Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220304-041605_Opera%20Mini.jpg
 
LICHA ya Yanga kutambia pointi 11 zaidi ilizoipiku Simba katika harakati za ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa klabu ya Simba, Salim Abdallah ‘Try Again’ ameonya wana mechi 15 watakazocheza kimkakati na wanaamini kushangaza wengi.

Amesisitiza; “Sawa tunaanza mzunguko wa pili tukiwa tumezidiwa pointi 11, lakini tuna mechi 15 mbeleni, hivyo tusubiri, msiwe na haraka na mambo.”

Yanga Jumapili iliyopita ilifikisha pointi 42 na kujiimarisha kileleni kwenye msimamo ikiwapiku watani zao Simba kwa pointi 11 na kesho Wekundu wa Msimbazi wataikaribisha Biashara United ikiwa ni mechi yao ya kwanza ya mzunguko wa pili.

Screenshot_20220304-072257_Instagram.jpg
 
TEN-HAG AJIFUNZA KIINGEREZA KISA UNITED
.
Kocha anayeinoa Ajax, Erik ten Hag ameanza kujifunza lugha ya kiingereza kwa ajili ya mazungumzo kati yake na uongozi wa Manchester United.
.
Imeelezwa Erik Ten Hag ameanza kuonyesha kila dalili ya kutaka kuchukua mikoba ya kocha wa mpito wa sasa Man United, Ralf Tangnick atakayemaliza muda wake mwisho wa msimu huu.
.
Kwa upande wa mabosi wa Ajax wanafahamu nia ya Erik Ten Hag ya kutaka kuondoka msimu huu utakapoisha kwani wamekaa na kufanya mazungumzo kuhusu hatima yake, huku Man United ikitajwa kuwa sehemu pekee ambayo anaweza kwenda kuwanoa vijana wa Old Trafford.
Screenshot_20220304-072613_Instagram.jpg
 
DROO YA ROBO FAINALI FA CUP
.

Middlesbrough vs Chelsea
Southampton vs Manchester City
Crystal Palace vs Everton or Boreham Wood
Notts Forest or Huddersfield Town vs Liverpool
.
Nani kutwaa ndoo __?
Screenshot_20220304-072753_Instagram.jpg
 
MTIBWA KUISHTAKI YANGA TFF
.
Inaelezwa kuwa Uongozi wa Mtibwa Sugar umejipanga kuishitaki klabu ya Yanga kwa Shirikisho la Soka Nchini (TFF), wakishinikiza walipwe madai yao kutokana na mauzo ya aliyekuwa Mchezaji wao Aboutwaleeb Mshery (21).
Screenshot_20220304-073431_Instagram.jpg
 
HATMA YA MBAPPE PSG IKO HIVI
.
Kutoka kwa Fabrizio, Mkurugenzi mkuu wa klabu ya Paris Saint-Germain Leonardo amefunguka kuhusu mkataba wa Kylian Mbappe
.
“Tuna nafasi ngapi za kuongeza mkataba wa Mbappe? Siwezi kusema kwa usahihi, lakini uwezekano upo.”
.
“Mradi tu hajasaini [na klabu nyingine], Paris St Germain itajaribu kwa kila kitu ili kumbakisha Kylian Mbappé hapa".
.
Leonardo amekanusha pia tetesi za PSG kumpa Mbappe ofa ya mshahara wa Euro milioni 50 (Sh Bilioni 128).
.
Lipi litakua chaguo sahihi kwa Mbappe, Abaki PSG au atimkie Madrid __!!
Screenshot_20220304-073608_Instagram.jpg
 
BIASHARA: TUNAZITAKA POINTI TATU DHIDI YA SIMBA
.
Kocha Mkuu wa Biashara United, Vivier Bahati amefunguka kuelekea mchezo dhidi ya Simba SC:
.
“Hii mechi itakuwa ngumu sana kwa sababu tunacheza na Simba ambayo imetoka kupoteza mchezo wao wa kimataifa na wanapambana kutafuta pointi muhimu ili kujiweka katika nafasi ya kutetea ubingwa,” amesema Vivier na kuongeza;
.
"Tunahitaji kuanza vizuri mzunguko wa pili kwa kutafuta pointi dhidi ya Simba kama ilivyokuwa katika mchezo wa duru la kwanza.”
Screenshot_20220304-073735_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom