Makapuku Forum

Makapuku Forum

Eric Ten Haag moja kati ya vitu ambavyo anataka vipewe uzito pale Old Trafford ni:

-Yeye kuwa na sauti kwenye dirisha la usajili

-Kuingia na bench lake la ufundi (amefanikiwa)

Lakini wakati anafanya majadiliano na Bwana Fletcher kuna vitu vingi walipishana juu ya kikosi cha United na namna anataka kiwe

Inasemekana anahitaji mabadiliko makubwa sana ambayo kwa jicho la kawaida ni ngumu
Screenshot_20220416-124344_Instagram.jpg
 
Nahodha Mark Noble wa West Ham baada ya ushindi wao dhidi ya Lyon kwenye Europa League, alitumia muda wake kusafisha dressing room kabla ya kuondoka, hufanya hivyo kwa heshima ya mpinzani wao

Ana miaka 18 ndani ya West Ham na atastaafu mwishoni mwa msimu huu
Screenshot_20220416-125109_Instagram.jpg
 
Baadhi ya mashabiki wa Manchester United waliwasili katika viunga vya Carrington kwa ajili ya kufanya maandamano ya kupinga wamiliki wa klabu hiyo ambao ni familia ya Glazer.

Mashabiki hao wa Manchester United walionekana wakiwa wamebeba mabango yaliyoandikwa "GLAZERS OUT" ili kuwashinikiza wamiliki hao waachie timu yao baada ya kuona mwenendo wa klabu yao sio mzuri, hata hivyo imeripotiwa kuwa polisi walipigiwa simu kuja kuwatawanya waandamanaji hao na walifanikiwa.
Screenshot_20220416-125659_Instagram.jpg
 
Picha mbalimbali zikionesha msafara na nyumbani kwa Mzee Zorro ulipo msiba wa Maunda Zorro ambapo Watu mbalimbali wamejitokeza kwa ajili ya kumsindikiza Mwimbaji huyu kwenye siku yake hii ya kuzikwa.

Kwenye picha anaonekana mmoja wa Mtoto wake watatu aliowaacha.
Screenshot_20220416-130118_Instagram.jpg
 
Picha mbalimbali zikionesha msafara na nyumbani kwa Mzee Zorro ulipo msiba wa Maunda Zorro ambapo Watu mbalimbali wamejitokeza kwa ajili ya kumsindikiza Mwimbaji huyu kwenye siku yake hii ya kuzikwa.

Kwenye picha anaonekana mmoja wa Mtoto wake watatu aliowaacha. View attachment 2189507

Picha ya huyo mtoto imenitoa chozi...
Mungu awalinde jamani
 
• Ni furaha kwa mashabiki wa Yanga kwani mshambuliaji wao, Chico Ushindi ameanza kufanya mazoezi baada kupona majeraha yaliyokuwa yanamsumbua.
Mchezaji huyo huyo amekuwa akisumbuliwa na majeraha toka amejiunga na Wananchi kwani hajapata muda wa kutosha kuwaonyesha mashabiki alichonacho.

Mtaalam wa mazoezi ya viungo wa timu hiyo, Helmy Gueldich aliweka wazi kuwa staa huyo ana kipaji kikubwa na atawashangaza wengi atakapomaliza programu yao.
Screenshot_20220416-134612_Instagram.jpg
 
Wizara ya Afya imetangaza nafasi za ajira 1650 kwa wataalamu wa kada mbalimbali za afya nchini.

Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi Aprili 16, 2022 na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Profesa Abel Makubi imeeleza kuwa wizara hiyo imepata kibali cha kuajiri ambapo wataalamu hao wataajiriwa na kupangiwa vituo vya kazi ambavyo vipo chini ya uendeshaji wa moja kwa moja wa wizara hiyo.

Miongoni mwa nafasi hizo, zipo za madaktari bingwa (25), madaktari (215), wafamasia(15), maafisa maabara(62), wateknolojia (dawa, maabara, mionzi, macho-155), maafisa uuguzi (140), maafisa uuguzi wasaidizi (467), wauguzi (140), wakemia (2), madaktari wa afya kinywa na meno (15), tabibu meno (19), watoa tiba kwa vitendo (15), wazoeza viungo kwa vitendo(31), maafisa wazoeza viungo (33), maafisa afya mazingira(40), wasaidizi wa afya (134), wahandisi vifaa tiba (17), wateknolojia vifaa tiba (40) , watunza kumbukumbu wa wfya (10) na madereva (4).
Screenshot_20220416-135207_Instagram.jpg
 
Katika ripoti CAG imeeleza Serikali imepata hasara ya Sh2.42 bilioni kutokana na stika 21,208 za viza zinazodaiwa kughushiwa na kumbukumbu zake kufutwa kwa makusudi kwenye Mfumo wa Maombi ya Viza (VAS) na maofisa uhamiaji wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Ilielezwa kati ya Januari mosi 2019 hadi Juni 30, 2019 ukaguzi ulibaini Watanzania 41 na wageni 107,119 waliwasili nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Wageni 33,558 waliwasili kupitia KIA, ingawa taarifa zao ambazo ni pamoja na stakabadhi za mapokezi ya fedha (ERV), fomu za kuingia nchini, pamoja na taarifa za uwekaji fedha benki hazikuweza kupatikana.
Screenshot_20220416-135309_Instagram.jpg
 
Simba inamkosa beki wake Joash Onyango kwenye mchezo dhidi ya Orlando Pirates katika kombe la Shirikisho Afrika hapo kesho April 17 kwenye uwanja wa Mkapa.
Unadhani Henoc Inonga acheze na nani kuuweka ukuta wao salama ni Pascal Wawa au Kenedy Juma?

Screenshot_20220416-135416_Instagram.jpg
 
Kocha wa klabu ya Simba, Pablo Franco hii leo katika mahojiano yake na Waandishi wa Habari ameomba sapoti ya mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa siku ya kesho ili kuwapa morali wachezaji katika mchezo wao wa robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Orlando Pirates.
Pablo amesisitiza kuwa ni wazi timu yake imekuwa na rekodi nzuri inapocheza nyumbani kwahiyo wachezaji na timu kwa ujumla wanakila sababu ya kutumia faida ya uwanja wa nyumbani na kuhakikisha wanashinda pambano hilo.
Screenshot_20220416-135511_Instagram.jpg
 
Kocha Mkuu wa Simba Pablo Franco amewatoa hofu wachezaji wake na kuwaonya juu technolojia ya usaidizi kwa waamuzi (VAR), ambapo mitambo yake itatestiwa na Orlando Pirates ya Afrika Kusini itakapokuwa ikipiga tizi kwa Mkapa, kabla ya kuvaana na Simba kwenye robo fainali ya Kombe la Shirikisho Aprili 17, 2022 katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam.
Screenshot_20220416-135600_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom