Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220305-075207_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20220305-075233_Opera%20Mini.jpg
 
| Opah Clement Yikatel Kayseri
.
Mshambuliaji wa klabu ya Simba Queens kinara wa kutiskisa nyavu , Opa Clement amekwea Pipa kuelekea nchini Uturuki kwaajili ya kufanya majaribio ya mwezi mmoja katika klabu ya Yikatel Kayseri inayoshiriki ligi Kuu nchini humo.
.
Kila la kheri
Screenshot_20220305-131039_Instagram.jpg
 
PIGO:: CHICO HATIHATI KUIKOSA GEITA
.
Winga wa Yanga amepatwa na majeraha akiwa mazoezini hali iliyomfanya apelekwe Hospitali kwa vipimo zaidi.
Screenshot_20220305-131355_Instagram.jpg
 
SAKHO: HUYU KAPOMBE ANAJUA
.
Kama unamchukulia poa beki wa Simba, Shomari Kapombe basi pole yako, kwani kwa Pape Sakho umwambii kitu kuhusu Kapombe ndio beki anayemvutia nchini;
.
“Kapombe yuko na sifa nyingi kulingana na mahitaji ya beki wa kulia, ndio maana amekuwa akinivutia mpaka amekuwa rafiki yangu wa karibu hata tukiwa nje ya maisha ya timu.” amesema Sakho na kuongeza;
.
“Nashukuru kwa wakati huu nimekuwa kwenye kiwango ingawa sio katika ubora kama ule ambao naamini ninao bado nahitajika kujitoa zaidi na kusaidia timu.”

………..
Screenshot_20220305-131901_Instagram.jpg
 
LUIS: BADO NAIPA NAFASI SIMBA KUCHUKUA UBINGWA
.
Kiungo wa zamani wa Simba, Luis Miquissone anasema kutokana na mwenendo wa Ligi Kuu Bara ulivyo msimu huu bado timu ya Simba inaweza kutwaa ubingwa na ikautetea kwa mara ya tano mfululizo.
.
"Bado naipa nafasi kubwa timu yangu (Simba) kufanya hivyo lakini hata katika mashindano mengine kama kombe la Shirikisho (ASFC), nalo wanaweza kufanya vizuri na kuchukua ubingwa” amesema Luis (via Goal Africa)
Screenshot_20220305-132055_Instagram.jpg
 
DJUMA SHABANI KUIKOSA GEITA KESHO
.
Imethibitishwa beki Djuma Shabani (23) ni miongoni mwa wachezaji wa Yanga ambao hawakusafiri na timu jana kutokana na matatizo binafsi.
.
Sasa ni rasmi Yanga kesho itawakosa mastaa wake wawili, kiungo khalid Aucho na beki Djuma Shabani.
Screenshot_20220305-132220_Instagram.jpg
 
MAJANGA: AUCHO ABAKI DAR
.
Baada ya kukoseka kwenye msafara wa timu ulioondoka jana Dar na kutua Mwanza. Taarifa za ndaani zinaeleza kuwa staa wa Yanga, Khalid Aucho hayupo sawa kiafya ndio sababu ya kuachwa Dar na kuna uwezekano akaelekea nyumbani.

......……..
Screenshot_20220305-132339_Instagram.jpg
 
"Hadi kufikia Februari, 2022, Tanzania inakadiriwa kuwa na Watu 1,700,000 wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (WAVIU) ambapo, WAVIU Milioni 1,491,147 sawa na 88% ya WAVIU wote walikuwa wanatambua hali zao za VVU ikilinganishwa 83% mwezi Machi 2020"

"Vilevile kati ya WAVIU Milioni 1,471,450 sawa na 99% ikilinganishwa na WAVIU 98.6% Machi 2021 wako katika tiba endelevu ya ARV na 95.8% walikuwa wamefubaza VVU ikilinganishwa na
94.8%, Machi 2022"

"Kati ya Wenye Virusi vya UKIMWI (WAVIU) Milioni 1,471,450 sawa na 99% ikilinganishwa na WAVIU 98.6% Machi 2021 wako katika tiba endelevu ya ARVs na 95.8% walikuwa wamefubaza VVU ikilinganishwa na 94.8% Machi 2022"

"Hii imetokana na kwamba Tanzania imeendelea kujipima kwa malengo ya 95-95-95, ambapo 95% ya WAVIU wanatakiwa kujua hali zao za maambukizi, 95% ya wanaojua hali zao wawe wameanza dawa za kufubaza VVU na 95% ya walio kwenye dawa wawe wamefubaza VVU chini ya kopi 1000 ifikapo 2025" ——— Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akitoa taarifa ya mafanikio ya Wizara kwa kipindi cha mwaka mmoja wa Uongozi wa Rais Samia
Screenshot_20220305-201627_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom