Makapuku Forum

Makapuku Forum

Sheffield United inakumbana na upinzani mkubwa kutoka kwa Atalanta katika harakati za kuiwania saini ya winga wa Manchester United na Ivory Coast, Amad Diallo, 19, kwa mkopo katika dirisha hili. Diallo ni miongoni mwa wachezaji ambao Man United ina mpango wa kuhitaji kuwauza katika dirisha hili.
Screenshot_20210822-125204_GBInsta.jpg
 
“Naomba niweke wazi Wananchi wasiwe na taharuki nyumba za Vijijini haziko katika mpango wa kutozwa kodi ya majengo vilevile nyumba zilizojengwa kwa vifaa ambavyo sio vya kudumu kama zile udongo zilizoezekwa kwa nyasi hazihusiki na kodi ya majengo"

“Kodi ya majengo ni kodi ambayo inatozwa kutokana na maendelezo juu ya ardhi, mara nyingi Watu wanaichanganya na kodi ya ardhi, hii kodi ya ardhi inalipwa kule Wizara ya ardhi kodi ya pango la ardhi ni ardhi ambayo haina chochote au ina jengo juu yake, kodi ya jengo ni yale maendelezo juu ya ardhi ndio inayolipwa kwa sasa"

“Na kodi hii mwanzoni ilikuwa ikikusanywa na wenzetu wa Local Government na baadae ikahamishiwa TRA na wakati tunaanza kuikusanya utaratibu ulikuwa tofauti kidogo ilikuwa jengo linathaminishwa alafu inatozwa kwa asilimia fulani ya hiyo thamani ya jengo"

“Kiukweli utaratibu huu ulikuwa na usumbufu sana utakuta nyumba zilizothaminishwa zinakuwa ni chache ukilinganisha ambazo hazijathaminishwa, utakuta mtaa mwingine nyumba yake imethaminishwa analipa asilimia na mwingine nyumba yake haijathaminishwa analipa Tsh. Elfu 10 "——— asema Mkurugenzi wa Huduma na Elimu Kwa Mlipakodi Richard Kayombo kwenye Clouds360 ya Clouds Tv
Screenshot_20210823-144156_GBInsta.jpg
 
“Viwango vya kodi ni Tsh. 12,000 kwa mwaka kwa nyumba ya kawaida na itakuwa inalipiwa 1000 kwa mwezi na ghorofa ni Tsh. 60,000 kwa kila sakafu kwa mwaka ambapo italipiwa 5000 kwa kila sakafu kwa mwezi”

"Lengo sio kuwaumiza wapangaji ni kulinda tozo kwa njia rahisi bila ya kuwabugudhi Wapangaji"

“Wananchi wanapolipa kodi ni sharti wajulishwe kwamba kodi imekwenda kufanya nini? kwa sababu Wananchi wanauliza kwanini walipe kodi? wanalipa kodi kwa sababu inaenda kuleta maendeleo"

“Wananchi wakielezwa vizuri huwa wanaelewa sana wanakubali na wanalipa lakini wakiona inatumika vibaya utawakatisha tamaa wasijikie vizuri na kuwa wagumu wa kulipa"———Richard Kayombo, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu Kwa Mlipakodi via Clouds360 ya Clouds TV
Screenshot_20210823-144453_GBInsta.jpg
 
Wafanyakazi watano wa Mamlaka ya Mapato (TRA) Azaria (Dereva), Joel Mitondwa, Said Budi, Bernard Mushingi na Vahadi Hassan wamefariki kwa ajali ya gari katika eneo la Hanseketwa Old Vwawa Wilayani Mbozi Mkoani Songwe leo asubuhi.

Wafanyakazi hao ni kikosi kazi cha Fast Track na wamefariki wakiwa wanafukuzana na gari walilokua wanadhani limebeba bidhaa za magendo (halipo kwenye picha), Kamanda wa Polisi Mkoani Songwe, Janeth Magomi amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo leo asubuhi.
Screenshot_20210823-144634_GBInsta.jpg
Screenshot_20210823-144651_GBInsta.jpg
Screenshot_20210823-144711_GBInsta.jpg
Screenshot_20210823-144726_GBInsta.jpg
Screenshot_20210823-144741_GBInsta.jpg
 
Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe na wenzake watatu wamesomewa mashitaka sita ikiwemo la kutaka kumdhuru aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai wakati huo, Lengai Ole Sabaya.

Pia inadaiwa Freeman Mbowe alituma kiasi cha shilingi laki sita kwa Washitakiwa wenzake kwa ajili ya kufanya maandalizi ya vitendo vya Ugaidi ikiwemo kutaka kulipua vituo vya mafuta, mikusanyiko ya Watu, kukata miti na kuisambaza barabarani.

Mbali na Mbowe wengine kwenye kesi hiyo ni waliokuwa Walinzi wake, Halfan Bwire Hassan, Adam Hassan Kasekwa na Mohamed Abdallah Ling'wenya ambapo wamesomewa mashitaka hayo leo Jumatatu, tarehe 23 Agosti 2021, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam.

Mashtaka hayo ni pamoja na kula njama za kutenda ugaidi ambapo Mbowe anatuhumiwa kufadhili vitendo hivyo vya kulipua vituo vya mafuta kwa kutoa zaidi ya shilingi laki sita, pia Watuhumiwa wote wanatuhumiwa kushiriki vikao vya kutenda kosa la ugaidi huku Mshtakiwa wa pili anatuhumiwa kumiliki bastola yenye risasi tatu kwa ajili ya kutenda kosa la ugaidi huku Mshtakiwa wa kwanza akituhumiwa kumiliki nguo, begi na koti zote za Jeshi la Wananchi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).
Screenshot_20210823-145224_GBInsta.jpg
 
Mbunge wa Kawe, Askofu Josephat Gwajima amefika Bungeni Dodoma muda huu kuitikia wito uliomtaka kufika mbele ya Kamati ya Maadili na Madaraka ya Bunge ili kujibu tuhuma mbalimbali ikiwemo kusema uongo na kushusha hadhi na heshima ya Bunge.
Screenshot_20210823-145409_GBInsta.jpg
 
Dereva wa Lori la mizigo lililokua likitoka Dar es salaam kuelekea nchini Zambia amepata majeraha kidogo baada ya Lori alilokuwa akiliendesha kupinduka maeneo ya Kimara Dar es salaam na kusababisha foleni karibu na eneo la ajali, akiongea na Ayo TV Dereva huyo amesema chanzo cha ajali ni kumkwepa bodaboda ambapo Trela ndio likayumba na kusababisha lori hilo kuanguka, Polisi wamewataka Madereva kuangalia njia mbadala wakati jitihada za kuliinua lori zinaendelea.
Screenshot_20210823-145548_GBInsta.jpg
Screenshot_20210823-145605_GBInsta.jpg
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa amethibitisha kutokea kwa ajali leo asubuhi katika eneo la Kwa Mbonde, Kata ya Picha ya Ndege, Kibaha baada ya Basi la Sauli ambalo lilikuwa linatokea Dar es salaam kwenda Tunduma kuacha njia na kutoka nje ya barabara kama mita kumi kisha likagonga Scania lililobeba mchanga.

RPC Nyigesa amesema Watu wanne wamepata michubuko kutokana na ajali hiyo na kufikishwa Tumbi Hospitali ambako wametibiwa na kuruhusiwa.

“Chanzo cha ajali hiyo ni Dereva wa Sauli kuyapita magari mengine bila kuchukua tahadhari(Wrong Overtaking) akaacha Barabara Wataalamu wanaita kuchochora, majeruhi kwenye ajali hiyo ni wanne na wote wametibiwa na kuruhusiwa” ———Nyigesa.
Screenshot_20210823-145733_GBInsta.jpg
Screenshot_20210823-145749_GBInsta.jpg
 
Kesi ya Mbowe, wenzake yahamishiwa Mahakama Kuuu
Hadija Jumanne, Mwananchi
Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na wenzake watatu, wamesomewa maelezo ya mashahidi na vielelezo na kesi yao imefungwa rasmi Mahakama ya Kisutu na kuhamishiwa Mahakama Kuu kwa ajili ya kusikilizwa.

Uamuzi huo umetolewa leo Jumatatu Agosti 23, 2021 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama, hiyo Thomas Simba baada ya washtakiwa kusomewa maelezo ya mashahidi na vielelezo.

Hata hivyo upande wa mashtaka unatarajia kuwa na mashahidi 24 na vielelezo 19 kuthibitisha mashtaka dhidi ya washtakiwa hao
Screenshot_20210823-150041_GBInsta.jpg
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla leo Augosti 23, 2021 amekabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Mkoa wa Lindi baada ya mwenge huo kukamilisha zoezi la uzinduzi na uwekaji mawe ya msingi kwenye miradi ya maendeleo iliyogharimu zaidi ya Sh105 bilioni
Screenshot_20210823-150403_GBInsta.jpg
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha imetupilia mbali pingamizi lililowasilishwa na mawakili wa utetezi wanaomuwakilisha mshitakiwa wa pili Sylivester Nyegu katika kesi ya unyang'anyi wa kutumia silaha inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili.

Uamuzi huo umetolewa leo Agosti 23, 2021 na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Odira Amworo ambaye aliahirisha shauri hilo la jinai namba 105, 2021 mwishoni mwa wiki baada ya Mawakili Edmund Ngemela na Sylvester Kahunduka kuweka pingamizi
Screenshot_20210823-150509_GBInsta.jpg
 
Yanga wamekatika kambi yao nchini Morocco, timu inarejea nyumbani. Sababu kadhaa zimetajwa kufikia hatua hiyo ya kusitisha kambi yao ya maandalizi.

1. Idadi kubwa ya wachezaji kuitwa kwenye timu za taifa.

2. Baadhi ya wachezaji kukutwa na maambukizi ya Corona na kuwekwa karantini [haijathibitishwa na uongozi wa Yanga].

Nimejaribu kutafuta ukweli kutoka kwa uongozi wa Yanga juu ya haya yanayozungumzwa, bahati nzuri kiongozi mmoja ambaye yupo na timu amenithibitishia kwamba ni kweli wamesitisha kambi na baadhi ya wachezaji na viongozi wanarejea leo.

Lakini kuna kundi jingine la wachezaji na viongozi watabaki Morona watarejea baadae [Agosti 27]. Taarifa niliyopewa ni kwamba kuna sababu za kiuongozi ambazo zipo nje ya uwezo wao.
Screenshot_20210823-151041_GBInsta.jpg
 
farhan jr

CRISTIANO RONALDO NA SIMULIZI YA ALBERT FANTRAU

Kwanza kabisa chukua Biblia, kisha fungua LUKA 10:2 "Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache Kwa hivyo, mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake"

Tafsiri fupi ni kuwa mavuno ni mengi ila Watenda kazi ni wachache! Tusahau kidogo kuhusu rejea hiyo, ikiwa imetimu saa 5:32 Asubuhi kwa saa za Afrika Mashariki, ikiwa sawa na saa 3:32 Asubuhi Lisbon Ureno

Stori inarudi nyuma miaka ya 90! Visiwani huko Madeira, nyumbani kwa Cristiano Ronaldo! Jioni moja ya upepo mkali wa bahari ya Atlantic, juu ya milima ya volcano kuna mbungi itapigwa

Lakini kabla hawajaingia kwenye mechi kuna Scout mmoja aliwaita vijana wawili mbele ya Kocha wao! Akamuita Cristiano Ronaldo na fundi mali mwingine anaitwa Albert Fantrau, akawatazama kwanza kwa tabasamu

Kisha akawaambia nimetoka mbali huko Lisbon! Nimekuja visiwani kuwatazama ubora wenu, nimepata masimulizi yenu kuhusu miguu kama ya Eusebio na utashi kama Luis Figo, ila mimi nitaondoka na mmoja kati yenu, atakaefunga mabao mengi kuliko mwenzie

Ronaldo na Fantrau wakaingia uwanjani huku wakijua mmoja tu atapata nafasi ya kuondoka! Mechi ilipoanza ni Cristiano Ronaldo alianza kuweka bao la kwanza, kisha Fantrau akaweka chuma ya pili

Tayari mzani umebalance! Scout anatazama mechi, ilipigwa pande zuri kwa Fantrau akawachukua mabeki kisha Kipa, Cristiano alikuwa kwa kasi nae anasogea! Fantrau alipomuona CR7 akampa pande, Ronaldo akaweka chuma ya tatu (bao lake la pili)

Ronaldo kwa mshangao akamtazama Albert na kumuuliza, kwanini amempa yeye afunge? Kifupi Fantrau akasema "Ronaldo wewe ni bora zaidi yangu, nenda kapambane" Ronaldo aliondoka kupitia hapo

Lakini miaka mingi baadae Fantrau kwasasa anaishi maisha anayotaka, anakula bata zote kutokana na Ronaldo anaemfadhili Rafiki yake kwa kila kitu, amelipa vyema fadhila
Screenshot_20210823-151248_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom