Kirusi kingine kipya cha corona kimeibuka katika nchi za China, Japan na Korea.
China kwa sasa inapambana na visa vya Uviko-19 zaidi ya mara mbili katika milipuko inayokua kwa kasi, katika mkakati wa nchi hiyo kutokomeza ugonjwa huo.
Machi 15 nchi hiyo imeripoti zaidi ya wagonjwa wapya 5,000 waliothibitishwa kupata Uviko-19, zaidi ya mara mbili ya idadi iliyoripotiwa Jumatatu Machi 14 na hesabu kubwa zaidi ya kila siku tangu janga hilo lianze zaidi ya miaka miwili iliyopita.
Kutokana na hali hiyo, Waziri wa Afya nchini Ummy Mwalimu amewataka wananchi waendelea kujitokeza kupata chanjo kwa kuwa haina madhara kama baadhi ya watu wanavyosema.
Pia amesema aina mpya ya kirusi kipya kilichoibuka nchini China, Japan pamoja na Korea ni tahadhari hivyo amewataka wananchi kuendelea kuwa makini huku akisisitiza wajitokeze kupata chanjo.
"Kwa sasa kitu ambacho kinaweza kutusaidia kujikinga na Uviko-19 ni chanjo kwa kuwa ni salama sana, nawaomba wote ambao hamjapata mkapate chanjo ili tuweze kujikinga," Amesema Waziri Ummy.