Mwimbaji wa R&B, Robert Sylvester Kelly maarufu R Kelly amekutwa na hatia katika mashtaka yote yanayomkabili ikiwemo unyanyasaji wa kingono kwa Wanawake na Watoto, rushwa, utekaji nyara na biashara ya ngono.
R Kelly anadaiwa pamoja na mambo mengine anadaiwa kutumia umaarufu wake na utajiri wake kuwarubuni Wanawake kwa ahadi za kusaidia kazi zao za muziki, baadhi ya Mashuhuda (Waathirika) wameiambia Mahakama kwamba walikuwa chini ya umri wakati wakinyanyaswa kijinsia na R Kelly.
Hukumu ya R Kelly inatarajiwa kutolewa May 04,2022 na huenda akahukumiwa kifungo cha miaka 10 au kifungo cha maisha gerezani.
Kampuni ya Facebook ambayo inamiliki pia Mtandao wa Instagram imetoa taarifa leo Jumatatu September 27,2021 ya kwamba imesitisha kwa muda mpango wa kutengeneza Instagram version maalumu kwa ajili ya Watoto wenye umri chini ya miaka 13 kufuatia Wazazi na Wanaharakati kusema Instagram zitawaharibu Watoto.
Mkuu wa Instagram Adam Mosseri amesema mpango wao umeeleeweka vibaya na kusema hawakuwa na lengo la kuja na Instagram kama wanazotumia Watu wazima ila walipanga kuitambulisha Instagram ambayo ingewapa mafundisho Watoto na kuwapa elimu za masuala mbalimbali yasiyokiuka maadili.
"Wote tunajua Watoto wadogo wanamiliki simu Duniani kote na wanapakua Application zenye mambo ya kikubwa sisi tulipanga kuwaletea Application inayoendana na umri wao ambayo pia Wazazi wangekuwa na uwezo wa kuwafuatilia"
"Kwakuwa Watu wamekosoa na kuja juu tunasimamisha kwa muda mpango huu lakini tutakutana na Wazazi, Watunga Sheria, Watunga Sera na Wadau mbalimbali ili tuwaelimishe zaidi kuhusu hili"
Rais Samia amemuapisha Balozi Mteule Togolani Idriss Mavura kuwa Balozi wa Tanzania nchini Korea Kusini na pia amemuapisha Mathew Kilama kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, shughuli za uapisho zimefanyika leo Ikulu ya Chamwino Dodoma.
Watengenezaji wa chanjo ya Covid 19 aina ya Pfizer - BioNTech wamesema wana mpango wa kuomba kibali cha kuruhusu chanjo hiyo kutumiwa na Watoto wenye umri wa chini ya miaka 12 kufuatia ripoti za Watoto pia kuugua Covid 19.
Kwa mujibu wa ripoti iliyochapishwa na American Academy of Pediatrics wastani wa Watoto 266 hulazwa Hospitali ndani ya Wiki moja nchini Marekani kwa kuugua Covid 19.
Kwa sasa baadhi ya Nchi ikiweno Uingereza zimeruhusu Watoto kuanzia umri wa miaka 12 kwenda juu kupewa chanjo baada ya maambukizi kwa Watoto kuongezeka huku kufunguliwa kwa Shule kukichangia kuambukizana.
Vinyozi katika mkoa wa Helmand nchini Afganistan wamepigwa marufuku na Wapiganaji wa Taliban kutowanyoa au kuwapunguza ndevu wanaume wakisema hatua hiyo inakiuka sheria ya Kiislamu.
Vilevile wamepiga pia marufuku saluni, madukani na maeneo mengine kusipigwe miziki “Kinyozi yeyote akikutwa anamnyoa Mtu ndevu au kupiga miziki ataadhibiwa vikali na hatokuwa na haki ya kulalamika"
Rais Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa wajumbe watatu kujaza nafasi katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kama ifuatavyo:
1. Asina Abdillah Omar ambaye ameteuliwa kwa kipindi cha pili kuendelea na majukumu ya tume baada ya kipindi chake cha kwanza kumalizika Septemba 15, 2021.
2. Magdalena Rwebangira kutoka Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS)
3. Jaji Jacob Mwambengele, ambaye ni Jaji wa Mahakama ya Rufani.
Uteuzi wa viongozi hao umeanza Septemba 14 mwaka huu.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amelielekeza Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kuanza msako wa kuwabaini na kuwakamata wezi wa vifaa vya magari na vibaka na kuwachukulia hatua kali za kisheria.
Makalla ametoa maelekezo hayo leo Septemba 27, 2021 wakati wa kikao cha tathimini ya ziara yake ya kusikiliza migogoro jimbo kwa jimbo ambapo amesema kumeanza kuibuka vitendo vya wizi na kuleta taharuki kwa wananchi jambo ambalo hawezi kulifumbia macho.
Rais wa Korea Kusini, Moon Jae-in amepiga marufuku ulaji wa nyama ya mbwa leo (Jumatatu), ofisi yake imesema, ikizungumzia utamaduni huo ambao umekuwa kero kwa jumuiya ya kimataifa.
Nyama hiyo imekuwa sehemu ya vyakula vya Korea Kusini, huku karibu mbwa milioni moja wakiaminika kuliwa kila mwaka, lakini matumizi yameporomoka katika miaka ya karibuni kutokana na watu kuanza kuchukulia wanyama hao kama marafiki badala ya mifugo.
Utamaduni huo sasa ni mwiko miongoni mwa kizazi kipya, huku shinikizo likiongezeka kutoka kwa wanaharakati wa haki za wanyama.
Bodi ya ligi ya Afrika Kusini (PSL) imeomba radhi kwa Chama cha soka Afrika Kusini (SAFA) kwa kitendo cha Maofisa wake kumzuia Kocha wa timu ya Taifa (Bafana Bafana) kuingia uwanjani kutazama mchezo kati ya Orlando Pirates na Mamelodi Sundowns
PSL wamekiri wazi kulikuwa na makubaliano ya Mwalimu kuingia viwanjani kutazama mechi bila vikwazo na watafuatilia kwa karibu kuhakikisha haijirudii
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.