Makapuku Forum

Makapuku Forum

BREAKING: Roman Abramovich ametangaza rasmi nia yake ya kuiuza Klabu ya Chelsea:
.
"Siku zote nimekuwa nikichukua maamuzi kwa nia ya dhati ya Klabu. Nimechukua uamuzi wa kuuza Klabu. Ninaamini hii ni kwa manufaa ya Klabu, mashabiki, wafanyakazi, pamoja na wafadhili na washirika wa Klabu. Inaniuma kuachana na Klabu kwa namna hii. Hata hivyo, ninaamini hii ni kwa manufaa ya Klabu. Natumai kwamba nitaweza kutembelea Stamford Bridge kwa mara ya mwisho ili kuwaaga ninyi nyote.
Screenshot_20220304-073921_Instagram.jpg
 
| YANGA KUONDOKA DAR LEO
.
Yanga inaondoka leo jijini Dar kwenda Mwanza kuwahi mchezo wao wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Geita Gold utakaopigwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, huku ikiwa ipo kileleni mwa msimamo ikikusanya pointi 42 kupitia mechi 16 na kufunga mabao 28 na yenyewe wavu wake ukiguswa mara nne.
.
Straika raia wa DR Congo, Fiston Mayele ndiye kinara wa mabao wa Yanga akifunga tisa akifuatiwa na Saido mwenye mabao sita, huku Feisal Toto akitupia manne na Aucho amefunga matatu hadi sasa akilingana na winga Jesus Moloko

......……..
Screenshot_20220304-075659_Instagram.jpg
 
MSUVA KUKOMAA NA WYDAD FIFA
.
Kwa mujibu wa Maghrib Foot imeripotiwa kuwa, Simon Msuva amekamilisha kwa asilimia 80 mchakato wa kuishtaki klabu yake ya Wydad Casablanca huko Fifa (shirikisho la kimataifa la soka) ambapo wakati wowote kuanzia sasa atawapeleka huko ili kupata haki yake.
Screenshot_20220304-075853_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom