

Mikono ya kihamu ya Farhan Jr
NIMEONA NINI SIMBA VS TP MAZEMBE?
Ni kwanza matokeo ya mahusiano! Nilisema kwenye NETWORKING wiki kadhaa nyuma! Nikasema CLUBS VS CLUBS (klabu dhidi ya Klabu)
Wakati CEO wa Simba alipiga picha na Mmiliki wa TP Mazembe ambae pia ni Makamu Mwenyekiti wa klabu duniani, Moise Katumbi Chapwe! Ni sehemu ya kujenga mahusiano yao
Mazembe aliwahi kuja nchini kwa SIMBA SUPERCUP! Sio rahisi kuileta klabu Tajiri nchini kwetu na ikacheza michuano bali ni matokeo ya mahusiano yenu mazuri
Niwape mifano ya duniani kote kuna mechi nyingi zinachezwa kuelekea msimu mpya kama ambavyo Simba Day wanayo yao hapa nchini
FC Barcelona wana mechi ya kombe inafahamika kama JOAN GAMPER ama JOAN GAMPER TROPHY! Mechi zao zinahusisha timu ambazo wao wana mahusiano nayo tu na sio timu ambazo hawana link nazo
Msimu huu wamecheza na Juventus, wana mahusiano mazuri sana tangu EUROPEAN SUPERLEAGUE! Licha ya kuwa Juventus hakuwa na msimu mzuri ila bado ni Juventus
Hakuna michuano nje ya inayoandaliwa na Mashirikisho ikahusisha watu ambao hawana mahusiano! Kuna Audi Cup ya Bayern Munich, kuna Emirates Cup ya Arsenal zote zinahusisha wale wenye mahusiano
Simba kumleta TP Mazembe nadhani ni hatua kubwa licha ya kuwa hawakuwa vizuri msimu uliopita lakini bado ni TP MAZEMBE tusisahau
TP MAZEMBE ipo nchini Morocco kwasasa, tayari hao Mazembe tunasema wabovu lakini wamecheza mechi na miamba WYDAD CASABLANCA, hao hao Mazembe tunaosema wabovu wanaanza hatua ya pili Klabu bingwa Afrika
Hao Mazembe tunaosema ni wabovu ila wapo nafasi ya tano kwa ubora Afrika wakiwa na points 1572, Mazembe tunaosema wabovu wamebeba Ligi ya Congo mara tatu mfululizo mpaka sasa
Wabovu hiyo kwioo??


View attachment 1929248