Makapuku Forum

Makapuku Forum

• Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema Ukraine inawatumia Raia kama ngao ya kujilinda na kusema Ukraine imeomba Safe Corridor ili zitumike kuwaokoa Watu kutoka Ukraine lakini wala haziwaondoi Watu hao "Jeshi letu liliacha kushambulia ili Raia wasio na hatia waondoke kwanza lakini Ukraine imegoma kuwaruhusu Raia kuondoka"

Putin amezifananisha tabia anazodai zinafanywa na Ukraine za kuwatumia Raia kama ngao ya kukwepa mashambulizi na Watu walioamini itakadi za kinazi za Adolf Hitler ambao anasema walijificha nyuma ya Raia kutafuta huruma na kuwatumia kama ngao ya kukwepa kushambuliwa badala kuwaruhusu Raia hao waondoke salama ili mapambano yaendelee.

Kauli ya Putin inakuja baada ya Naibu Meya wa Mji wa Mariupol nchini Ukraine kusema bado Wanajeshi wa Urusi wanaendelea kushambulia Mji huo licha ya makubaliano yaliyofikiwa na Urusi na Ukraine kwamba wasitishe mapigano kwa muda mfupi katika Miji miwili ya Mariupol na Volnovakha iliyokumbwa na mapigano ili kuwaruhusu Raia kuondoka.

Miongoni mwa waliotengenezewa Corridor ili pamoja na Raia wa Tanzania ambapo Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliopo Moscow nchini Urusi umetoa taarifa kwa Wanafunzi wote wa Kitanzania walioko kwenye Chuo cha Taifa cha Sumy nchini Ukraine kwamba Serikali ya Urusi imetengeneza Safe Corridor ya Wanafunzi hao kutoka Ukraine kupitia Urusi kuanzia leo March 05,2022 .
Screenshot_20220305-203124_Instagram.jpg
 
"Serikali ya Awamu ya Sita imehakikisha Watu wanaoishi na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (WAVIU) wanapata bure dawa za kufubaza makali ya
Virusi vya UKIMWI (ARVs) na vitendanishi kwa ajili ya vipimo vya VVU"

"Serikali imewezesha upatikanaji wa bidhaa hizi kwa asilimia 100"——— Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akitoa taarifa ya mafanikio ya Wizara kwa kipindi cha mwaka mmoja wa Uongozi wa Rais Samia
#
Screenshot_20220305-204121_Instagram.jpg
 
Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliopo Moscow nchini Urusi umetoa taarifa kwa Wanafunzi wote wa Kitanzania walioko kwenye Chuo cha Taifa cha Sumy nchini Ukraine kwamba Serikali ya Urusi imetengeneza Safe Corridor ya Wanafunzi hao kutoka Ukraine kupitia Urusi kuanzia leo March 05,2022 .

"Wanafunzi wanatakiwa kutoka Chuoni kuelekea eneo la Sudja ambapo watapokelewa na Jeshi la Urusi, kutoka Urusi watasafirishwa na Jeshi hilo hadi eneo la Belgorod ambapo watapokelewa na Maafisa wa Ubalozi wa Tanzania uliopo Moscow kwa taratibu nyingine za kurejea Tanzania"

"Wanafunzi wanashauriwa kutoka Chuoni kwa makundi na kubeba Bendera ya Tanzania ili kuwatambulisha wanapopita kwenye Safe Corridor ili kurahisisha uratibu wa zoezi la mapokezi"
Screenshot_20220305-205239_Instagram.jpg
 
Naibu Meya wa Mji wa Mariupol nchini Ukraine amesema bado Wanajeshi wa Urusi wanaendelea kushambulia Mji huo licha ya makubaliano yaliyofikiwa na Urusi na Ukraine kwamba wasitishe mapigano kwa muda mfupi katika Miji miwili ya Mariupol na Volnovakha iliyokumbwa na mapigano ili kuwaruhusu Raia kuondoka.

Naibu Meya huyo amesema zoezi la kuwasaidia Raia kuondoka salama kwenye Mji wake limesimamishwa kutokana na Urusi kukiuka makubaliano na kuendeleza mashambulizi.
Screenshot_20220305-210223_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom