Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kinda Eduardo Camavinga ametimiza ahadi yake ya kuwapa jezi 166 za Real Madrid kwa wafanyakazi wote wa klabu ya Rennes

Thamani ya jezi hizo ni EURO 15,000 jumla
Screenshot_20210928-044350_Instagram.jpg
 
"Kutokana nafasi yangu ninayocheza jukumu la kwanza ni kufunga kwahiyo moyoni nina malengo hayo ya kuhakikisha nafunga na kuisaidia timu yangu nashukuru hilo limeanza kutimia."

- Fiston Mayele.
Screenshot_20210928-044718_Instagram.jpg
 
MUKOKO, SAIDO WABAKI DAR
.
Yanga inatarajia kuwakosa nyota wake wanne kwenye mchezo dhidi ya Kagera Sugar, wachezaji ambao wamebaki Dar es Salaam, Yassin Mustafa, Balama Mapinduzi, Saido Ntibazonkiza, Mukoko Tonombe na Dickson Ambundo.
.
“Wachezaji waliobaki watatu hawapo fiti, Mukoko anaendelea kutumikia adhabu ya kadi nyekundu.” amesema Meneja wa Yanga, Saleh Hafidh
Screenshot_20210928-044911_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

MUTSHIMBA MUGALU, HITAJI LA DUNIA YA SASA

Niliwahi kuhoji kwanini Pep Guardiola alimuhusudu sana Gabriel Jesus mbele ya lethal Striker kama Sergio Kun Aguero! Niliwahi kumshangaa Pep kwanini amkatae Etoo na kumuamini Messi

Nikaja pia kujiuliza kwanini Chris Mugalu anapata sana nafasi ndani ya Simba?? Kwanini anawaweka nje Meddie Kagere na John Bocco? Hili swali liliwahi kunisumbua sana

Awali ya yote nikaja kufanya homework yangu kwanza ya kuugawa uwanja! Kwenye nusu mbili, Nusu ya kwanza ni ZONE A chini ya mstari, huku ni BASIC FOOTBALL, mpira wa maelekezo zaidi na kujilinda

Juu ya mstari ambayo nimeiita ZONE B ni sehemu ya Creativity (Ubunifu) na Tactical Flexibility (Mnyumbuliko wa kimfumo na kimbinu) hii ndio sehemu ambayo unahitaji akili kama ya Mugalu mtu anaekupa vingi kwa pamoja

Manchester City pale Guardiola alimkataa Aguero kwakuwa licha ya kuwa ni Mfungaji bora ila haipi timu balance, hakabi, hachezeshi na hashuki! Lakini Jesus anakupa vyote na una uhakika yoyote atafunga kama yeye hatofunga

Ndipo hapo nakuja kumtazama MUGALU na ile concept ya STRIKER VS FORWARD! Dunia ya sasa inahusudu zaidi Forward kuliko Straika! Kwangu Mugalu ni Forward mzuri, Bocco na Kagere ni Masteika wazuri

Mugalu ni mzuri kwenye Link Up plays, kuwachezesha wengine na kuhakikisha nafasi zinapatikana na kubwa zaidi ni uwezo wake wa pressing hivi vinamfanya awe na vitu vya ziada kwa Mwalimu, ukiwa nae una uhakika kama sio yeye basi yoyote atafunga

Ni kawaida kwasasa kuona Heat Map ya Mugalu ni kubwa kuliko wachezaji wote ndani ya Simba kutokana na kuwa mchezoni muda wote! Na hata suala la kukosa mabao ndicho pia Gabriel Jesus pale City alilaumiwa nacho

Hii inatokana na uwezo wao mkubwa wa kukaa kwenye njia kila wakati na wanaonekana wanakosa zaidi kwakuwa wapo mchezoni muda wote na wanazijua njia muda wote

Mimi namuamini Chris Mugalu, kimfumo anailipa sana timu
Screenshot_20210928-045018_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

PEP GUARDIOLA NA SIMULIZI YA SIR ALEX FERGUSON

Bado macho yangu ni makavu! Usiku wa saa nane wakati sauti ya bundi na milio ya wadudu usiku, naendelea kupitia kitabu cha ANOTHER WAY OF WINNING cha Pep Guardiola

Asubuhi moja ya kijua cha kiangazi Septemba 10,2010 kwenye majengo ya shirikisho la soka barani Ulaya (UEFA) pembezoni mwa Ziwa Geneva, Uswisi! Kwenye kikao cha mwaka cha Makocha, Pep alipata bahati kubwa

Licha ya kuwa alimfunga Ferguson na United yake fainali ya UEFA 2009 Ila kwake alimuhusudu sana Fergie na ni kawaida yake kupenda Makocha wazee kama ilivyo Marcelo Bielsa ambae yeye kwake ndio Godfather

Pep yeye akiwa Kijana Mdogo bado aliona ndio muda sahihi wa kukaa na Sir Alex na kujadili mpira, wakiwa wameketi, Pep akawa anamsikiliza Fergie akimpa tactical trends za Ulaya nzima, maana Babu alikuwa Mtaalam mno wa mifumo

Pep aliendelea kuketi kama Kijana mtiifu mwenye ndoto kubwa, akimsikiliza Babu akipangua vihendo kuanzia kwa Arrigo Sacchi, Bobby na mafundi wengi wa soka! Kazi ya Pep ilikuwa ni kuongeza kahawa tu kwenye kikombe cha Fergie

Kumbuka ni Pep Guardiola huyo ambaye tayari ametwaa ubingwa wa Ulaya mbele ya Fergie na United yake ila bado anatumia muda wake kujifunza, haringi kabisa maana kila muda kwake yeye ni football tu

Kwakuwa Nyon iligubikwa na Makocha wakubwa wengi, Pep ndio kwanza alikuwa anachipukia hivyo alionekana Mtoto pale! Alikuwepo Mourinho alimtoa Pep Nusu UEFA 2010, Carlo Ancelotti, Claudio Ranieri, Babu Fergie na wengine

Wakati wapo Makocha wakubwa wamejikusanya wanajadili kabla ya kurudi kikaoni, Pep akajitoa pale na kujisogeza pembeni Kwakuwa alikuwa anajiona mdogo na hawezi kuongea kitu mbele ya Magwiji

Wakati Pep kajitenga pembeni, Jose Mourinho alimuona, ikabidi Mourinho atoke kwenye lile kundi na kwenda kupiga nae stori maana alikuwa mwenyewe kajitenga, wana kisa chao hawa kumbuka

ITAENDELEA....
Screenshot_20210928-045259_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

NJE YA 18 SPECIAL - SIMBA VS YANGA

Kwanza wafanye Shomari Kapombe na Mohamed Hussein wasicheze! Ni kuizima ile overlaping fullback style kisha hii itasaidia kupoteza numerical superiority, ndio silaha ya Simba

Kocha wa Yanga akamuweka Farid Mussa kule kwa Kapombe, wote wanakimbia sana! Kumfanya Shomari asipande kabisa, kisha akamuweka Moloko kwa Zimbwe asicheze

Simba wakapoteza option ya kwanza ya mchezo! Wakaopt plan B sasa! Nayo ni kucheza kupitia kati! Three man Midfielders, Kanoute, Lwanga na Bwalya

Kocha wa Yanga alijua hilo! Akaja na double pivot ya Khalid Aucho na Yannick Bangala! Kisha akampa Feisal Salum ile free role! Hapo amempa homework Lwanga kucheza na Feisal, Simba wakapoteana

Yanga wakajua ili Simba wacheze wanataka nafasi! Basi walichojaribu kufanya Yanga ni kulinda shape yao wakati wa pressing! Yannick alikuwa anarudi kuwa defender wa tatu, kuhakikisha nafasi haipo

Gameplan ya Simba ilifeli kutokana na vitu viwili! Basics per Creativity zone! Kwenye zote ya kukaba (Basics) Simba walijitahidi sana ila zone ya juu kushambulia (creativity) walikosa silaha ya kupasua ngome

Midfield battle! Maestro Feisal alikuwa katika ubora mkubwa sana, alikuwa mwepesi kwenye kusaka eneo na kutoa pass kwa eneo, alikuwa anapiga progressive passes, hakuwa anarudi nyuma! Fast going

Dickson Job, ni kama mzoefu sana wa Derby ila hapana! Ni kinda tu ila anafanya makubwa sana! Ni beki pekee mwenye uwezo wa kucheza zonal, man to man na combined marking! He was superb

Itafika siku Chris Mugalu ataanza kuhukumiwa kwa takwimu, itafika siku watu watamtaka afunge sasa! Amepata chance nyingi ila hakuzitumia, nafikiri anapaswa kuongeza umakini
Screenshot_20210928-045553_Instagram.jpg
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amelielekeza Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kuanza msako wa kuwabaini na kuwakamata wezi wa vifaa vya magari na vibaka na kuwachukulia hatua kali za kisheria.

Makalla ametoa maelekezo hayo leo Septemba 27, 2021 wakati wa kikao cha tathimini ya ziara yake ya kusikiliza migogoro jimbo kwa jimbo ambapo amesema kumeanza kuibuka vitendo vya wizi na kuleta taharuki kwa wananchi jambo ambalo hawezi kulifumbia macho.
View attachment 1955360
Huu mchezo sijui kama dar utaisha..
 
Farhan Jr

MUTSHIMBA MUGALU, HITAJI LA DUNIA YA SASA

Niliwahi kuhoji kwanini Pep Guardiola alimuhusudu sana Gabriel Jesus mbele ya lethal Striker kama Sergio Kun Aguero! Niliwahi kumshangaa Pep kwanini amkatae Etoo na kumuamini Messi

Nikaja pia kujiuliza kwanini Chris Mugalu anapata sana nafasi ndani ya Simba?? Kwanini anawaweka nje Meddie Kagere na John Bocco? Hili swali liliwahi kunisumbua sana

Awali ya yote nikaja kufanya homework yangu kwanza ya kuugawa uwanja! Kwenye nusu mbili, Nusu ya kwanza ni ZONE A chini ya mstari, huku ni BASIC FOOTBALL, mpira wa maelekezo zaidi na kujilinda

Juu ya mstari ambayo nimeiita ZONE B ni sehemu ya Creativity (Ubunifu) na Tactical Flexibility (Mnyumbuliko wa kimfumo na kimbinu) hii ndio sehemu ambayo unahitaji akili kama ya Mugalu mtu anaekupa vingi kwa pamoja

Manchester City pale Guardiola alimkataa Aguero kwakuwa licha ya kuwa ni Mfungaji bora ila haipi timu balance, hakabi, hachezeshi na hashuki! Lakini Jesus anakupa vyote na una uhakika yoyote atafunga kama yeye hatofunga

Ndipo hapo nakuja kumtazama MUGALU na ile concept ya STRIKER VS FORWARD! Dunia ya sasa inahusudu zaidi Forward kuliko Straika! Kwangu Mugalu ni Forward mzuri, Bocco na Kagere ni Masteika wazuri

Mugalu ni mzuri kwenye Link Up plays, kuwachezesha wengine na kuhakikisha nafasi zinapatikana na kubwa zaidi ni uwezo wake wa pressing hivi vinamfanya awe na vitu vya ziada kwa Mwalimu, ukiwa nae una uhakika kama sio yeye basi yoyote atafunga

Ni kawaida kwasasa kuona Heat Map ya Mugalu ni kubwa kuliko wachezaji wote ndani ya Simba kutokana na kuwa mchezoni muda wote! Na hata suala la kukosa mabao ndicho pia Gabriel Jesus pale City alilaumiwa nacho

Hii inatokana na uwezo wao mkubwa wa kukaa kwenye njia kila wakati na wanaonekana wanakosa zaidi kwakuwa wapo mchezoni muda wote na wanazijua njia muda wote

Mimi namuamini Chris Mugalu, kimfumo anailipa sana timu
View attachment 1955368
Muda mwingine anakeraaaa huyu jamaaq
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom