

Farhan jr
Katika transformation kubwa ambayo Simba wameifanya kwa misimu mitatu nyuma ni eneo la usajili na uhamisho wa wachezaji, eneo wamejifunza vingi
Afrika Mashariki hii timu nyingi zinafanya sajili za kujuana, za kishkaji na kwenda mbali zaidi zina mikono ya watu ndani ya system ya timu (SYSTEMIC REGISTRATION)
Sajili hizo mara nyingi haziendi kutibu shida ya timu bali kutibu matatizo kwenye mifuko ya watu, kupitia 10% ndio maana sajili nyingi za kimataifa zilikuwa zinafeli sana nchini, Simba ikiwemo
Hakuna njia iliyosalia ya kubadili upepo zaidi ya kukubali kujifunza, kupata EE BALANCE yaan Exposure na Experience, ndipo CEO alipopaswa kusafiri kufahamu wenzao wanafanyaje
Alifika Al Ahly pale Misri, TP Mazembe (alipata kuonana na Viongozi) pamoja na Mamelodi Sundowns, yote hii ni miamba Afrika ambayo imebobea kwenye biashara za wachezaji
Katika darasa kubwa alilopata CEO ni networking, kati ya Klabu na AGENCIES (Mawakala) ambao wapo kwenye mfumo wa Kampuni, yes ndio njia rahisi zaidi ya kupata wachezaji wazuri kwa gharama nzuri kisha kufanya biashara kubwa
Simba kupitia Agencies wakapata faida ya kuwa na Scouts zaidi ya 62 Afrika nzima, ni rahisi wao kumpata Sakho mwingine kutoka Bambali, Peter Banda mwingine kutoka Lilongwe au Kanoute mwingine kutoka Mali
Hii biashara ni WIN WIN, kwakuwa walichowin Simba ni kuwa na uwanja mzuri wa mazungumzo kabla ya biashara (PHATIC FUNCTION PER BUSINESS) ndio urahisi huu walimpata Peter Banda mbele ya Sherrif Tiraspol
Wamejifunza kitu, hata ukitazama sajili zao za kimataifa msimu huu, watoto wengi wana misimu zaidi ya nane mbele na biashara kubwa mbele, zoezi kubwa walilosalia nalo ni dirisha la ndani, kuna sehemu padogo pana shida, JE NI WAPI HAPO?
Lets end here, but tomorrow we shall continue tackling some more problems concerning this case

ITAENDELEA