Makapuku Forum

Makapuku Forum

Taarifa kutoka ndani ya Simba zinasema kocha Pablo Franco aliwasilisha ripoti akiweka bayana alichokiona tangu alipotua klabuni hapo, huku akitaja majina ya kufyekwa na vitu vinavyotakiwa kuboreshwa ikiwamo wachezaji wapya watatu ambao ni wakali kuliko waliopo kwa ajili ya michuano ya ndani na ya kimataifa.

Inaelezwa kuwa, huenda Simba ikaachana na wachezaji watatu wa kigeni wanaoweza kutolewa kwa mkopo ili nafasi zijazwe na majembe watatu wanaotakiwa, huku wanaotajwa ni beki wa kati Pascal Wawa, Duncan Nyoni na Pape Ousmane Sakho.

Simba imetinga makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kuing’oa Red Arrows ya Zambia na Kocha Pablo anataka kuhakikisha inafika mbali zaidi kuliko msimu uliopita katika Ligi ya Mabingwa Afrika ilipoishia ya robo fainali.

Taarifa zaidi zinasema Pablo katika usajili wa dirisha dogo lililofunguliwa jana ametaka kiungo mshambuliaji (namba 8) mwenye uwezo zaidi wa Sadio Kanoute anayecheza nafasi hiyo mara kwa mara.

Pia amependekeza washambuliaji wa kati watakaocheza pacha yaani namba 9 na 10 wenye uwezo mkubwa wa kutupia nyavuni kuliko Meddie Kagere, John Bocco na Chriss Mugalu.
Screenshot_20211217-163058_Instagram.jpg
 
Wakati baadhi ya watu kwa takriban wiki moja sasa wakiwa na hofu kutokana na kuugua kikohozi kikali, mafua, maumivu ya kichwa, mgongo na homa, Serikali imesema hali hiyo ni ya kawaida kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa, (mvua) zinazoendelea kunyesha maeneo tofauti.

Hata hivyo, baadhi ya madaktari wameliambia Mwananchi kuwa ni vema watu wachukue tahadhari zilizotolewa dhidi ya ugonjwa wa Uviko-19.

Desemba mwaka jana liliibuka wimbi la tatu la virusi vya Uviko-19 vilivyojulikana kama Delta na watu kadhaa duniani walifariki dunia, huku wengine wakiugua.

Hofu ya wimbi hilo kuingia hapa nchini iliondolewa wiki iliyopita na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aliyewahakikishia Watanzania kuwa virusi hivyo bado havijaingia nchini na kushauri watu waendelee kujikinga.

Akizungumza na Mwananchi, daktari bingwa wa magonjwa ya mfumo wa upumuaji kutoka Hospitali ya Aga Khan, Alex Masao alikiri kuhudumia wagonjwa wengi wenye dalili hizo kwa takribani wiki mbili sasa.

“Tunapokea wagonjwa wengi wiki hii na kwa kifupi tu kati ya wagonjwa 10 tunaowapokea Aga Khan sasa hivi, sita wanakuja na malalamiko ya homa, mafua, kifua, kuchoka na maumivu ya mwili,” alisema.
Screenshot_20211217-163257_Instagram.jpg
 
"Nilipata mashtaka, nilipata nafasi ya kusikilizwa na leo hukumu imetolewa, kazi ya kusema kweli ina safari kidogo na nadhani kwa Mimi ambaye ni Mwanachama wa CCM kwa imani na ninayeamini katika kusema kweli bila kuweka chembe ya fitna ndani yake, Mimi ninayeamini katika ahadi nyingine ya CCM inayosema 'nitafanya jitihada kujielimisha na kuitumia elimu yangu kwa faida ya wote', kwangu Mimi hii ni mitihani midogo"

"Nitakaaa na Wasaidizi wangu tutatafakari na nitawajulisha hatua ambayo itafuata, kubwa ninalomalizia ni kwamba kazi ya kusema kweli bado ina safari na binafsi sitokata tamaa kwakuwa ninachokifanya kinalinda maslahi mapana ya Nchi yetu, Watu wake, Mamlaka ya Nchi na CCM" ———Mbunge Polepole baada ya TCRA kumtaka asimamishe kurusha maudhui ya kipindi chake cha Shule ya Uongozi
Screenshot_20211217-163619_Instagram.jpg
 
Mwalimu wa Shule ya Msingi Magemo iliyopo Kaunti ya Bungoma nchini Kenya, Wycliffe Akeve amejimwagia petrol na kujichoma moto baada ya kupewa barua ya kusitishwa kwa mkataba wake wa kazi.

Ajira ya Mwalimu huyo imesitishwa na Mwajiri wake baada ya kudaiwa amempa mimba mmoja wa Wanafunzi wake.

Baada ya kupokea barua hiyo Mwalimu huyo alijifungia kwenye Ofisi ya Walimu na kujichoma moto kabla ya Watu kumuokoa ambapo kwa sasa amelazwa Hospitali ya Bungoma akiendelea na matibabu kufuatia majeraha makubwa aliyoyapata.
Screenshot_20211217-164210_Instagram.jpg
 
Kutakuwa na njia tatu za kuchangia ujenzi wa uwanja wa klabu ya Simba.

1. Kuchangia kupitia mitandao ya simu
  • Vodacom [M-Pesa]
  • Tigo [TigoPesa]
  • Aitel [Airtel Money]

2. Lipa Namba
- kuna lipa namba ambazo tayari zimesajiliwa na watu wataweza kuchangia.

3. Bank [NMB]

Jina la ambalo litakalotoka kabla ya kukamilisha muamala ni Simba Sports Club Tanzania Ltd.

Taarifa zaidi kuhusu namna ya kuchangia itatolewa kwenye vyanzo rasmi vya mawasiliano vya klabu.
Screenshot_20211217-164519_Instagram.jpg
 
BREAKING|

Klabu ya Simba imezindua rasmi KAMPENI ya kuchangia ujenzi wa uwanja. Kampeni hiyo inaitwa SIMBA YETU, UWANJA WETU.

Mtendaji Mkuu wa Simba Babra na Mwenyekiti wa Wanachama Bw. Murtaza Mangungu kwa pamoja wamezindua kampeni hiyo.
Screenshot_20211217-164625_Instagram.jpg
 
Kwenye kurasa rasmi za Instagram kwa Klabu kubwa duniani, bila shaka hakuna Admn mwenye majigambo na vitisho kama wa Bayern Munich

Just imagine kaweka frame tatu za Lewandowski akiwa mazoezini, basi tu kuikumbusha dunia kuhusu Mpoland
Screenshot_20211217-165019_Instagram.jpg
 
Shaffih Dauda

Ni kipindi cha usajili wa dirisha dogo, ni wakati wa vijana kuwa makini katika kipindi hiki kwa maslahi mapana ya maisha yao ya soka na vipaji vyao.

Ni kweli kwenye vilabu vya Simba na Yanga wachezaji wanapata angalau maslahi mazuri [maisha mazuri, mshahara mzuri, posho na bonus] lakini vijana wengi wanazika career zao.

Huwezi kupata vitu vyote kwa wakati mmoja hasa kwa vijana wanaokua, lazima uchague kimoja, kuendeleza kipaji au uchague kibunda. Bahati mbaya sana vijana wa kibongo wanachagua vibunda kuliko kuendeleza vipaji vyao.

Niliwahi kuzungumza wakati Salamba anatoka Lipuli kwenda Simba, anatoka kwenye timu aliyokuwa na uhakika wa kucheza kila mara anaenda kwenye timu ambayo eneo lake lina Bocco, Kagere na Okwi unategemea atapata nafasi ya kutosha?

Mifano ipo mingi ya wachezaji waliofanya vizuri kwenye timu nyingine lakini wakakwama Simba, Yanga, Azam kwa sababu ya kukosa nafasi. Mohamed Rashid, Ilanfia, Waziri Jr si wachezaji wabaya lakini kutokana na mahitaji ya hivi vilabu walishindwa kutoboa.

Kwa hiyo kwa mchezaji ambaye bado kijana, naona kipaumbele ni career yake kuliko pesa. Anatakiwa kuwa sehemu ambayo atacheza mechi za kutosha ili kulinda kipaji na kiwango chake kikue zaidi halafu badae atapata kibunda huku akiwa anapata nafasi ya kucheza.

Lakini ikitokea kijana mdogo anawaza kibunda kwanza, atapata lakini huenda akaingia shimoni halafu kutoka ikawa jambo jingine.

Hivi vilabu pia vinatakiwa kulinda vipaji vya watoto, wanaweza kuona kijana mwenye uwezo wakamsaini halafu wakamwacha kwenye timu ambayo atapata nafasi. Ikifika wakati unamuhitaji unamchukua unamtumia.
Screenshot_20211217-165135_Instagram.jpg
 
Kifua, mafua tishio kwa wachezaji Simba
.
“Nashkuru Mungu tumeweza kufika salama jana tumekuwa na changamoto kidogo baadhi ya wachezaji nafikiri karibu robo tatu wamekuwa wakiugua mafua na kifua na homa za hapa na hapa sijui ni kutokana na hali ya hewa au ni nini na baadhi ya benchi la ufundi” amesema Matola na kuongeza

“Mpaka sasa hatujui itakuwaje kwani hatujui chanzo na tumeacha madaktari wafanye vipimo na baadae tujue nini tatizo kwani hata mimi na baadhi ya watu wa benchi la ufundi wanaumwa”
.
- Kocha Msaidizi wa timu ya Simba, Selemani Matola.
Screenshot_20211217-165510_Instagram.jpg
 
Morrison, Bwalya kuikosa Kagera
.
Meneja wa Simba, Patrcik Rweyemamu amesema wachezaji TISA wameachwa kwa sababu mbalimbali ikiwamo kuwa majeruhi, kuugua na matatizo ya kifamilia, lakini jeshi lililopo Bukoba, lipo tayari kupeleka moto kwa Kagera ili kuendeleza wimbi lao la ushindi.
.
Wachezaji walioachwa ni; Bernard Morrison, Rally Bwalya, John Bocco, Chris Mugalu, Taddeo Lwanga, Erasto Nyoni, kipa, Jeremiah Kisubi, Israel Mwenda na Pascal Wawa.
Screenshot_20211217-165633_Instagram.jpg
 
Prisons yaipiga mkwara Yanga
.
“Yanga wasitarajie mteremko, tunawasubiri kwa hamu tuliwaona kwenye mechi zao, lakini niwaombe mashabiki waje kwa wingi waone pira gwaride, tutakomaa na kuweka rekodi Jumapili,” amesema Jeremiah Juma mchezaji pekee hadi sasa kufunga hat trick ligi kuu.
Screenshot_20211217-165744_Instagram.jpg
 
“Nimewaomba viongozi wampeleke Kibwana nchini Tunisia sehemu aliyopelekwa pia Yacouba kwa ajili ya matibabu zaidi ya kina, kwani kule ni mahali tulivu na penye mazingira rafiki,”

- Kocha Nasreddine Nabi.
Screenshot_20211217-165839_Instagram.jpg
 
Mahakama kuu divisheni ya makosa ya rushwa na uhujumu uchumi imetupilia mbali mapingamizi mawili yaliyotolewa na upande wa utetezi katika kesi ya ugaidi inayomkabili mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu na kupokea hati ya ukamataji mali.

Mbowe na wenzake hao, Halfan Bwire, Adamu Kasekwa na Mohamed Ling’wenya wanakabiliwa na kesi hiyo inayosikilizwa na Jaji Joachim Tiganga.

Uamuzi huo unahusu mapingamizi mawili ya mawakili wa utetezi katika kesi hiyo ambayo ni orodha ya vielelezo na mnyororo wa utunzaji vielelezo.

Akitoa uamuzi huo leo Ijumaa Desemba 17, 2021 Jaji Tiganga amesema mahakama inapokea kielelezo hicho na kinakuwa ni kidhibiti cha 14.View attachment 2047560
MICHONGO

1639758020853.png
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom