Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kamanda wa Kikosi cha Usalama barabarani nchini SACP Wilbroad Mutafungwa amemfungia leseni Dereva wa Basi la kampuni ya Sauli kwa muda wa miezi sita kutokana na kitendo chake cha kuyapita magari mengine bila kuchukua tahadhari (Wrong Overtake) asubuhi leo akielekea Tunduma kutokea Dar na kusababisha ajali na Watu wanne kujeruhiwa.

Mutafungwa amesema kitendo hicho kilichofanywa na Dereva huyo ni ukiukwaji wa sheria za usalama barabarani na ameeleza kuwa Dereva huyo atatakiwa kukaa bila leseni kwa muda wa miezi sita na kurudi tena darasani. View attachment 1905552View attachment 1905553
Aiseee
 
Mwili wa Mchambuzi wa soka aliyekua akifanya kazi na TBC Theogenes Alexander Kashasha maarufu kama Mwalimu Kashasha umezikwa leo kwenye makaburi ya Kinondoni Dar es Salaam, Kashasha alizaliwa 17 november 1957 na alifariki August 19 2021. RIPTeacher
Screenshot_20210824-053528_GBInsta.jpg
Screenshot_20210824-053642_GBInsta.jpg
 
Kamanda Mstaafu Kanda Maalum ya Dar es saalaam Kamishna Suleiman Kova leo kwenye Amplifaya ya Clouds FM ameelezea tukio la Mbunge wa Kawe Askofu Josephat Gwajima kuomba kubadilisha kiti na microphone vilivyokua vimeandaliwa kwa ajili yake kuvitumia wakati akihojiwa na Kamati ya Bunge Dodoma, Kova ameelezea tukio kama hili kwa kutumia uzoefu wake akiwa Polisi na kuhoji Watu mbalimbali wenye tuhuma.

"Wakati mwingine Mtu akishafanya jambo flani anakuwa na hisia flani ambazo sio za kawaida labda anafikiri nikikaa hapa naweza nikadhurika, ni tatizo la kisaikolojia kwa Mtu ambae ana msongo wa mawazo anakuwa hajiamini na haamini Mtu yeyote yule, kwahiyo anaweza kufanya jambo lolote lile”

"Mfano mimi zamani nilikua nahoji Wahalifu, akiletwa kwangu akisikia ni Kova anapoingizwa mule ndani anadondoka chini paap bila kumgusa, yani anaona amekutana na kitu cha hatari sana kutokana na yeye anavyoelewa, kama ni madhambi anayakumbuka yote" ——— Kamanda Mstaafu Kanda Maalum Dar es salaam Kamishna Suleiman Kova. View attachment 1905546
Kama ikitekelezeka itakuwa imekaa vizuri
 
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na wenzake wameiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwamba watamtumia aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Simon Sirro kama Mashahidi wao wakati wa usikilizwaji wa kesi hiyo katika Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi maarufu “Mahakama ya Mafisadi".

Hayo yamebainishwa na Wakili wa Mbowe na wenzake, Peter Kibatala baada ya kesi hiyo kuletwa chini ya hati ya dharura leo huku Washtakiwa hao wakisomewa mashitaka upya na kufikia mashtaka saba ikiwemo la kutaka kumdhuru Sabaya.

Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba anayesikiliza kesi hiyo amesema kwamba mchakato wa kesi hiyo kwenda Mahakama ya Mafisadi umekamilika.
Screenshot_20210824-053811_GBInsta.jpg
 
Baada ya Yanga kusitisha kambi nchini Morocco ambayo ilibidi imalizike Agosti 27 uongozi umetoa taarifa rasmi kuwa maandalizi yao ya msimu ujao yataendelea Avic Town iliyopo Kigamboni jijini Dar es Salaam. Pia wamesema jezi mpya zitatambulishwa Jumatano Agosti 25 kuelekea kilele cha Wiki ya Mwananchi Agosti 29
Screenshot_20210824-055015_GBInsta.jpg
 
Mwanaume huyu anaitwa Gerard Moreno yuko pale Villarreal, moja kati ya wakata vyavu hodari sana pale LA LIGA

Kwenye penati ni hatari, amefunga mabao 11 ya penati msimu uliopita

Ingali silaha yake kubwa ni mbio akiwa na mpira, very fast
Screenshot_20210824-055232_GBInsta.jpg
 
Manchester United chini ya OGS, wenyewe wana imani nae sana kuwa atawafikisha sehemu

Ila bado United imekuwa na vipindi tofauti, maji kupwa maji kujaa!

Wanaamini kuwa Sir Alex Ferguson alipitia kama haya, huenda atafikia alipofika Ferguson
Screenshot_20210824-063849_GBInsta.jpg
 
Jules Kounde CHELSEA
.
Chelsea ipo kwenye hatua nzuri katika mazungumzo na wawakilishi wa Sevilla ili kuipata saini ya beki wa timu hiyo na Ufaransa, Jules Kounde, 22, katika dirisha hili na inatarajiwa kukamilisha dili hilo kwa kuwaruhusu Davide Zappacosta, 29, Kurt Zouma, 26, na Ike Ugbo, 22, kuondoka ili kupata pesa kutokana na mauzo yao.
Screenshot_20210824-065100_GBInsta.jpg
 
JUST IN | Mabingwa wa England, Manchester City wamethibitisha kuwa watatambulisha SANAMU la David Silva na Vincent Kompany nje ya Uwanja wa Etihad kabla ya mechi dhidi ya Arsenal Jumamosi hii.
Screenshot_20210824-065712_GBInsta.jpg
 
Beki wa zamani wa Barcelona Jean-Clair Todibo:

"Nikiwa Barcelona, hatukuruhusiwa kumgusa Messi kwenye mazoezi. Tuliambiwa kukaa mbali na yeye lakini ni sawa tu. Yeye ndiye GOAT. Hutakiwi kumjeruhi. "

Screenshot_20210824-065929_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom