Makapuku Forum

Makapuku Forum

Yanga SC imetangaza rasmi kuwa katika mchezo wa Jumapili itawakosa Fiston Mayele, Shaban Djuma waliojiunga nao kutokea AS Vita ya Congo DR pamoja na Khalid Aucho kutokana na ITC zao kuchelewa kufika kabla ya usajili wa CAF kufungwa.

“Achana na habari za porojo eti Yanga inadaiwa ndio maana wachezaji wake watatu (Mayele, Aucho na Djuma) hawatocheza sababu inadaiwa, hii akili ya wapi kwa nini CAF wasizuie wachezaji wote tuliowasajili, si wangezuiwa wachezaji wote tuliowasajili, hizo ni mbinu za kututoa mchezoni” ——— Hajis manara
Screenshot_20210908-135723_Instagram.jpg
 
Jeshi la Polisi Mbeya limewaonesha (nusu picha) Watoto waliokua wameuzwa kwa shilingi elfu 25 na elfu 30 kwa Wafugaji ili wakawatumikishe kwenda kuchunga mifugo.

Imeelezwa kwamba kutokana na Watoto hao kutoonekana nyumbani kwa muda mrefu baadhi ya familia zilianza kuweka msiba zikiamini Watoto wao wamefariki.

Tayari Polisi Mbeya wanawashikilia Watu wawili kwa tuhuma hizi na kusema walikamatwa Septemba 5, 2021 saa mbili usiku katika kijiji cha Mabango, Wilayani Mbarali wakiwa kwenye harakati za kuwasafirisha Watoto hao.

Watuhumiwa hao kuwa ni Daniel Julius (21) na Kamungu Julius (30) wote Wakazi wa wilaya ya Mbarali na kwamba wanadaiwa kuwachukua Watoto 11 wanaoishi katika magumu na wengine kutoka kwa wazazi wao na kisha kwenda kuwauza.

RPC Matei amesema kuwa baada ya kuwahoji Watuhumiwa walikiri kuwa walikuwa wakimuuza kila Mtoto mmoja kwa gharama kati ya shilingi elfu ishirini na tano (sh.25,000) hadi elfu thelathini 30,000.
Screenshot_20210908-135847_Instagram.jpg
 
Bodi ya Utendaji ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) imekubali kuipa Tanzania dola za Marekani milioni 567.25 (Sh1.3 trilioni) ambazo ni msaada wa dharura kwa ajili ya kushughulikia janga la Uviko-19.

Mlipuko wa ugonjwa huo nchini umesababisha kuanguka kwa sekta ya utalii na kuongeza hitaji la ufadhili mkubwa ili kukabiliana na athari za kiafya na kiuchumi za janga hilo.

IMF iliidhinisha msaada huo wa dharura wa kifedha chini ya kituo cha mikopo ya haraka kwa lengo la kuunga mkono juhudi za mamlaka katika kukabiliana na janga hilo kwa kushughulikia gharama za haraka za kiafya, kibinadamu na za kiuchumi.
Screenshot_20210908-140304_Instagram.jpg
 
Uongozi wa Yanga umethibitisha kuwakosa wachezaji wao watatu kuelekea mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Rivers United.

Msemaji wa Yanga, Haji Manara amesema kwamba Yanga itawakosa wachezaji watatu ambao ni kiungo Khalid Aucho, beki Djuma Shaban na mshambuliaji Fiston Mayele.
Screenshot_20210908-140953_Instagram.jpg
 
Umoja wa Watemi wa Kisukuma kwa kushirikiana na Umoja wa Machifu Tanzania wamempa jina la ‘Angaya’ Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan lenye maana ya Nyota Angavu.

Akisoma hotuba leo Jumatano Septemba 8, 2021 mbele ya Rais Samia katika tamasha la Utamaduni linalofanyika Viwanja vya Msalaba Mwekundu Kisesa wilayani Magu Mkoa wa Mwanza, Katibu wa Umoja wa Machifu wa Kisukuma, Mtemi Aaroni Mikomangwa amesema jina hilo ni kutambua mchango wa Serikali anayoiongoza kwa kuthamini na kusimamia utu wa wanyonge pamoja na utamaduni wa Mtanzania.
Screenshot_20210908-141053_Instagram.jpg
 
Bunge la Jamhuri ya Muungano limepitisha muswada wa sheria unaotamka kuwa kukutwa na bangi, mirungi sasa ni kosa la jinai.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Profesa Adelardius Kilangi aliwasilisha muswada huo bungeni jana Jumanne Septemba 7, 2021 ambapo muswada umeongeza uzito wa bangi na mirungi kwenye makosa yanayosikilizwa katika Mahakama Kuu na mahakama za wilaya.

Profesa Kilangi amesema awali sheria haikutamka kama ni kosa la jinai ingawa ilizuia kitendo hicho bila kutamka jinai.
Mirungi na bangi ni miongoni mwa dawa za kulevya ambazo Serikali imekuwa ikipambana kukomesha vitendo hivyo kama ilivyo kwa dawa zingine.

"Lengo la marekebisho haya ni kupunguza mrundikano wa kesi mahakama za wilaya zinazosubiri kupelekwa Mahakama Kuu kwa ajili ya kusikilizwa," amesema Kilangi.

Amesema mbali na marekebisho ya vifungu vya 15 na 15A katika kuongeza uzito huo, kifungu cha 17 kinarekebishwa ili kufanya kuwa kosa la jinai kitendo cha kukutwa na au kutumia kiwango kidogo cha dawa za kulevya.
Screenshot_20210908-141152_Instagram.jpg
 
Siku kadhaa baada ya kusambaa kwa video mitandaoni inayowaonyesha wanafunzi wa shule ya Sekondari Makurumla iliyopo katika Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam, wakiwa wameshikwa na wazazi wao kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kujihusisha na vitendo vya kiuhalifu, Mwananchi Digital imetembelea shuleni hapo na kuzungumza na Mwalimu Mkuu, Naomi Alimosa Mwasangopole ambaye amewakataa wanafunzi hao akieleza kuwa walishafukuzwa kwa utovu wa nidhamu ikiwemo kujihusisha na kuvuta bangi, wizi pamoja na ngono zembe
Screenshot_20210908-141311_Instagram.jpg
 
Zikiwa zimetimia siku 74 tangu ilipojulikana kutoweka kwa askari Emmanuel Govela, Jeshi la Polisi mkoani hapa limesema uchunguzi wake umekuwa mgumu na wanamchukulia ni mtoro kazini.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Onesmo Lyanga alisema jana kuwa kazi ya kumtafuta Govela (39) ambaye taarifa za kutoweka kwake zilijulikana Juni 26, 2021 imekuwa ngumu kwa upande wao kutokana na mazingira ya tukio lenyewe.

Lyanga alisema wanamchukulia Govela ni mtoro kazini kwa sababu aliondoka bila utaratibu.

Aliwaomba wote wanaofahamu na kumuona askari huyo watoe taarifa ili waone jinsi ya kushirikiana nao kuhoji.
Soma zaidi gazeti la Mwananchi
Screenshot_20210908-141426_Instagram.jpg
 
INASEMEKANA

Klabu ya Yanga inaweza ikawakosa wachezaji wake watatu beki wa kulia Shaban Djuma, Beki wa kati Yannick Bangala na Kiungo wa kati Khalid Aucho kwenye mchezo wa awali wa Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF Champions league) dhidi ya Rivers United ya Nigeria September 12 kutokana na kuchelewa kupata ITC zao.
Screenshot_20210908-142050_Instagram.jpg
 
Banda kukipiga Mtibwa Sugar
.
Beki Abdi Banda aliyekuwa anacheza soka la kulipwa nchini Afrika kusini katika klabu ya Highlands Park ameonekana akiwa katika mazoezi ya timu ya Mtibwa Sugar inayoshiriki Ligi Kuu nchini.
.
Banda ameoneonekana katika fukwe ya bahari Coco Jijini Dar es Salaam sambamba na wachezaji wenzake wakiendelea na mazoezi.
.
Banda amesema alikuwa ajiunge na
klabu ya Ajax Capetown lakini akiwa kwenye harakati za kujiunga na klabu hiyo aliugua Uviko 19.
Screenshot_20210908-143329_Instagram.jpg
 
Yanga SC imetangaza rasmi kuwa katika mchezo wa Jumapili itawakosa Fiston Mayele, Shaban Djuma waliojiunga nao kutokea AS Vita ya Congo DR pamoja na Khalid Aucho kutokana na ITC zao kuchelewa kufika kabla ya usajili wa CAF kufungwa.

“Achana na habari za porojo eti Yanga inadaiwa ndio maana wachezaji wake watatu (Mayele, Aucho na Djuma) hawatocheza sababu inadaiwa, hii akili ya wapi kwa nini CAF wasizuie wachezaji wote tuliowasajili, si wangezuiwa wachezaji wote tuliowasajili, hizo ni mbinu za kututoa mchezoni” ——— Hajis manara View attachment 1929184

Wameanzaa
 
KOEMAN KUPEWA DILI NOU CAMP
.
Rais wa Barcelona, Joan Laporta amesema wamempa ofa ya mkataba mpya Kocha Ronald Koeman licha ya miamba hiyo ya Nou Camp kuanza msimu kwa mwendo wa kusuasua.
.
Koeman, 58, amebakiza muda usiofikia mwaka mmoja kwenye mkataba wake wa sasa huko Nou Camp baada ya kusaini miaka miwili alipotua klabuni hapo mwaka 2020.
.
Baada ya mkataba wake kubaki siku chache, bosi Laporta hataki kuwafanya mastaa wa Barca kumdharau kocha huyo Mdachi kutokana na kuwa na mkataba mfupi kwa maana hana uwezo na ndio maana hapewi dili jipya.
.
Laporta amesema: “Koeman nitamsapoti kwa kila kitu, namheshimu na nina uhakika atafanya kazi kwa raha kwa kadri inavyowezekana.
Screenshot_20210908-144038_Instagram.jpg
 


Mikono ya kihamu ya Farhan Jr

NIMEONA NINI SIMBA VS TP MAZEMBE?

Ni kwanza matokeo ya mahusiano! Nilisema kwenye NETWORKING wiki kadhaa nyuma! Nikasema CLUBS VS CLUBS (klabu dhidi ya Klabu)

Wakati CEO wa Simba alipiga picha na Mmiliki wa TP Mazembe ambae pia ni Makamu Mwenyekiti wa klabu duniani, Moise Katumbi Chapwe! Ni sehemu ya kujenga mahusiano yao

Mazembe aliwahi kuja nchini kwa SIMBA SUPERCUP! Sio rahisi kuileta klabu Tajiri nchini kwetu na ikacheza michuano bali ni matokeo ya mahusiano yenu mazuri

Niwape mifano ya duniani kote kuna mechi nyingi zinachezwa kuelekea msimu mpya kama ambavyo Simba Day wanayo yao hapa nchini

FC Barcelona wana mechi ya kombe inafahamika kama JOAN GAMPER ama JOAN GAMPER TROPHY! Mechi zao zinahusisha timu ambazo wao wana mahusiano nayo tu na sio timu ambazo hawana link nazo

Msimu huu wamecheza na Juventus, wana mahusiano mazuri sana tangu EUROPEAN SUPERLEAGUE! Licha ya kuwa Juventus hakuwa na msimu mzuri ila bado ni Juventus

Hakuna michuano nje ya inayoandaliwa na Mashirikisho ikahusisha watu ambao hawana mahusiano! Kuna Audi Cup ya Bayern Munich, kuna Emirates Cup ya Arsenal zote zinahusisha wale wenye mahusiano

Simba kumleta TP Mazembe nadhani ni hatua kubwa licha ya kuwa hawakuwa vizuri msimu uliopita lakini bado ni TP MAZEMBE tusisahau

TP MAZEMBE ipo nchini Morocco kwasasa, tayari hao Mazembe tunasema wabovu lakini wamecheza mechi na miamba WYDAD CASABLANCA, hao hao Mazembe tunaosema wabovu wanaanza hatua ya pili Klabu bingwa Afrika

Hao Mazembe tunaosema ni wabovu ila wapo nafasi ya tano kwa ubora Afrika wakiwa na points 1572, Mazembe tunaosema wabovu wamebeba Ligi ya Congo mara tatu mfululizo mpaka sasa

Wabovu hiyo kwioo??

Screenshot_20210908-144256_Instagram.jpg
 


Mikono ya kihamu ya Farhan Jr

Klabu zote Kusini mwa Jangwa la Sahara ni FEEDER CLUBS kwa miamba huko Kaskazini mwa Afrika ambazo tunaziita BIG CLUBS

Kwenye kila msimu ukifanya vizuri una uhakika wa kuuza Wachezaji wengi muhimu kuelekea klabu hizo kubwa, hapo lazima uwe na PLAN B

Kwenye dirisha hili la usajili Simba wameuza Clatous Chama na Luis Miquisson, lakini fahamu kuwa hata Rally Bwalya alikuwa mbioni kuondoka ijapo haijatimia

Simba wamefanya kitu gani kuendana na kasi ya Wachezaji wake kuondoka kwenda kwenye malisho makubwa zaidi? Ndipo hapo kuna kitu klabu zote FEEDERS duniani wanafanya

Tutazame kitu kuhusu SIMBA VS AGENCIES! Niliwahi kusema mahusiano ya Simba na Kampuni kubwa za Uwakala barani Afrika umewapa malipo makubwa sana, ikiwemo kuchukua wachezaji kwa bei ndogo na kuuza kubwa

Ndio maana kuelekea Pre Season na dirisha la Usajili Simba walipokea maombi ya wachezaji 74 Afrika nzima hii wakitaka kujiunga na Simba, ila sote tunafahamu Simba bado hana scouting network kubwa Afrika, hivyo jicho lake ni AGENCIES

Wao wanaona sehemu kubwa Afrika, wamewaletea vijana wengi wadogo sana ambao wanafahamu baada ya muda itakuwa biashara kubwa! Simba itafaidika, wao watafaidika na Mchezaji atafanikiwa

Kwanini Simba hawakutangaza wapi wanaenda wachezaji wao, Chama na Miq mapema? Lakini ni kwenye eneo hili la mahusiano kati ya Klabu, Wakala na Klabu anayoenda! EXCLUSIVITY ni kanuni ya kibiashara, Simba walikubali kutunza siri kwa engo ya kuitazama Kesho yao kibiashara

Al Ahly walipofika muda wao wakamtangaza Miquisson, Berkane ulipofika muda wao wakamtangaza Chama, hii ndio BUSINESS PERSPECTIVE, usinyee kambi

Simba wao wanafahamu ukweli kuwa Afrika ina Wachezaji wengi bora tena wa bei nafuu, ila unahitaji macho ya AGENCIES wakuletee kitu hicho, ndio maana wapo nao karibu
Screenshot_20210908-144515_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom