Makapuku Forum

Makapuku Forum

• Baba Mzazi wa Mwimbaji Maunda Zorro ikiwa leo ndio siku ya maziko ameomba kumwimbia mwanae Maunda hapa msibani kama ishara ya kumuaga, Maunda amefariki akiwa na umri wa miaka 36 na ameacha Watoto watatu wa kiume.
Screenshot_20220416-123030_Instagram.jpg
 
Mwili wa Mwimbaji Hellen Maunda Zorro aliyefariki kwa ajali ya gari Kigamboni DSM tayari umewasili nyumbani kwa Baba yake Maweni Kigamboni kwa ajili ya kuagwa na kuzikwa leo hii, Maunda amefariki akiwa na umri wa miaka 36, alizaliwa Feb. 2 1986 na amefariki 13 April 2022 na ameacha Watoto watatu wa kiume.
Screenshot_20220416-123236_Instagram.jpg
 
Mwili wa Mwimbaji Hellen Maunda Zorro aliyefariki kwa ajali ya gari Kigamboni Dar es salaam juzi tayari umewasili nyumbani kwa Baba yake kwa ajili ya kuagwa na kuzikwa leo hii.

Maunda amefariki akiwa na umri wa miaka 36, alizaliwa February 2 1986 na amefariki tarehe 13 April 2022. #RIPMaunda
Screenshot_20220416-123432_Instagram.jpg
 
Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) imetoa tahadhari ya mvua kubwa kwa baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba leo Jumamosi April 16,2022.

TMA imetoa pia angalizo la mvua kubwa kwa maeneo machache ya mikoa ya Dar es salaam na Pwani (ikihusisha visiwa vya Mafia)

"Athari zinazoweza kujitokeza ni baadhi ya makazi kujaa maji pamoja na kuathirika kwa baadhi ya shughuli A uvuvi na usafirishaji, tafadhali zingatia na ujiandae"
Screenshot_20220416-123523_Instagram.jpg
 
DILUNGA NJE WIKI NNE !!
.
Kiungo mshambuliaji wa Simba, Hassan Dilunga amefanyiwa upasuaji nchini Afrika Kusini na sasa imefahamika atakuwa nje kwa muda usiozidi wiki nne kabla ya kurudi tena uwanjani kukiwasha.
.
Dilunga aliumia goti la kulia, Februari mwaka huu katika mazoezi ya timu hiyo akijiandaa na mchezo dhidi ya ASEC Mimosas
.
“Kutokana na matibabu niliyoenda kufanyiwa huko, nitakaa wiki tatu hadi nne, ninaamini nitarejea nikiwa fiti nawashukuru sana viongozi wangu,” amesema Dilunga
Screenshot_20220416-123921_Instagram.jpg
 
ORLANDO KUITESTI VAR LEO !!
.
Wakati VAR ikifungwa jana mchana kwenye Uwanja wa Mkapa, ikitumia zaidi ya saa tano, mitambo hiyo itatestiwa wakati wageni Orlando watakapokuwa wakifanya mazoezi ya mwisho kabla ya mchezo wa kesho uwanjani hapo.
.
Awali ilikuwa mitambo hiyo ijaribiwe katika mazoezi ya Simba leo saa 4:00 asubuhi, lakini imeahirishwa kwani inatakiwa kujaribiwa muda kamili wa mchezo husika.
.
Msimamizi wa VAR kwa Tanzania, Leslei Liunda aliye pia mkufunzi wa Waamuzi wa Caf alisema kila kitu kinaendelea vizuri kuhusu mitambo hiyo na leo saa 1:00 usiku itatumika kwa mara ya kwanza nchini.

……..
Screenshot_20220416-124018_Instagram.jpg
 
Orlando Pirates ilipewa jina hilo kutokana na Mwanasiasa nguli ambaye alikuwa Meya wa jiji la Johanesburg anaitwa Edward Orlando Leeke, hivyo kutokano na umaarufu wake wakatumia jina Orlando

Hilo Pirates ilikuja baada ya movie maarufu zaidi miaka ya 1940 huko Kusini ilifahamika kama Sea Hawk ambapo Mwigizaji Mkuu alikuwa Errol Flyn hivyo kutokana na movie hiyo kuelezea kuhusu Maharamia wakachukua jina hilo

Na sasa itambulika kama ORLANDO PIRATES ambao tayari wapo nchini Tanzania
Screenshot_20220416-124214_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom