Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mwili wa Marehemu Maunda Zoro tayari umewasili nyumbani kwake alipokuwa akiishi na Mume wake kwaajili ya Ibada na kuaga kisha kwenda kuzika katika makaburi yaliyopo hapa hapa Tuangoma, Kigamboni.
Screenshot_20220416-143115_Instagram.jpg
 
Wizara ya Afya imepata kibali cha kuajiri Wataalamu 1650 wa vitengo mbalimbali vya Afya ambao wataajiriwa na kupangiwa vituo vya kazi ambavyo vipo chini ya uendeshaji wa moja kwa moja wa Wizara ya Afya.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Dr. Abel Makubi amesema huu ni utekelezaji wa ahadi iliyotolewa na Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Vitengo vitakavyonufaika na nafasi hizi ni pamoja na Madaktari Bingwa (25), Madaktari (215), Wafamasia(15), Maafisa Maabara(62), Wateknolojia (Dawa, Maabara, Mionzi, Macho-155), Maafisa Uuguzi (140).

Vitengo vingine ni Maafisa Uuguzi Wasaidizi (467), Wauguzi (140), Wakemia (2), Madaktari wa Afya Kinywa na Meno (15), Tabibu Meno (19), Watoa Tiba kwa Vitendo (15), Wazoeza Viungo kwa Vitendo(31), Maafisa Wazoeza Viungo (33), Maafisa Afya Mazingira(40), Wasaidizi wa Afya (134), Wahandisi Vifaa Tiba (17), Wateknolojia Vifaa Tiba (40) na Watunza Kumbukumbu wa Afya (10) na Madereva (4).
Screenshot_20220416-152011_Instagram.jpg
 
Mwili wa Mwimbaji Hellen Maunda Zorro aliyefariki kwa ajali ya gari Kigamboni DSM tayari umewasili nyumbani kwa Baba yake Maweni Kigamboni kwa ajili ya kuagwa na kuzikwa leo hii, Maunda amefariki akiwa na umri wa miaka 36, alizaliwa Feb. 2 1986 na amefariki 13 April 2022 na ameacha Watoto watatu wa kiume. View attachment 2189474
Nenda maunda sote safari yetu ni moja
 
VAR KUTUMIA JENERETA !!
.
Meneja wa uwanja wa Mkapa, Godon Nsanjigwa amesema Teknolojia ya V.A.R iliyofungwa kwenye uwanja huo haitotumia nishati ya umeme wa TANESCO badala yake itatumia jenereta ili kuzuia uwezekano wa kuharibika kwa teknolojia hiyo endapo umeme utakatika katikati ya mchezo.
.
Screenshot_20220416-153821_Instagram.jpg
 
Siku chache baada ya kutembelea Ukraine na kuzungumza na Rais wa Ukraine, Urusi imetangaza kumzuia Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson kuingia Urusi kutokana na msimamo wake wa uhasama wa Uingereza kuhusu vita vya Ukraine.

Waziri wa mambo ya nje ya Urusi Liz Truss amesema, Waziri Mkuu wa zamani Theresa May na waziri wa kwanza wa Scotland Nicola Sturgeon ni miongoni mwa Wanachama 13 wa Serikali ya Uingereza na wanasiasa waliozuiwa pia kuingia nchini humo.

Hatua hiyo imechukuliwa kwa kuzingatia hatua ya uhasama isiyo na kifani ya Serikali ya Uingereza, hasusani kuweka vikwazo dhidi ya Maaafisa Wakuu wa Urusi na kusema Urusi itaongeza orodha hiyo hivi karibuni.

Urusi tayari imemzuia Rais wa Marekani Joe Biden na maafisa wengine wengi wa Marekani kuingia nchini humo.
Screenshot_20220416-155657_Instagram.jpg
 
cocastic navyokuambiaga uweke akiba ya maneno uwe unasikia 🤣
Ila sio kesi, mnaweza kupindua meza kibabe… mnadaiwa bao nyingine 3

Cc Saint Anne
Huyu dogo huwaga anajikalia tu lecture room pale yudizim hafatilii Mpira ila anaongea tu ooh tunanyanyua kwapa🤣

Ila wanaweza kutulipa.. Pep siyo mtu mzuri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom