Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mkataba mwingine kwa mabingwa wa nchi wa udhamini kutoka kampuni ya Africarriers (africarriers.limited) wenye thamani ya Tsh. 800 milioni.

Mdhamini atatoa mabasi matatu;
Basi moja litatumiwa na Simba Senior Team
Basi la pili litatumiwa na Simba Queens
Basi la tatu litatumiwa na timu ya vijana (Simba Youth)

Nembo (logo) ya Africarriers itawekwa mbele kwenye jezi za timu ya vijana (Simba Youth) na begani kwenye jezi za Simba Queens.

Africarriers ni kampuni ambayo inajihusisha na biashara ya kuuza na kukopesha magari nchini.

NguvuMoja
Screenshot_20210924-201401_Instagram.jpg
Screenshot_20210924-201425_Instagram.jpg
Screenshot_20210924-201450_Instagram.jpg
Screenshot_20210924-201508_Instagram.jpg
 
“Wiki iliyopita tulisaini na Air Tanzania (@airtanzania_atcl) kama Official Airline Partner na leo tumesaini na Africarriers (@africarriers.limited) kama Official Road Transport Partner.”- Mtendaji Mkuu Barbara Gonzalez (@bvrbvra).

Neno moja kwa CEO wa mabingwa NguvuMoja
Screenshot_20210924-201800_Instagram.jpg
 
Club ya Simba leo imeingia mkataba wa miaka minne wa udhamini na kampuni ya Africarriers ambapo una thamani ya Tsh milioni 800.

Mkataba huo ambao umesainiwa mbele ya CEO wa Simba SC Barbara Gonzalez na mlezi wa Simba Queens Fatema Dewji utawezesha Simba SC, Simba Youth na Simba Queens kupewa mabasi matatu mapya.
Screenshot_20210924-201425_Instagram.jpg
 
Shirikisho la soka nchini (TFF) kwa kushirikiana na Kitengo cha Elimu ya Afya kwa Umma limetoa tiketi za bure kwa ajili kutazama mechi ya ngao ya jamii kati ya Simba na Yanga kesho Jumamosi ambapo tiketi hizo za bure ni maalum kwa Mashabiki 100 wa kwanza wataokubali kuchanja chanjo ya covid 19 palepale uwanjani.
Screenshot_20210924-202300_Instagram.jpg
 
Club ya Yanga SC imemtangaza Kocha wao wa zamani Mwinyi Zahera kuwa Mkurugenzi wa Maendeleo ya soka la vijana huku wakimtangaza pia Cedric Kaze Raia wa Burundi kuwa Kocha wao msaidizi.
Screenshot_20210924-202429_Instagram.jpg
Screenshot_20210924-202448_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom