa sana
Unaweza kujiuliza nawezaje kuchambua wakati chama limefungwa Guys huwa nakuwa na ganzi kama ya dakika 10 hivi ila baada ya hapo ni lazima kazi ziende kwa mujibu wa taaluma yangu
All the best Reds, lakini kheri kwenu pia Wananchi kwakuwa ni sehemu ya familia yangu pia



Sasa Wananchi mnataka kuchukua bila kufungwa kweli??
mwanaume na nusuuuuu

Ilikuwa ni mechi nzuri katika sanaa ya uzuiaji na haikuvutia kwa sababu hazikuonekana zikitengenezwa nafasi nyingi za kufunga, lilikuwa ni swala la nani angeweza kufanya kosa kubwa ili aadhibiwe, timu zote mbili zilikosa funguo ya kuifungua safu ya ulinzi ya timu pinzani ( unlock defensive patterns ).
Inakera kucheza dhidi ya Kibwana Shomary, alicheza vyema mbele ya Morrison, akaonyesha umwamba kwa Sakho na hakumuhofia Shomary Kapombe.
